MAKALA hii imeandaliwa maalum ili iweze kutumika katika kipindi cha redio za Kiswahili ulimwenguni.
Lengo lake ni kutathmini maendeleo na matatizo ya demokrasia Afrika katika kipindi cha takriban miaka 20 hivi. Na hili linaweza kufanywa vizuri zaidi kama litafanyika kwa njia ya mjadiliano ndani ya studio kwa ushirikiano na mwandishi na mabingwa au wanataaluma wa demokrasia popote pale walipo duniani.
Mwandishi amejaribu kuainisha maeneo kama 19 hivi ambayo anadhani kuna matatizo na kama yakishughulikiwa ipasavyo basi Afrika inaweza kuwa na demokrasia safi na bora zaidi.
Muda wa kujadili mada hizi kwa ukamilifu na kwa undani zaidi unapendekezwa kuwa kati ya wiki nane na wiki 14.
Muundo wa kipindi utaanza kwa walioko studio kusoma sura moja au mbili kwenye Blogi na kisha kuanza kujadili kwa kuvuta mawazo ya wasikilizaji na wachangiaji kwenye yale yanayotakiwa kufikiwa mwisho wa kipindi kwa maana wote kukubaliana kwamba hilo ni tatizo na njia zilizopendekezwa zinafaa au hata pia kuongeza mawazo juu ya kibunifu kuhusu ufumbuzi wa tatizo au matatizo yaliyozungumzwa.
Sehemu ya pili itahusika zaidi na kupata ufafanuzi wa mawazo ya mwandishi na nini hasa ujumbe wake katika sehemu husika.
Sehemu ya tatu itakuwa ni kuachia jopo la wataalamu kuchangia mawazo yao kwa kukosoa au kuongeza vipengee vipya vitakavyochangia kuifanya blogi hii kuboreshwa zaidi kwa malengo ya hatimaye kuwa na kijitabu kuhusu DEMOKRASIA NA AFRIKA baada ya miaka 20.
Sammy Makilla
Barua-pepe: smakilla@out.ac.tz+255-732-929832
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment