Sunday, June 15, 2008

17. Demokrasia, fedha za wafadhili na wawekezaji

HALI ilivyo sasa ni kuwa wanaofaidika sana na fedha za wafadhili na wawekezaji ni wale walioko makao makuu ya nchi.

Endapo mikoa itakuwa na fursa ya kuendesha mambo yake ya uchumi na kijamii ni wazi kuwa fedha nyingi tu za wafadhili na wawekezaji sasa hazitaishia Dar es salaam bali zitamiminika kwa kiasi cha kutosha mahitaji ya mikoa na kanda mbalimbali nchini.

Katika mtazamo wa kisekta uliogusiwa mahala fulani katika makala hizi inaaminika kuwa Tanzania inaweza kugawanya katika kanda zinazofaa kuendeleza:. Katika uvuvi, kilimo cha umwagiliaji maji na utalii wa kando ya bahari na biashara ya kimataifa.. Katika utalii wa wanyama na sura ya nchim, kilimo maalum, elimu, tiba na huduma za afya.. Katika ufugaji na uuzaji nyama, ngozi, maziwa na mboji.. Katika kilimo cha nafaka, utalii wa kando ya maziwa.. Katika kilimo cha mboga, maua, matunda na viwanda vya usindikaji vyakula.. Katika uchimbaji madini, teknolojia nyeti, utengenezaji vito na urembo.

Bila shaka kila mkoa nchini unaweza ukajikita katika kile unachokiona una nafasi ya kufanya vizuri sana na kuhakikisha watu wake wananufaika sasa na sio baada ya WAO kwisha kufa.

Haya hayawezi kupatikana kwa urahisi kama demokrasia haitiririki hadi mkoani na watu wakawa na kiongozi wanayemchagua, bunge lao dogo na wizara zinazofanya kazi ya kuleta maendeleo haraka katika mazingira yao kwa kutumia mbinu na ubunifu wa asili wa wakazi wao.
***

No comments: