MAHAKAMA ni mhimili muhimu katika taifa linaloamini katika demokrasia.
Jaji Mkuu kama kiongozi wa kitaifa ana haki sawa na Rais au Waziri Mkuu au Spika au Kiongozi yeyote wa chama cha kisiasa kilicho madarakani.
Wote wanaaminiwa na umma kufanya kazi zao si kwa faida yao binafsi bali kwa faida ya taifa na wananchi wake.
Haifai kabisa kiongozi yeyote au mtu yeyote kusababisha mahakama na uongozi wake kufanya kazi kwa upendeleo kwa sababu za kifedha au ksiasa au kimadaraka.
Kwa sababu ya hili tunaamini kuwa ni vyema Jaji Mkuu akachaguliwa na bunge kwa umoja wake na kupitishwa na rais na sio vinginevyo.
Kufanya hivyo ni kuhakikisha kuwa Jaji Mkuu anawajibika kwa wananchi kupitia kwa wabunge waliowachagua na sio kwa mtu fulani aliyeko madarakani kwa wakati huo.
Endapo, Tanzania, itafanikiwa katika hili sio tu nchi itakuwa na heshima bali tarafu nzima ya sheria na unasheria Afrika itapata heshima kubwa itakayoihakikishia Tanzania nafasi ya uongozi Afrika.
Ni lazima wanasheria wetu waone mbali zaidi ya kuwa wanasheria hapa nchini kwa maana kwamba wafikiriwe kuwa majaji katika mahakama za Afrika Mashariki, Afrika na dunia kama ndio kigezo kikuu cha kufanikiwa kitaaluma.
***
Sunday, June 15, 2008
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment