Sunday, June 15, 2008

7. Demokraia, unyanyasaji wakulima, wanafunzi na vijana

KWA KUKOSA ajenda zinazoeleweka katika kilimo, elimu na ajira wakati mwingine nchi zetu zimeishia pengine bila kujua kufanya maisha yawe magumu sana kwa wakulima, wanafunzi na vijana kwa ujumla.

Ukiangalia kwa undani utakuta katika taasisi zote hizi kuna udikteta unaojificha na unaotumia fursa hiyo kulinda ubinafsi wao na sio kutetea maslahi ya umma mkubwa ulio chini yao.

Ni laizma tubuni mifumo inayofaa kuhakikisha kwamba viongozi katika kata, mashule, vyuo na taasisi zingine wanafanya mambo yao kwa uwazi na kwa namna ambayo inagundua dalili za kuzuka matatizo mapema kabla haayajalipuka na hivyo kuweza kufanya maamuzi yayakayoepusha mizozo na migongano isiyo ya lazima.

Ni lazima tujitahidi kutenga kati ya masuala ya kisiasa na yale ya kiuchumi na kijamii [ikiwemo elimu] ili kuhakikisha mtu hakwazi katika azma zake za maisha na siasa au wanasiasa au mashabiki wa wanasiasa fulani. Ni lazima pia tutenge urafiki na kazi. Na kutoa kazi kwa wale tu ambao wanaimudu kazi hiyo kwa kujenga mazingira yote yanayokubalika kwa watu wa aina zote na kwa shughuli za aina zote.

Katika miaka hii ambayo tuna wataalamu wengi mara kadhaa ukilinganisha na hali ilivyokuwa huko nyuma kwanini tushindwe kuwa na wataalamu wa menejimenti na oganaizesheni wanaoweza kutushauri njia bora za kuendesha kata, vijiji au shulena vyuo kwa namna ambayo ni nadra kuzuka migogoro isiyo ya lazima?
***

No comments: