Umuhimu wa kiongozi mkuu wa nchi
Upo ushahidi tosha kwamba nchi au kampuni hutegemea sana uwezo, nia, sababu, visheni, msimamo na mwelekeo wa kiongozi wake mkuu.
Kiongozi huyo akiwa anaona mbali na mbele; ana nia ya kweli ya kuwajenga watu wake, ana wasaidizi wenye uwezo na wanaofaa, anajua anachokifanya na anajituma kwa moyo wake wote huweza kufanikisha malengo mengi yaliyoko mbele yake.
Kiongozi huyo akiwa kinyume cha hapo juu, yaani sio mtu mwenye kuona mbali na mbele, sio mwenye uwezo, sio mwenye nia ya kweli ya kuwatumikia watu wake, hana visheni na katawaliwa na ubinafsi wa hali ya juu, choyo, husuda, tamaa na mambo kama hayo hawezi kuipeleka nchi au kampuni popote pale. Sana sana atairudisha nyuma miaka kadhaa kama sio kuimaliza kabisa.
Aidha kiongozi ambaye hana sifa njema za uongozi huweza kuwa mateka wa wafanyabiashara, wanasiasa na wanajamii wengine waliomweka madarakani. Kwa namna hii, hata maamuzi na utendaji wake huyumbishwa kwa matakwa ya wafadhili wake.
Ndivyo ilivyo katika kazi ya kukuza na kuimarisha demokrasia katika nchi. Kiongozi wa juu asipokuwa na nia, sababu na uwezo wa kuitetea na kujienga demokrasia katika nchi yake basi ujenzi wa demokrasia katika nchi inakuwa ni sawa na kupanda kilima kirefu na chenye hatari ya kila aina njiani.
Hapa Afrika kama kweli wakuu wetu wa nchi wana nia ya kujenga demokrasia ya kweli na ya kudumu kazi hii itakuwa rahisi na itafanyika kwa kasi kuliko inavyofanyika hivi sasa.
Ukiangalia kwa mapana na marefu kitabu hiki kinaonesha kuna mambo kadhaa ambayo yakifanyika basi nchi za Kiafrika zitakuwa mfano wa kuigwa na nchi nyingine duniani.
Mambo hayo ni pamoja na kuwa na Katiba inayoendana na Mfumo tuliomo. Aidha Tume Huru ya Uchaguzi, Utawala wa Sheria ndani ya Mfumo wa Vyama Vingi na Haki za Binadamu kwa mapana na marefu.
Vyombo vya Habari huru, wagombea huru, Kutobibiwa kwa fedha za umma Hazina na vyma vya siasa, Viongozi wa nchi na watumishi wenye nia, sababu na uwezo wa kujenga demokrasia ya kudumu na iliyo hai wakati wote na inayofanya kazi iliyokusudiwa na waasisi wa mfumo huu.
Mambo mengine ni ushirikishwaji watu katika maamuzi kwa vitendo na sio kwa maneno, Kasi ya Maamuzi na Utekelezaji wake na Uwajibikaji kwa wote.
Demokrasia pia haiwezi kujengwa kwa dhati kwenye nchi yenye umasikini na njaa kali. Katika hali kama hii matajiri watatumia mali zao kuvuruga sio tu demokrasia bali pia mfumo wa kichumi na kisiasa wa nchi.
Kiongozi huonesha njia wengine wakafuata
Sasa tuoneshe kwanini tunasema kuwa kama kiongozi wa nchi ana nia, uwezo na sababu ya kukubali na kuiachia demokrasia ifanye kazi nchini basi kukua na kuimarika demokrasia katika nchi inakuwa ni jambo rahisi. Na hili tunalisema katika hali ya unyonge kwa sababu viongozi wetu leo wamejigeuza kuwa wao ni mabwana na sisi ni watwana wao. Kwa hiyo hata kama tunataka jambo na wao hawataki pamoja na wingi wetu wanaweza kulikataa hilo jambo nasi tusiwe na lolote la kufanya.
Ikiwa kiongozi wa nchi anaamua kwamba kweli kutokana na mabadiliko makubwa ya kijamii, kiuchumi na kisiasa yaliyotokea nchini basi nchi inahitaji katiba mpya basi mara moja nchi nzima itarindima kwa sauti moja ya kukubalika kuwepo kwa katiba mpya. Kama kiongozi huyo anaona katiba mpya ni hatari kwake na kwa chama chake cha siasa na wapambe wake atakataa na ndio mwanzo wa demokrasia kupiga maktaimu hadi maamuzi sahihi yafanyike.
Hivyo ndivyo ilivyo kwa Tume Huru ya Uchaguzi na Wagombea huru. Yeye kiongozi mkuu akikubali tu haya tayari yatafanyika. Akikataa hakuna kitakachofanyika. Demokrasia itaendelea kusinyaa na kuwa na utapiamlo wa kujitakia.
Iwapo mkuu wa nchi atavikataza vyombo vya dola kujifanya mabwana na kuanza kuwanyanyasa watu kutokana na itikadi zao hilo halitafanyika. Akikaa kimya polisi kinyume na inavyotakiwa watajiona wao mabwana na kuanza kuwaonea na kuwanyima watu uhuru na haki zao za msingi.
Kiongozi bora hawezi kuuza au kununua haki za watu wake ziwe zile za uhuru wa kuamua wanachotaka au zile za kisiasa kwa kulea ujinga na umasikini. Atavipiga vitu hivi ili kuhakikisha watu wanakuwa huru ili waikuze na kuipanua demokrasia kutokana na uhuru huo.
Kiongozi mkuu akikataa kupakwa mafuta kwa mgongo wa chupa na vyombo vya habari vya nchi na akavisifu vinavyosema ukweli siku zote na kuvikebehi vinavyompaka 'goldstar' au 'coral' waziwazi basi msingi wa kuwa na vyombo vya habari huru utajengwa, tena haraka sana.
Ndivyo ilivyo pia kwa watumishi wa umma. Kama kiongozi mkuu anakemea wao kufanya kazi zao kwa kukiogopa chama fulani basi yaliyotokea na yanatokea kwenye Hazina za nchi hayawezi kutokea. Na fedha ya wananchi itakuwa salama hata kama chama fulani kinaondolewa madarakani. Kinyume chake kila baada ya uchaguzi mkuu wanaoingia madarakani wataikuta hazina haina kitu.
Ni kiongozi mkuu pia anayeweza kuzuia ubia usio mtakatifu kati ya wafanyabiashara, hazina na mangimeza wa serikali unaoziingiza nchi katika matatizo ya kila aina kila mwaka.
Kiongozi Mkuu akijua kuwa wizara ni vyombo vya kurahisisha uzalishaji mali na utoaji huduma hawezi kuunda baraza la watu 30 au zaidi ili kuwapendeza na kuwatafutia kazi waliomuunga mkono. Badala yake ataunda Baraza dogo la Mawaziri na kuweka mkakati wa kuzifanya kazi nyingine za serikali kuwa zinafanyika kwa gharama fulani kwa watumiaji na hivyo kupunguza kwa kiasi kikubwa gharama za uendesheja serikali.
Haiyumkiniki kukosa demokrasia ndani ya chama chochote na kisha utegemee kwamba viongozi wa chama hicho hicho watatekeleza majukumu ya kidemokrasia kitaifa. Demokrasia huanzia ndani ya chama, kinyume cha hivyo ni longolongo tu.
Kiongozi wa nchi akijua kwamba kuwepo kwa demokrasia kutarahisisha kazi yake ya kujenga uchumi, utamaduni na jamii bora na imara basi shughuli zote za kimaendeleo katika nchi zinakuwa nyepesi zaidi.
Kiongozi wa nchi kama anatumia hekima na busara katika vita vya kuwatoa wananchi kutokana na umasikini, ujinga na maradhi anaweza akachangia kwa kiasi kikubwa kuwepo kwa msingi imara wa demokrasia. Jambo hili likifanyika, hata hivyo, kisiasa kwa ajili ya kupata umaarufu wa papo kwa hapo linaweza kuichimbua demokrasia na kuigeuza miguu juu, kichwa chini.
Mambo ya msingi kuzingatia
Kwa maneno mengine kuna mambo ya msingi ya kuzingatia kabla ya kukuza na kuimarisha demokrasia nchini. Mambo hayo ni pamoja na kutosheleza mahitaji ya msingi ya wananchi, matumizi ya lugha mama katika nchi kwa mapana na marefu, madaraka walipo watu, matumizi ya Teknohama katika kila sekta na hata ile ya kisiasa, haki za binadamu na tathmini za kazi za watu na kujua mchango wa kila mtu katika maendeleo ya nchi. Haya yakiwepo na kuzingatiwa wakati wote basi yumkini nchi inakuwa katika nafasi nzuri zaidi ya kukuza na kuendeleza demokrasia katika maeneo mbalimbali ya kijamii, kisiasa na kiuchumi.
Haya yote ni mambo yaliyo ndani ya uwezo wa kiongozi wa nchi. Tathmini ya kiongozi yeyote kwa hiyo katika suala lal ujenzi wa demokrasia itafanyika kwa kuoanisha alichokifanya au kukizuia katika ujenzi wa demokrasia nchini mwake. Kiongozi anayekuwa kizingiti cha kukua demokrasia hawezi kuwa kiongozi safi na bora. Lakini upo uwezekano mkubwa kwa kiongozi anayekuwa chachu ya kukua demokrasia nchini mwake kuwa kiongozi safi na bora.
Kiongozi anayejiaminisha kwamba demokrasia ipo na hakuna tena la kufanya katika kuiboresha demokrasia hii atatambulika kwa hicho alichokuwa. Nacho sio kingine ila mgando wa demokrasia kwa kipindi fulani, yaani, ule muda anaokuwa madarakani.
Na hata kama kiongozi huyo hatawafanyia watu makubwa lakini akafanikisha kusimamisha tu misingi imara ya demokrasia basi kwa vyovyote vile watu na nchi yake watamheshimu na kumpa kiti cha juu katika kumbukumbu zao na historia yao.
Nchi hupata viongozi wa kila aina kadri miaka inavyopita. Hata hivyo, unaweza kugawa viongozi wa nchi katika vipindi vyote katika makundi matatu makubwa; Kwanza, kuna viongozi wanaoingia na kutoka madarakani bila kuleta tofauati yoyote katika maisha ya jamii na nchi -ni kama vile hawakuwepo; Pili, kuna viongozi wanaoingia na hadi kutoka madarakani huwa wameibomoa na kuiparananyisha kama sio kuisambaratisha nchi vibaya sana: na mwisho kuna viongozi wanaoingia na kutoka madarakani huku wakiiacha nchi imepiga hatua kadhaa mbele kimaendeleo.
Haya yote hutegemea kiongozi kaingi a madarakani kwa nia gani. Kama kiongozi huingia ili kujinufaisha yeye na jamaa zake tu basi ndio unapata aina zile mbili za kwanza. Na kama kiongozi kaingia ili kuwa endeleza watu na nchi yake ndipo unapopata ile aina ya mwisho.
Kwa kuhitimisha, pamoja na yote yaliyosemwa hatima ya nchi hutegemea sana kiongozi aliyeko madarakani. Akiwa anajua anachotaka na kule anakokwenda kama anavyojua watu wake wanachotaka na wanakotak kwenda bila kuyumbishwa wala kubabaishwa na watu wake basi nchi inaweza kupiga hatua kubwa ya kimaendeleo. Kiongozi huyo kama hajui anakokwenda na anafuata mkumbo tu basi maendeleo na ustawi huwa ni kitu adimu.
Monday, September 14, 2009
Sunday, July 26, 2009
DEMOKRASIA, TEKNOHAMA NA WIZI WA KURA
INDIA, taifa lenye kufuata demokrasia na lenye watu wengi kuliko mataifa mengine duniani yanayofuata demokrasia mwaka huu kwa mara ya kwanza liliweza kuendesha uchaguzi wake mkuu kwa kutumia TEKNOHAMA.
Nchi hiyo imedhihrisha inawezekana kabisa kuondoa mkono wa mtu unaolaumiwa sana kwa kupandikiza majina ya uongo katika daftari la wapiga kura, kutowaandikisha wapiga kura walio na haki ya kupiga kura, kuingiza kura za uongo, kuharibu na kupoteza kura za halali na mambo mengine kama hayo.
Jambo hili linaashiria kwamba ikiwa patakuwa na muundo na mfumo unaokubalika wa Katiba mpya katika mfumo wa vyama vingi na Tume Huru isiyoegemea upande mmoja na kisha kutumiwa TEKNOHAMA haki na usawa katika upigaji kura ni mambo yanayoweza kuwa kitu cha uhakika zaidi kuliko ilivyo sasa.
Katika nchi nyingi za Kiafrika kile kinachoitwa Tume ya Uchaguzi ni kiumbe cha chama tawala na seriklai yake. Ni zao la Katiba za viraka na ziizopitwa na wakati. Ni zao za sheria zilizopitwa na wakati na zisizokidhi matarajio ya ushindani wa kisiasa, soko huru na haki za binadamu.
Kwa kuwa wanaoongoza taasisi hizo ni watu wanaolishwa fadhila na chama tawala matokeo yake sikuzote ni kukisaidia na kukipendelea chama hicho kishinde hata pale kinapostahili kushindwa.
Uhakika wa kura ya mpiga kura kwenda kwa yule anayemtaka, Haki na Ukweli ni vitu vinavyowezekana endapo kutakuwa na upigaji kura kieletroniki.
Madhali nchi kama India imeshaanza kazi kama hii kinachotakiwa ni kwa chombo cha Umoja wa Mataifa kinachoshughulika na Demokrasia na Haki za Binadamu kuwa wakala wa kukodisha vifaa vya Teknohama toka India ili vitumike wakati wa uchaguzi katika nchi mbalimbali za Kiafrika na dunia ya tatu kwa ujumla.
Vinginevyo, utafiti uendelee kufanyika zaidi ili kuja na mashine bora zaidi za kieletroniki zitakazoondoa kabisa wizi na ujanja wa aina nyingine wakati wa kupiga kura Afrika na duniani kote kwa ujumla.
Ikumbukwe kwamba WIZI NA RUSHWA KUBWA KULIKO ZOTE ni zile zinatokea wakati wa chaguzi katika nchi mbalimbali Afrika. Ukkomesha wizi na rushwa hii katika ngazi hiyo utakuwa umelisaidia bara hili sio haba.
Nini kifanyike
Serikali ya India ambayo kwa sasa iko karibu na nchi za Kiafrika kuliko wakati wowote uko nyuma inaweza kuanza kwa kuwaalika wanasiasa na vijana wa vyama mbalimbali vya kisiasa kwenda India ili kupata mafunzo ya muda mfupi kuhusu upigaji kura kielektroniki. Huko watajifunza kwa nadharia na vitendo na hivyo kutambua uboa na udhaifu wa njia hiyo ya kupiga kura. Endapo wataona ni jambo linaloifaa Tanzania basi bila shaka watakuwa na hamasa ya kuja kulieleza, kulieneza na kulifanya likubalike hapa Afrika kwa urahisi.
Kama shabiki wa Teknohama nimekuwa nikijiuliza hivi kuna uwezekano wa kuwa na sanduku la kura lenye kutumia betri na linaloweza sio tu kupokea kura bali kuhakikisha halikubali kura mbaya na kisha kupiga hesabu ndani kwa ndani na kuonesha kwenye skrini juu yake kila mgombea kapata kura ngapi? Kisha boksi hilo liwe na uwezo wa kutuma majibu hayo kioto kwenda kwenye kompyuta kuu ya uchaguzi kiwilaya, kimkoa na kitaifa ?
Boksi hilo litakuwa na uwezo pia wa kuainisha vidole vya mpiga kura na kama namba yake inaendana na alama hiyo anakubalika na kama sivyo anakataliwa?
Simu za Mkononi
Kuna wanaofikiria pia upo uwezekano wa kutumia simu za mkononi maalum au za kawaida katika uchaguzi mkuu na upigaji kura wakati wowote.
Simu maalum za kupiga kura zitakuwa ni simu ambazo zinatumika kwa ajili hiyo tu na taifa litawajibika kumnunulia kila mpigaji kura simu yake kutokana na kodi za wananchi. Simu hiyo itanunuliwa mara moja tu katika maisha ya mtu. Na wale wanaokufa zitarekebishwa ili wapewe wapigaji kura wapya wanaoingia kwenye orodha ya wapiga kura baada ya kutimiza umri wao.
Aidha kwa simu za kawaida baada ya wananchi kuandikisha simu zao zote itachaguliwa namba moja mama itakayokubalika katika kupiga kura na masuala mengine ya kijamii na kiuchumi katika mfumo maalum wa kurahisisha na kupanua matumizi ya simu za mkononi.
Kwa kutumia namba ya simu yako iliyoandikishwa na inayokubalika baada ya kila kitu kuthibitishwa utaweza kupiga kura yako ukiwa unastarehe nyumbani kwako bila ya kwenda mahala ukacheleweshwa, kunyeshewa na mvua na kuchomwa na jua bila ya sababu ya maana. Jambo hili sio tu litawapa nafuu kubwa wapiga kura lakini pia litachangia idadi kubwa ya watu kupiga kura wakati wowote upigaji kura unapohitajika bila ya kugonja miaka mitano.
Itakuwa ni rahisi pia kufanya chaguzi ndogo kwa sababu gharama yake itakuwa ni ile tu ya uratibu na mawasiliano.
Kwa kifupi, Waafrika ambao ndio wanaokabiliwa na tatizo hili la wizi wa kura wanastahili kuwa mstari wa mbele kutafuta ufumbuzi wake. Mawazo haya ninaamini yanaweza yasifae au kukubalika lakini lengo langu la kuamsha mjadala kama Teknohama inaweza kutusaidia kuwa na chaguzi za huru, haki na zenye ukweli zaidi litakuwa limefanikiwa.
Nchi hiyo imedhihrisha inawezekana kabisa kuondoa mkono wa mtu unaolaumiwa sana kwa kupandikiza majina ya uongo katika daftari la wapiga kura, kutowaandikisha wapiga kura walio na haki ya kupiga kura, kuingiza kura za uongo, kuharibu na kupoteza kura za halali na mambo mengine kama hayo.
Jambo hili linaashiria kwamba ikiwa patakuwa na muundo na mfumo unaokubalika wa Katiba mpya katika mfumo wa vyama vingi na Tume Huru isiyoegemea upande mmoja na kisha kutumiwa TEKNOHAMA haki na usawa katika upigaji kura ni mambo yanayoweza kuwa kitu cha uhakika zaidi kuliko ilivyo sasa.
Katika nchi nyingi za Kiafrika kile kinachoitwa Tume ya Uchaguzi ni kiumbe cha chama tawala na seriklai yake. Ni zao la Katiba za viraka na ziizopitwa na wakati. Ni zao za sheria zilizopitwa na wakati na zisizokidhi matarajio ya ushindani wa kisiasa, soko huru na haki za binadamu.
Kwa kuwa wanaoongoza taasisi hizo ni watu wanaolishwa fadhila na chama tawala matokeo yake sikuzote ni kukisaidia na kukipendelea chama hicho kishinde hata pale kinapostahili kushindwa.
Uhakika wa kura ya mpiga kura kwenda kwa yule anayemtaka, Haki na Ukweli ni vitu vinavyowezekana endapo kutakuwa na upigaji kura kieletroniki.
Madhali nchi kama India imeshaanza kazi kama hii kinachotakiwa ni kwa chombo cha Umoja wa Mataifa kinachoshughulika na Demokrasia na Haki za Binadamu kuwa wakala wa kukodisha vifaa vya Teknohama toka India ili vitumike wakati wa uchaguzi katika nchi mbalimbali za Kiafrika na dunia ya tatu kwa ujumla.
Vinginevyo, utafiti uendelee kufanyika zaidi ili kuja na mashine bora zaidi za kieletroniki zitakazoondoa kabisa wizi na ujanja wa aina nyingine wakati wa kupiga kura Afrika na duniani kote kwa ujumla.
Ikumbukwe kwamba WIZI NA RUSHWA KUBWA KULIKO ZOTE ni zile zinatokea wakati wa chaguzi katika nchi mbalimbali Afrika. Ukkomesha wizi na rushwa hii katika ngazi hiyo utakuwa umelisaidia bara hili sio haba.
Nini kifanyike
Serikali ya India ambayo kwa sasa iko karibu na nchi za Kiafrika kuliko wakati wowote uko nyuma inaweza kuanza kwa kuwaalika wanasiasa na vijana wa vyama mbalimbali vya kisiasa kwenda India ili kupata mafunzo ya muda mfupi kuhusu upigaji kura kielektroniki. Huko watajifunza kwa nadharia na vitendo na hivyo kutambua uboa na udhaifu wa njia hiyo ya kupiga kura. Endapo wataona ni jambo linaloifaa Tanzania basi bila shaka watakuwa na hamasa ya kuja kulieleza, kulieneza na kulifanya likubalike hapa Afrika kwa urahisi.
Kama shabiki wa Teknohama nimekuwa nikijiuliza hivi kuna uwezekano wa kuwa na sanduku la kura lenye kutumia betri na linaloweza sio tu kupokea kura bali kuhakikisha halikubali kura mbaya na kisha kupiga hesabu ndani kwa ndani na kuonesha kwenye skrini juu yake kila mgombea kapata kura ngapi? Kisha boksi hilo liwe na uwezo wa kutuma majibu hayo kioto kwenda kwenye kompyuta kuu ya uchaguzi kiwilaya, kimkoa na kitaifa ?
Boksi hilo litakuwa na uwezo pia wa kuainisha vidole vya mpiga kura na kama namba yake inaendana na alama hiyo anakubalika na kama sivyo anakataliwa?
Simu za Mkononi
Kuna wanaofikiria pia upo uwezekano wa kutumia simu za mkononi maalum au za kawaida katika uchaguzi mkuu na upigaji kura wakati wowote.
Simu maalum za kupiga kura zitakuwa ni simu ambazo zinatumika kwa ajili hiyo tu na taifa litawajibika kumnunulia kila mpigaji kura simu yake kutokana na kodi za wananchi. Simu hiyo itanunuliwa mara moja tu katika maisha ya mtu. Na wale wanaokufa zitarekebishwa ili wapewe wapigaji kura wapya wanaoingia kwenye orodha ya wapiga kura baada ya kutimiza umri wao.
Aidha kwa simu za kawaida baada ya wananchi kuandikisha simu zao zote itachaguliwa namba moja mama itakayokubalika katika kupiga kura na masuala mengine ya kijamii na kiuchumi katika mfumo maalum wa kurahisisha na kupanua matumizi ya simu za mkononi.
Kwa kutumia namba ya simu yako iliyoandikishwa na inayokubalika baada ya kila kitu kuthibitishwa utaweza kupiga kura yako ukiwa unastarehe nyumbani kwako bila ya kwenda mahala ukacheleweshwa, kunyeshewa na mvua na kuchomwa na jua bila ya sababu ya maana. Jambo hili sio tu litawapa nafuu kubwa wapiga kura lakini pia litachangia idadi kubwa ya watu kupiga kura wakati wowote upigaji kura unapohitajika bila ya kugonja miaka mitano.
Itakuwa ni rahisi pia kufanya chaguzi ndogo kwa sababu gharama yake itakuwa ni ile tu ya uratibu na mawasiliano.
Kwa kifupi, Waafrika ambao ndio wanaokabiliwa na tatizo hili la wizi wa kura wanastahili kuwa mstari wa mbele kutafuta ufumbuzi wake. Mawazo haya ninaamini yanaweza yasifae au kukubalika lakini lengo langu la kuamsha mjadala kama Teknohama inaweza kutusaidia kuwa na chaguzi za huru, haki na zenye ukweli zaidi litakuwa limefanikiwa.
DEMOKRASIA NA TAASISI ZA KIJAMII NA KIIMANI
MWAKA 1961 Tanzania ilipopata uhuru kulikuwa na vikundi huru kadhaa vikishughulika na mambo mbalimbali kuanzia maslahi ya ukoo, mtaa na kabila. Taasisi nyingi zilizokuwepo zilikuwa kwa ajili ya kutoa huduma na msaada kwa makundi fulani ya kikabila, kieneo, kidini, kibiashara,kikazi na kiuzalishaji mali.
Miaka michache baadaye chama cha TANU kikaitangaza nchi hi ni ya chama kimoja. Makundi mengi ya kijamii na kiuchumi yakanyimwa haki na uhuru wa kufanya kazi zao za kuisaidia jamii au wanasiasa wakaingizwa kwenye makundi hayo ambao badala ya kujenga walivibomoa na kuvimalizia mbali kabisa.
Mbadala ukawa ni chama cha TANU na baadaye CCM kulazimisha watu wote waliotaka maendeleo na neema kujiunga na makundi maalum yaliyoanzishwa kwa nia, sababu na maguvu ya kukifanya chama hicho kiwe na nguvu na uwezo kuliko sehemu yoyote ya jamii katika nchi hii.
Makundi hayo ni pamoja na yale ya vijana,wanawake, wazee/wazazi, wafanyakazi, wanafunzi na kadhalika. Huu ukawa mwanzo wa kile ambacho leo tunaita ubaguzi wa kichama au kisiasa ambao ni ile hali ya chama tawala kutumia mabavu ili kujinufaisha na kuwanufaisha wale wanaokiunga mkono katika masuala mbalimbali ya kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni. Wengi watakumbuka kwamba ili mtu kuwa na uhakika wa kupata fursa ya kuendelea na masomo ulipaswa uwe na kadi ya TANU/CCM au vinginevyo ulikuwa huna njia nyingine ya kujiendeleza. Hili limekwisha kiuwaziwazi lakini bado liko kimafichomaficho.
Demokrasia ya kweli na inayofanya kazi haiwezi kuwepo kama kuna chama chochote cha siasa kinachotumia fursa ya kuwa chama kinachosimamia serikali kisha kuviamuru vyombo vya dola kubeza, kudharau, kupiga vita, kuvinyonya na kuvitendea isivyo haki vikundi vya kijamii visivyo na unasaba na chama tawala na jumuiya zake.
Ni muhimu kwa vijana, wanafunzi, wanawake, wazee, wafanyakazi, wanavijijini, wakulima, wafanyabiashara, watumishi wa umma na wengineo wawe na haki ya kuunda, kuanzisha na kuendeleza kikundi chochote cha kijamii na kiuchumi ambacho wanaamini kitakuwa na manufaa kwao na kwa jamaa zao na kwa jamii yao mtaani au kijijini.
Isipokuwa hivyo basi kutakuwa na mifukuto na migogoro na mioto ya chini kwa chini isiyoisha katika makundi ya kijamii ambayo badala ya kuchangia maendeleo ya watu vitakuwa ni vitu vinavyohujumu na kupoteza fursa mbalimbali za maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Mathalani, katiba inaruhusu haki ya kila mtu kuwa na uhuru wa kiimani na kuabudu. Kwa mapana yake na marefu ni kwamba raia yeyote wa nchi hii ana haki ya kukataa au kukubali kujiunga na kundi hili au lile katika masuala ya imani, dini na ibada. Na ni mwiko kwa serikali yoyote, iliyopo madarakani na zitakazokuja kupora na kupoka haki ya dini yoyote ile katika kukubali au kukataa taasisi fulani. Ni haki ya kidemokrasia ya mwananchi pia kuanzisha, kujenga na kuendeleza taasisi mpya endapo haridhiki au hakubaliani na zile zilizopo.
Hili linadhihirisha kwa wabunge na mawaziri wetu kwamba yale yanayofanyika leo katika kuinyima sehemu fulani ya jamii haki zao kwa upande mmoja lakini wakati huo huo kwa upande mwingine wabunge na mawaziri hao kuipa sehemu nyingine sio tu haki zao tu bali na ziada isiyodaiwa pia.
Huku hakuwezi kutafsiriwa kwa namna nyingine ila ni dhuluma na uonevu kwa yale makundi yanayonyimwa haki na maslahi yao mchana kweupe.
Aidha kitendo cha kuwa na bodi au mamlaka kuwalangua wakulima na kuwakatisha tamaa katika shughuli zao za kilimo hakutafsiriki kwa njia nyingine yoyote ile ila ni wizi wa jasho la mkulina na dhuluma na uonevu kwa waliomo katika sekta ya ukulima, uvuvi na ufugaji. Haki hapa ni kwa watu hawa kuwezeshwa kama wenye viwanda walivyowezeshwa kuzalisha na kuuza wao wenyewe kile wanachokizalsha.
Wafanyakazi wanapoamua hili au lile ili kupigania haki na maslahi yao na kisha kuingiliwa na mahakama au polisi pia hakuwezi kutafisrika kwa njia nyingine yoyote ile ila ni dhuluma na uonevu kwa wafanyakazi wa nchi hii. Mfanyakazi mmoja mmoja na kwa pamoja wana haki saa yoyote, wakati wowote na mahala popote kuonesha kutoridhika na hali ilivyo au uamuzi fulani na ni ruksa kwao kukutana, kuandamana, kupinga na kuonesha kilio na kutoridhika kwao.
Wachimbaji madini wana haki ya kidemokrasia ya kutafuta riziki yao ya kila siku. Na pale mgodi unapopewa ardhi ambayo wachimbaji wadogo ndipo walipokuwa wakipatia riziki yao wachimbaji hao wadogo wana kila haki ya kulipwa fidia ya kutosheleza riziki yao ya kila siku kwa miaka yao ya uhai iliyobakia.
Kinachofanyika sasa sio tu ni mauaji yanayobarikiwa na wakubwa, dhuluma na uonevu bali unyang'anyi wa mali ya Mtanzania unaofanywa na wageni toka nje.
Kuna wanojiuliza hivi haki ya wanawake kuwa na makundi yao ni kwa CCM tu. Huu sio ubaguzi wa kijinsia kwa wanawake wasiokuwa wanachama wa chama fulani na kilichoshika pochi la taifa ? Kwanini tulilikataa Baraza la Wanawake wa Tanzania lilikosudiwa kuwa mwamvuli wa makundi ya aina yote ya wanawake katika jamii yetu. Hivi tunaamini kuna kundi la wanawake katika nchi hii wanaostahili kuneemeka wao peke yao na neema mbalimbali zinazokuja Tanzania toka ndani na nje ya nchi ?.
Vijana kuanzia Arusha hadi Zanzibar wameachwa kwenye mataa na watawala waliopo. Maana vijana wenye maana ni wale wa chama tawala tu. Kutokana na hili wale wasiokipenda chama hicho wana wakati mgumu katika kujikwamua kiuchumi na kijamii. Je, hili ni sawa. Na kweli katiba inayovumilia jambo hili ni katiba yenye haki, usawa na uhuru kwa watu wote ?
Utengwaji huu wa vijana kutokana na ubaguzi wa kisiasa au kichama umechangia sio haba kwa Zanzibar kuwa na 'teja' kwa karibu kila familia visiwani humo.
Kutokana na kundi la Wazee lililokuwepo kuwa na mwegemeo wa kisiasa kuna wazee kadhaa waliodhulumiwa na wanaoishi maisha ya dhiki na ya umasikini mkubwa leo lakini kundi hilo la wazee la kichama sio tu haliwajulii hali bali pia halina mpango wa kuwasikiliza achilia mbali kuwasaidia katika kupigania haki zao. Tunalojifunza hapa ni umuhimu wa wazee wa kila eneo kuwa na chombo chao kwa ajili ya kupigania haki na maslahi zao wakingali hai na sio pale wanapokwishakufa. Wazee wa kisiasa wakati wa sakata la wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki walikaa kimya kama hilo jambo haliwahusu kabisa. Lakini ni vyema hapa wazee tukakumbushana kwamba ukimuona mwenzio ananyolewa na wewe tia kcihwa chako maji.
Wanafunzi nao wanasukwasukwa na kulazimishwa kuwa katika makundi maalum ambayo yanaishia kwa viongozi wake kushirikiana na wale wanaowakandamiza na hivyo kufanya shule na vyuo vyetu sikuzote viwanja vya migogoro na mapambano badala ya mahala vijana hao wanapoweza wakati mwingi kusaidia kufanya tafiti mbalimbali za kuiendeleza nchi hii na watu wake.
Faida za vikundi huru vya kijamii na kiimani
Kuna faida mbalimbali za kuwa na vikundi huru vya kijamii na kiuchumi katika nchi:
Kwanza, vinapanua wigo wa kutatua matatizo ya kijamii na kutumia fursa za kiuchumi na kijamii zilizopo kwa makundi mbalimbali ya watu katika jamii,
Vikundi huru vya jamii na hasa pale vinavyopewa nafasi ya uwakilishi vijijini,mjini, tarafani, wilayani , mikoani na kitaifa vinawezesha sauti ya kila mtu kusikika,
Ni njia ya uhakika na ya kuaminika zaidi ya kupanua, kuendeleza, kujenga na kuimarisha demokrasia katika ngazi ya chini ya taifa hadi ile ya juu kabisa,
Makundi huru ya jamii yanasaidia kuondoa kutawaliwa makundi na chama chochote cha siasa,
Vikundi huru vya jamii pia vinasaidia kuondoa kutumiwa kwa vikundi na wanasiasa kama ilivyofanyika kule Kenya, Zimbabwe na nchi nyingine za Kiafrika zinazobeza, kudumaza na kulemaza demokrasia,
Vikundi kama hivi vinasaidia pia kupunguza rushwa na hongo za kisiasa kwa kuwa vinajenga uwezo wa watu kujikidhi wao wenyewe mahitaji yao yote ya msingi na kinachobakia kwao sio njaa na ukata bali ni kutafuta kuendelea juu zaidi,
Vikudni vya kijamii vikijiingiza katika miradi ya ujasiriamali jamii vina uwezo mkubwa pia wa kutoa ajira kabakaba kwa vijana, wanawake na hata wazee wasiokuwa na kazi,
Vikudni vya jamii vina uwezo mkubwa wa kuchangia katika kuendeleza rasilimal watu bila hili kuwa na ila au njama ya aina yoyote ile kwa vikundi vingine katika jamii tofauti ilivyo na pale dini fulani inapotaka kupora kazi hii toka serikalini na kuifanya wao,
Vikudni vya kijamii vinavyofanya kazi na vinavyojua wajibu wao na Utaifa na Uzalendo wao vina kila sababu ya kuzuia wanasiasa na wafadhili toka nje kuwatumia viongozi wa makundi fulani,
Aidha ni vikundi hivi aghalabu vinavyovuka upofu na uoni mfupi wa viongozi wasiojua taradadi na tarajali za jamii ndivyo vinavyoweza kuzuia Taasisi za kidini kutumia ombwe linaloachwa na Serikali dhaifu ili kudhulumu dini nyingine katika masuala ya elimu, afya na huduma za jamii.
Fedha ya mlipa kodi itumike kupeleka demokrasia vijijini na sio kuiua demokrasia vijijini.
Miaka michache baadaye chama cha TANU kikaitangaza nchi hi ni ya chama kimoja. Makundi mengi ya kijamii na kiuchumi yakanyimwa haki na uhuru wa kufanya kazi zao za kuisaidia jamii au wanasiasa wakaingizwa kwenye makundi hayo ambao badala ya kujenga walivibomoa na kuvimalizia mbali kabisa.
Mbadala ukawa ni chama cha TANU na baadaye CCM kulazimisha watu wote waliotaka maendeleo na neema kujiunga na makundi maalum yaliyoanzishwa kwa nia, sababu na maguvu ya kukifanya chama hicho kiwe na nguvu na uwezo kuliko sehemu yoyote ya jamii katika nchi hii.
Makundi hayo ni pamoja na yale ya vijana,wanawake, wazee/wazazi, wafanyakazi, wanafunzi na kadhalika. Huu ukawa mwanzo wa kile ambacho leo tunaita ubaguzi wa kichama au kisiasa ambao ni ile hali ya chama tawala kutumia mabavu ili kujinufaisha na kuwanufaisha wale wanaokiunga mkono katika masuala mbalimbali ya kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni. Wengi watakumbuka kwamba ili mtu kuwa na uhakika wa kupata fursa ya kuendelea na masomo ulipaswa uwe na kadi ya TANU/CCM au vinginevyo ulikuwa huna njia nyingine ya kujiendeleza. Hili limekwisha kiuwaziwazi lakini bado liko kimafichomaficho.
Demokrasia ya kweli na inayofanya kazi haiwezi kuwepo kama kuna chama chochote cha siasa kinachotumia fursa ya kuwa chama kinachosimamia serikali kisha kuviamuru vyombo vya dola kubeza, kudharau, kupiga vita, kuvinyonya na kuvitendea isivyo haki vikundi vya kijamii visivyo na unasaba na chama tawala na jumuiya zake.
Ni muhimu kwa vijana, wanafunzi, wanawake, wazee, wafanyakazi, wanavijijini, wakulima, wafanyabiashara, watumishi wa umma na wengineo wawe na haki ya kuunda, kuanzisha na kuendeleza kikundi chochote cha kijamii na kiuchumi ambacho wanaamini kitakuwa na manufaa kwao na kwa jamaa zao na kwa jamii yao mtaani au kijijini.
Isipokuwa hivyo basi kutakuwa na mifukuto na migogoro na mioto ya chini kwa chini isiyoisha katika makundi ya kijamii ambayo badala ya kuchangia maendeleo ya watu vitakuwa ni vitu vinavyohujumu na kupoteza fursa mbalimbali za maendeleo ya kijamii na kiuchumi.
Mathalani, katiba inaruhusu haki ya kila mtu kuwa na uhuru wa kiimani na kuabudu. Kwa mapana yake na marefu ni kwamba raia yeyote wa nchi hii ana haki ya kukataa au kukubali kujiunga na kundi hili au lile katika masuala ya imani, dini na ibada. Na ni mwiko kwa serikali yoyote, iliyopo madarakani na zitakazokuja kupora na kupoka haki ya dini yoyote ile katika kukubali au kukataa taasisi fulani. Ni haki ya kidemokrasia ya mwananchi pia kuanzisha, kujenga na kuendeleza taasisi mpya endapo haridhiki au hakubaliani na zile zilizopo.
Hili linadhihirisha kwa wabunge na mawaziri wetu kwamba yale yanayofanyika leo katika kuinyima sehemu fulani ya jamii haki zao kwa upande mmoja lakini wakati huo huo kwa upande mwingine wabunge na mawaziri hao kuipa sehemu nyingine sio tu haki zao tu bali na ziada isiyodaiwa pia.
Huku hakuwezi kutafsiriwa kwa namna nyingine ila ni dhuluma na uonevu kwa yale makundi yanayonyimwa haki na maslahi yao mchana kweupe.
Aidha kitendo cha kuwa na bodi au mamlaka kuwalangua wakulima na kuwakatisha tamaa katika shughuli zao za kilimo hakutafsiriki kwa njia nyingine yoyote ile ila ni wizi wa jasho la mkulina na dhuluma na uonevu kwa waliomo katika sekta ya ukulima, uvuvi na ufugaji. Haki hapa ni kwa watu hawa kuwezeshwa kama wenye viwanda walivyowezeshwa kuzalisha na kuuza wao wenyewe kile wanachokizalsha.
Wafanyakazi wanapoamua hili au lile ili kupigania haki na maslahi yao na kisha kuingiliwa na mahakama au polisi pia hakuwezi kutafisrika kwa njia nyingine yoyote ile ila ni dhuluma na uonevu kwa wafanyakazi wa nchi hii. Mfanyakazi mmoja mmoja na kwa pamoja wana haki saa yoyote, wakati wowote na mahala popote kuonesha kutoridhika na hali ilivyo au uamuzi fulani na ni ruksa kwao kukutana, kuandamana, kupinga na kuonesha kilio na kutoridhika kwao.
Wachimbaji madini wana haki ya kidemokrasia ya kutafuta riziki yao ya kila siku. Na pale mgodi unapopewa ardhi ambayo wachimbaji wadogo ndipo walipokuwa wakipatia riziki yao wachimbaji hao wadogo wana kila haki ya kulipwa fidia ya kutosheleza riziki yao ya kila siku kwa miaka yao ya uhai iliyobakia.
Kinachofanyika sasa sio tu ni mauaji yanayobarikiwa na wakubwa, dhuluma na uonevu bali unyang'anyi wa mali ya Mtanzania unaofanywa na wageni toka nje.
Kuna wanojiuliza hivi haki ya wanawake kuwa na makundi yao ni kwa CCM tu. Huu sio ubaguzi wa kijinsia kwa wanawake wasiokuwa wanachama wa chama fulani na kilichoshika pochi la taifa ? Kwanini tulilikataa Baraza la Wanawake wa Tanzania lilikosudiwa kuwa mwamvuli wa makundi ya aina yote ya wanawake katika jamii yetu. Hivi tunaamini kuna kundi la wanawake katika nchi hii wanaostahili kuneemeka wao peke yao na neema mbalimbali zinazokuja Tanzania toka ndani na nje ya nchi ?.
Vijana kuanzia Arusha hadi Zanzibar wameachwa kwenye mataa na watawala waliopo. Maana vijana wenye maana ni wale wa chama tawala tu. Kutokana na hili wale wasiokipenda chama hicho wana wakati mgumu katika kujikwamua kiuchumi na kijamii. Je, hili ni sawa. Na kweli katiba inayovumilia jambo hili ni katiba yenye haki, usawa na uhuru kwa watu wote ?
Utengwaji huu wa vijana kutokana na ubaguzi wa kisiasa au kichama umechangia sio haba kwa Zanzibar kuwa na 'teja' kwa karibu kila familia visiwani humo.
Kutokana na kundi la Wazee lililokuwepo kuwa na mwegemeo wa kisiasa kuna wazee kadhaa waliodhulumiwa na wanaoishi maisha ya dhiki na ya umasikini mkubwa leo lakini kundi hilo la wazee la kichama sio tu haliwajulii hali bali pia halina mpango wa kuwasikiliza achilia mbali kuwasaidia katika kupigania haki zao. Tunalojifunza hapa ni umuhimu wa wazee wa kila eneo kuwa na chombo chao kwa ajili ya kupigania haki na maslahi zao wakingali hai na sio pale wanapokwishakufa. Wazee wa kisiasa wakati wa sakata la wastaafu wa Jumuiya ya Afrika Mashariki walikaa kimya kama hilo jambo haliwahusu kabisa. Lakini ni vyema hapa wazee tukakumbushana kwamba ukimuona mwenzio ananyolewa na wewe tia kcihwa chako maji.
Wanafunzi nao wanasukwasukwa na kulazimishwa kuwa katika makundi maalum ambayo yanaishia kwa viongozi wake kushirikiana na wale wanaowakandamiza na hivyo kufanya shule na vyuo vyetu sikuzote viwanja vya migogoro na mapambano badala ya mahala vijana hao wanapoweza wakati mwingi kusaidia kufanya tafiti mbalimbali za kuiendeleza nchi hii na watu wake.
Faida za vikundi huru vya kijamii na kiimani
Kuna faida mbalimbali za kuwa na vikundi huru vya kijamii na kiuchumi katika nchi:
Kwanza, vinapanua wigo wa kutatua matatizo ya kijamii na kutumia fursa za kiuchumi na kijamii zilizopo kwa makundi mbalimbali ya watu katika jamii,
Vikundi huru vya jamii na hasa pale vinavyopewa nafasi ya uwakilishi vijijini,mjini, tarafani, wilayani , mikoani na kitaifa vinawezesha sauti ya kila mtu kusikika,
Ni njia ya uhakika na ya kuaminika zaidi ya kupanua, kuendeleza, kujenga na kuimarisha demokrasia katika ngazi ya chini ya taifa hadi ile ya juu kabisa,
Makundi huru ya jamii yanasaidia kuondoa kutawaliwa makundi na chama chochote cha siasa,
Vikundi huru vya jamii pia vinasaidia kuondoa kutumiwa kwa vikundi na wanasiasa kama ilivyofanyika kule Kenya, Zimbabwe na nchi nyingine za Kiafrika zinazobeza, kudumaza na kulemaza demokrasia,
Vikundi kama hivi vinasaidia pia kupunguza rushwa na hongo za kisiasa kwa kuwa vinajenga uwezo wa watu kujikidhi wao wenyewe mahitaji yao yote ya msingi na kinachobakia kwao sio njaa na ukata bali ni kutafuta kuendelea juu zaidi,
Vikudni vya kijamii vikijiingiza katika miradi ya ujasiriamali jamii vina uwezo mkubwa pia wa kutoa ajira kabakaba kwa vijana, wanawake na hata wazee wasiokuwa na kazi,
Vikudni vya jamii vina uwezo mkubwa wa kuchangia katika kuendeleza rasilimal watu bila hili kuwa na ila au njama ya aina yoyote ile kwa vikundi vingine katika jamii tofauti ilivyo na pale dini fulani inapotaka kupora kazi hii toka serikalini na kuifanya wao,
Vikudni vya kijamii vinavyofanya kazi na vinavyojua wajibu wao na Utaifa na Uzalendo wao vina kila sababu ya kuzuia wanasiasa na wafadhili toka nje kuwatumia viongozi wa makundi fulani,
Aidha ni vikundi hivi aghalabu vinavyovuka upofu na uoni mfupi wa viongozi wasiojua taradadi na tarajali za jamii ndivyo vinavyoweza kuzuia Taasisi za kidini kutumia ombwe linaloachwa na Serikali dhaifu ili kudhulumu dini nyingine katika masuala ya elimu, afya na huduma za jamii.
Fedha ya mlipa kodi itumike kupeleka demokrasia vijijini na sio kuiua demokrasia vijijini.
Sunday, July 12, 2009
DEMOKRASIA NA UHURU WA KIUCHUMI NA KIJAMII KWA MAENEO NA WATU
AFRIKA ya leo sio ya jana. Huko nyuma wananchi katika nchi nyingi za Kiafrika waliwachukulia viongozi wao kama vile viongozi hao walikuwa BABA zao. Na viongozi hao waliona raha kuitwa baba wa taifa au baba wa hili au lile. Ingawa kwa kiasi kikubwa ni wachache sana kati yao walioweza kutimiza wajibu wao kama baba. Baba alitarajiwa kuwafanyia wananchi (wanawe hata kama wa kufikia) yale yaliyo ya baraka, heri na wema wa dhati toka ndani ya moyo wa mtu. Baba alitakiwa kuwa kielelezo cha utu na ubinadamu. Haikutarajiwa hata siku moja kuwa baba atakuja geuka kuwa mtu anayependelea kati ya wanawe; atawaibia wanawe; atawadhulumu wanawe; atawasingizia uongo wa kutupwa wanawe; atawanyanyasa na kuwatesa wanawe; hatafanza ubaguzi kati ya wanawe; atawagandamiza wanawe; atawadhulumu wanawe; atawaonea na hata kuwaua wanawe.
Kwa bahati mbaya BABA wa jana na wa leo Afrika anayafanya madhambi haya hapo juu kila siku. Na mwananchi amechanganyikiwa na anajiuliza amwamini na amtegemee nani sasa.
Tatizo kubwa la Ubaba ni lile la kutaka kusimamia NYUMBA KUBWA YENYE VYUMBA ZAIDI YA 50 AU SHAMBA LA HEKTA ELFU lakini wewe unajua na unatumia tu vyumba viwili au vitatu katika jumba hilo au moja ya nane ya hekta katika shamba hilo.
Kinachotokea kwingine huna habari nayo. Labda uletewe na mtu habari. Na mjumbe huyo mara nyingi huleta uongo au habari za kupkwa. Na wewe kwa kuwa huna muda aghalabu utakuwa unaukubali uongo kuwa ukweli. Matokeo yake mpaka funza anatoka kwenye dole huku kaacha watoto milioni mwilini mwako ndio unagutuka, ala, kumbe kidoleni kuna mama wa mafunza!
Uhuru wa Mikoa na Demokrasia
Wapigania demokrasia hawataki uhuru wa mikoa eti kwa sababu wanataka kuigawa nchi au kuvunja umoja na mshikamano katika nchi. Mungu aepushilie mbali hayo. Wanataka uhuru kwa mikoa ili tujenge umoja na mshikamano imara zaidi kutokana na kutumika kikamilifu fursa za kiuchumi na kijamii zilizoko katika kila mkoa. Mikoa kama inakosa ubunifu na ujasiriamali na utundu wa kujaribu mambo mapya na ikazalisha kidogo basi keki ya taifa inakuwa ndogo. Mikoa ikijititimua na kuzalisha zaidi na keki ya taifa nayo inakuwa kubwa kila siku.
Na uhuru wa kiuchumi na kijamii hauwezi kupatikana kupitia meza ya katibu mkuu wa wizara ya serikali za mitaa au wizara kama hiyo. Uhuru wa mkoa unapatikana kwa njia moja tu. Kila mkoa kuendesha uchaguzi wa kumchagua Gavana wake au Kiongozi wao wa mkoa, wawakilishi wao na wajumbe wao wa ngazi za chini. Gavana atachagua mionngoni mwa wabunge wa mkoa husika mawaziri wa serikali itakayosimamia masuala ya uchumi na jamii ya mkoa husika. Kwa kitendo cha siku moja safari ndefu ya kuwa na mikoa inayojiendesha kiuchumi na kijamii itakuwa imeanza. Kwa saini moja tu ya Mkuu wa nchi demokrasia itakuwa imesimika mizizi ya kweli kuanzia vijijini na miji katika kila mkoa. Kwa sheria moja tu toka bunge la taifa kila mkoa utakuwa na wawakilishi wake wanaojua ni wapi kiatu kinafinya na wanaozungumzia kila kwenye kikao matatizo na ufumbuzi wa matatizo ya wananchi wanaowawakilisha na sio porojo, umbeya, uzushi na ngonjera zisizo kwisha.
Ipo hatari pia ya kujilimbikizia mamlaka iwe yale ya kisiasa, kiuchumi, kirasilimali au kifedha.
Badala ya kutumika vyema aghalabu hutapanywa. Na hiki ndicho kinachotokea kutokana na sakata ya B.O.T., EPA, baadhi ya dini kugawana fedha za wafadhili na serikali na kashfa nyingine katika wizara, taasisi na mashirika mbalimbali ya kiuchumi na kijamii nchini.
Kwa kuwa nchi ni kubwa na watu ni wengi vibilioni mia au mia mbili au mia tatu ikivigawa vinakuwa havina uwezo wa kubadili maisha ya yeyote ila kwa yule mchotaji anayewahi kutoka na tonge kubwa kabla hicho kilichotolewa hakijaanza hata kugawiwa.
Kinachotakikana hapa sio fedha bali uhuru wa kiuchumi na kijamii kwa wananchi huko huko mikoani na majimboni walipo kukaa chini na kuweka mipango na mikakati yao ya maendeleo na kukusanya nguvu zao za mwili na za kifedha kuleta mabadiliko yanayoweza kukifanya kidogo kuwa sio tu kikubwa bali kinachojizalisha na kujiendeleza chenyewe na hivyo kuwahakikishia wakazi wa mtaa, kata, tarafa, wilaya au mkoa maendeleo endelevu. Kinyume cha hivyo kama nchi ilivyo tegemezi kwa wafadhili basi mikoa nayo itaendelea kuwa tegemezi kwa serikali na kuwa vipofu kwa fursa pekee za kiuchumi wanazoweza kuzitumia wao wenyewe na kuondokana na utegemezi huu unaotulemaza na kutudamaza takriban karibu miaka hamsini kufikia sasa.
Demokrasia ya kweli
Demokrasia ya kweli itatokana tu na kila Mkoa kuwa na Gavana au kiongozi wake wa kumchagua na sio wa kupachikwa na chama chochote cha kisiasa kiwacho au serikali iliyoko madarakani. Kazi za serikali ni kusimamia wizara kisiasa na kiutawala na sio kusimamia mikoa kiuchumi na kijamii.
Kazi ya kusimamia maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya mkoa inastahili kufanywa na Gavana wa mkoa, mawaziri wa mkoa na wabunge wa mkoa. Hawa wamevaa kiatu husika na wanajua kinachofinya. Vinginevyo kazi hii ikifanywa katika ngazi za wizara, basi tutaishia kila waziri kutaka kupeleka miradi yote ya wizara yake katika mkoa wake kama sio jimbo lake la uchaguzi.
Gavana wa mkoa hatakuwa muuza siasa na sera bali mtendaji mkuu wa kiuchumi na kijamii. Mkoa utakuwa ni kampuni na yeye ni Mkurugenzi au Meneja Mkuu. Wakazi wa mkoa watategemea awe na mawaziri wa vitendo na sio wa maneno. Kama kuna waziri wa maji na umwagiliaji basi waziri huyo atahakikisha kila sehemu mkoani wanapata maji na kuna umwagiliaji maji. Kama ni waziri wa Viwanda na Biashara basi waziri huyo wa mkoa atahakikisha mkoa unapata wawekezaji ndani na nje ya nchi ili mkoa uwe na viwanda inavyovihitaji na vinavyoingiza faida na sio hasara au kugeuzwa kuwa maghofu au karakana au ghala za wafanyabiashara, wenye viwanda, taasisi zisizo za kiserikali na kadhalika.
Wabunge wa mkoa watakuwa ni wawakilishi wa maeneo ya watu kati ya 50,000 na laki mbili nao kazi yao kubwa itakuwa ni kuhakikisha sauti ya wananchi wake ndiyo inayotawala katika maamuzi na utekelezaji wowote wa masuala yanayohusu eneo lake. Jimbo lake litashindana na majimbo mengine mkoani kwa kuhakikisha wana rasilimali watu tosha, barabara nzuri, maji, umeme, mazingira bora kwa wawekezaji wa ndani na nje na vitu kama hivyo.
Kwa kufanya hivi kila jimbo, kila wilaya na kila mkoa utakuwa unapambana kuwaondoa watu wake toka kwenye umaskini unaowanyima haki yao ya kuchangia katika demokrasia na maendeleo ya kweli ya nchi na watu wake.
Katika hali tuliyonayo ambayo makosa ya serikali na yale ya wanasiasa yanaendelea kumasikinisha baadhi ya mikoa haitakuwa rahisi kujenga na kuimarisha demokrasia katika maeneo mengi katika nchi zetu za Kiafrika.
Bila umasikini wa kutupwa kuondoka itakuwa ni ndoto kutarajia kujengwa kwa demokrasia ya kweli na inayofanya kazi.
Hii ni demokrasia itakayoruhusu pamoja na mambo mengine mkulima kuuza mazao yake ndani na nje ya nchi; mvuvi kuuza samaki zake ndani na nje ya nchi; mwenye mali asili kama miti au madini kuuza alichokitafuta kwa gharama na kukipata ndani na nje ya nchi; Watanzania kuwa huru kufanya kazi au kwenda kucheza michezo nje ya nchi bila kuwekewa mikwara na mtu au taasisi yoyote.
Ni demokrasia ya kijamii na kiuchumi itakayowadhihirishia Watanzania kuwa anga ndio paa la matamanio na makusudio yao na yeyote anayewakwaza ni adui wa na adui wa taifa.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
Kwa bahati mbaya BABA wa jana na wa leo Afrika anayafanya madhambi haya hapo juu kila siku. Na mwananchi amechanganyikiwa na anajiuliza amwamini na amtegemee nani sasa.
Tatizo kubwa la Ubaba ni lile la kutaka kusimamia NYUMBA KUBWA YENYE VYUMBA ZAIDI YA 50 AU SHAMBA LA HEKTA ELFU lakini wewe unajua na unatumia tu vyumba viwili au vitatu katika jumba hilo au moja ya nane ya hekta katika shamba hilo.
Kinachotokea kwingine huna habari nayo. Labda uletewe na mtu habari. Na mjumbe huyo mara nyingi huleta uongo au habari za kupkwa. Na wewe kwa kuwa huna muda aghalabu utakuwa unaukubali uongo kuwa ukweli. Matokeo yake mpaka funza anatoka kwenye dole huku kaacha watoto milioni mwilini mwako ndio unagutuka, ala, kumbe kidoleni kuna mama wa mafunza!
Uhuru wa Mikoa na Demokrasia
Wapigania demokrasia hawataki uhuru wa mikoa eti kwa sababu wanataka kuigawa nchi au kuvunja umoja na mshikamano katika nchi. Mungu aepushilie mbali hayo. Wanataka uhuru kwa mikoa ili tujenge umoja na mshikamano imara zaidi kutokana na kutumika kikamilifu fursa za kiuchumi na kijamii zilizoko katika kila mkoa. Mikoa kama inakosa ubunifu na ujasiriamali na utundu wa kujaribu mambo mapya na ikazalisha kidogo basi keki ya taifa inakuwa ndogo. Mikoa ikijititimua na kuzalisha zaidi na keki ya taifa nayo inakuwa kubwa kila siku.
Na uhuru wa kiuchumi na kijamii hauwezi kupatikana kupitia meza ya katibu mkuu wa wizara ya serikali za mitaa au wizara kama hiyo. Uhuru wa mkoa unapatikana kwa njia moja tu. Kila mkoa kuendesha uchaguzi wa kumchagua Gavana wake au Kiongozi wao wa mkoa, wawakilishi wao na wajumbe wao wa ngazi za chini. Gavana atachagua mionngoni mwa wabunge wa mkoa husika mawaziri wa serikali itakayosimamia masuala ya uchumi na jamii ya mkoa husika. Kwa kitendo cha siku moja safari ndefu ya kuwa na mikoa inayojiendesha kiuchumi na kijamii itakuwa imeanza. Kwa saini moja tu ya Mkuu wa nchi demokrasia itakuwa imesimika mizizi ya kweli kuanzia vijijini na miji katika kila mkoa. Kwa sheria moja tu toka bunge la taifa kila mkoa utakuwa na wawakilishi wake wanaojua ni wapi kiatu kinafinya na wanaozungumzia kila kwenye kikao matatizo na ufumbuzi wa matatizo ya wananchi wanaowawakilisha na sio porojo, umbeya, uzushi na ngonjera zisizo kwisha.
Ipo hatari pia ya kujilimbikizia mamlaka iwe yale ya kisiasa, kiuchumi, kirasilimali au kifedha.
Badala ya kutumika vyema aghalabu hutapanywa. Na hiki ndicho kinachotokea kutokana na sakata ya B.O.T., EPA, baadhi ya dini kugawana fedha za wafadhili na serikali na kashfa nyingine katika wizara, taasisi na mashirika mbalimbali ya kiuchumi na kijamii nchini.
Kwa kuwa nchi ni kubwa na watu ni wengi vibilioni mia au mia mbili au mia tatu ikivigawa vinakuwa havina uwezo wa kubadili maisha ya yeyote ila kwa yule mchotaji anayewahi kutoka na tonge kubwa kabla hicho kilichotolewa hakijaanza hata kugawiwa.
Kinachotakikana hapa sio fedha bali uhuru wa kiuchumi na kijamii kwa wananchi huko huko mikoani na majimboni walipo kukaa chini na kuweka mipango na mikakati yao ya maendeleo na kukusanya nguvu zao za mwili na za kifedha kuleta mabadiliko yanayoweza kukifanya kidogo kuwa sio tu kikubwa bali kinachojizalisha na kujiendeleza chenyewe na hivyo kuwahakikishia wakazi wa mtaa, kata, tarafa, wilaya au mkoa maendeleo endelevu. Kinyume cha hivyo kama nchi ilivyo tegemezi kwa wafadhili basi mikoa nayo itaendelea kuwa tegemezi kwa serikali na kuwa vipofu kwa fursa pekee za kiuchumi wanazoweza kuzitumia wao wenyewe na kuondokana na utegemezi huu unaotulemaza na kutudamaza takriban karibu miaka hamsini kufikia sasa.
Demokrasia ya kweli
Demokrasia ya kweli itatokana tu na kila Mkoa kuwa na Gavana au kiongozi wake wa kumchagua na sio wa kupachikwa na chama chochote cha kisiasa kiwacho au serikali iliyoko madarakani. Kazi za serikali ni kusimamia wizara kisiasa na kiutawala na sio kusimamia mikoa kiuchumi na kijamii.
Kazi ya kusimamia maendeleo ya kiuchumi na kijamii ya mkoa inastahili kufanywa na Gavana wa mkoa, mawaziri wa mkoa na wabunge wa mkoa. Hawa wamevaa kiatu husika na wanajua kinachofinya. Vinginevyo kazi hii ikifanywa katika ngazi za wizara, basi tutaishia kila waziri kutaka kupeleka miradi yote ya wizara yake katika mkoa wake kama sio jimbo lake la uchaguzi.
Gavana wa mkoa hatakuwa muuza siasa na sera bali mtendaji mkuu wa kiuchumi na kijamii. Mkoa utakuwa ni kampuni na yeye ni Mkurugenzi au Meneja Mkuu. Wakazi wa mkoa watategemea awe na mawaziri wa vitendo na sio wa maneno. Kama kuna waziri wa maji na umwagiliaji basi waziri huyo atahakikisha kila sehemu mkoani wanapata maji na kuna umwagiliaji maji. Kama ni waziri wa Viwanda na Biashara basi waziri huyo wa mkoa atahakikisha mkoa unapata wawekezaji ndani na nje ya nchi ili mkoa uwe na viwanda inavyovihitaji na vinavyoingiza faida na sio hasara au kugeuzwa kuwa maghofu au karakana au ghala za wafanyabiashara, wenye viwanda, taasisi zisizo za kiserikali na kadhalika.
Wabunge wa mkoa watakuwa ni wawakilishi wa maeneo ya watu kati ya 50,000 na laki mbili nao kazi yao kubwa itakuwa ni kuhakikisha sauti ya wananchi wake ndiyo inayotawala katika maamuzi na utekelezaji wowote wa masuala yanayohusu eneo lake. Jimbo lake litashindana na majimbo mengine mkoani kwa kuhakikisha wana rasilimali watu tosha, barabara nzuri, maji, umeme, mazingira bora kwa wawekezaji wa ndani na nje na vitu kama hivyo.
Kwa kufanya hivi kila jimbo, kila wilaya na kila mkoa utakuwa unapambana kuwaondoa watu wake toka kwenye umaskini unaowanyima haki yao ya kuchangia katika demokrasia na maendeleo ya kweli ya nchi na watu wake.
Katika hali tuliyonayo ambayo makosa ya serikali na yale ya wanasiasa yanaendelea kumasikinisha baadhi ya mikoa haitakuwa rahisi kujenga na kuimarisha demokrasia katika maeneo mengi katika nchi zetu za Kiafrika.
Bila umasikini wa kutupwa kuondoka itakuwa ni ndoto kutarajia kujengwa kwa demokrasia ya kweli na inayofanya kazi.
Hii ni demokrasia itakayoruhusu pamoja na mambo mengine mkulima kuuza mazao yake ndani na nje ya nchi; mvuvi kuuza samaki zake ndani na nje ya nchi; mwenye mali asili kama miti au madini kuuza alichokitafuta kwa gharama na kukipata ndani na nje ya nchi; Watanzania kuwa huru kufanya kazi au kwenda kucheza michezo nje ya nchi bila kuwekewa mikwara na mtu au taasisi yoyote.
Ni demokrasia ya kijamii na kiuchumi itakayowadhihirishia Watanzania kuwa anga ndio paa la matamanio na makusudio yao na yeyote anayewakwaza ni adui wa na adui wa taifa.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
Saturday, July 11, 2009
DEMOKRASIA NA UWEZESHWAJI WA VYAMA VYA UPINZANI
HAIWEZEKANI kuwa na demokrasia ya kweli katika nchi nyingi za Kiafrika kutokana na nguvu kubwa iliyo nayo chama tawala ukilinganisha na udhaifu mkubwa wa vyama mbadala.
Kubwa zaidi ni kukosa uwezo wa kuwa na ofisi katika kila wilaya, mji na kijiji; pia kukosa uwezo wa kuwa na vyombo vya usafiri vinavyofaa na kutosheleza mahitaji yao; hali kadhalika, kuwa na fedha za kutosha kuwalipa baadhi ya watendaji wao ili washughulike na kazi moja tu ya kukijenga chama na uwezo wake wa kuchangia maendeleo ya nchi na watu wake.
Kwa sababu hii ninashauri watu wote ikiwemo wafadhili toka nchi za nje kwamba wakati umefika sasa wa kusaidia vyama mbadala kuwa na msingi bora na imara wa kuanza kushirikisha kikamilifu na kwa dhati katika siasa za vyama vingi nchini.
Ninapendekeza msaada huu usiwe ni sadaka bali ni mkopo wa riba nafuu na utakaolipwa baada ya miaka 20 au zaidi. Mikopo hiyo iwawezeshe wanasiasa na vyama vya siasa mbadala kujenga ofisi ambazo pia zitakuwa na vyumba au ghorofa za kukodishwa ili kuviingizia pato kila mwaka; vyombo vya usafiri na fedha za mbegu za kusimika vyema mizizi ya vyama hivyo hasa huko wilayani na vijijini.
Uhalali wa vyama mbadala kusaidiwa katika hili unatokana na ukweli huu hapa chini:
Vyama tawala vingi vilikuwa na miaka 35 au zaidi ya kujilimbikizia ukwasi na mali za kila aina wakati vyama mbadala havina zaidi ya miaka 10 toka vianze kutafuta wapi pa kuanzia. Isitoshe vyama tawala vinavibana vyama mbadala kwa kila hali ili visijenge na visiwe na uwezo kama wao wakijua fika kwamba kwa kuwaachia wapinzani kuwa na nguvu basi utakuwa ni msiba kwao. Kwa hiyo hatuwezi kutarajia serikali ya chama tawala fulani kusaidia kuimarisha chama cha upinzani waziwazi. Ingawa hili halizuii mtu mmoja mmoja katika chama tawala kusaidia chama hiki au kile mbadala kwa sababu moja au nyingine.
Aidha vyama vingi tawala kwa kupitia kisingizio cha ujamaa na utafa vilipora mali za wananchi na kuzifanya mali za chama. Hadi wa leo hakuna chama chochote tawala kilichokiri hili na kuzirudisha mali hizo ila pale ambapo chama hicho kimeondolewa madarakani na mahakama au wananchi wenyewe kudai na kunyakua kilichokuwa chao.
Vyama vingi tawala Afrika vimejenga nyufa na mianya makusudi ili kuiba fedha toka Hazina, bima, pensheni, mfuko wa usalama wa jamii, wizarani, serikali za mitaa na mashirika kama hayo kwa namna ambayo chama hakihusishwi kabisa na wizi huo ingawa kwa yakini mwizi ni chama na sio hao wanaotumiwa na wanasiasa na makuwadi wao wa fedha haramu wanazoibiwa wananchi wakiwemo wanyonge kama wazee, mayatima, wagonjwa, wanavijiji, walemavu na wengine kama hao.
Kwa kutumia mamlaka za kodi aidha vyama tawala katika nchi nyingi huwafanya wafanyabiashara na wenyeviwanda na wawekezaji ama kwa kupenda au kushawishiwa kiujanja au kulazimishwa au kwa kutoa rushwa kuvipatia fedha vyama hivyo kwa mihadi kwamba mali zao zitaongezeka pale chama kinaporudi madarakani.
Fedha nyingi ambazo vyama tawala vinapata hazitumiwi ili kuwaelewesha wananchi vijijini kwamba vyama vingi na demokrasia ni jambo zuri kwa nchi zetu bali hutumika kwa kazi kinyume cha hiyo. Aghalabu fedha hizo hutumika kuwaghilibu wananchi kwamba watakuwa maskini zaidi, wataingia katika matatizo makubwa na pengine hata watauawa wakichagua chama kingine kutawala nchi.
Ni vyama mbadala vichache sana ambavyo watumishi wake wana mishahara au uhakika wa kipato jambo ambalo ni tofauti kwa upande wa vyama tawala. Uhakika huu kwa vyama tawala unawapa watumishi wake jeuri, kiburi, tamaa na ulafi wa kupata zaidi na dharau ya kuwaburuza wananchi. Wakati unyonge huu unawapa watumishi wa vyama mbadala matende ya kuthubutu na kujaribu yale yanayoweza kuendeleza na kuimarisha upinzani nchini.
Hoja hizo hapo juu ni tosha kuonesha kwanini wazo la kuvisaidia vyama mbadala viwe na miguu yake vyenyewe ni suala muhimu na yakini ndio stata ya upinzani wa kweli katika nchi nyingi za Kiafrika.
Ili kukuza na kuimarisha demokrasia Afrika ni muhimu mambo haya yafanyike:
. Vyama mbadala viwezeshwa kuwa na majengo ya ofisi tarafani,wilayani, vijijini, kata, mitaani ili sio tu kuwa na makazi maalum yanayotambulika na kuheshimika lakini pia vyanzo vya mapato ya kila mwaka ya uhakika ili kuondokana na tamaa ya rushwa au misaada inayoua demokrasia badala ya kuijenga.
. Ni muhimu pia kwa kutambua ukubwa na upana wa nchi hii kwa vyama mbadala kupewa misaada na mikopo itakayowawezesha angalau kuwa na vyombo vya usafiri ambavyo vinaweza pia kukodishwa na kuingizia mapato chama wakati visipohitajika kwa shughuli za kichama.
. Ni muhimu watu kama Westminster Foundation for Democracy, George Soros Foundation, USIS na Umoja wa Mataifa kuangalia uwezekano wa kutoa mikopo au ruzuku katika miaka ya mwanzo ili angalau sehemu nyeti ya wafanyakazi wa vyama mbadala vya kisiasa kuwa wanalipwa mishahara.
. Hili liende sambamba na wahisani kusaidia kujenga uwezo wa menejimenti na utawala ili waweze kusimamia mambo yao kisayansi na sio kisanii.
. Hili linaweza kufanyika vizuri zaidi kama kila chama kitakuwa na mpango wa kuandaa 'Strategic Planning' yake kwa shughuli za ndani za kichama na ile ya kukikuza na kukiimarisha chama kitaifa.
Pamoja na mambo mengine Mpango huo wa Kimkakati utavisadia vyama hivyo kuwa na miundo na mifumo ya vyama isiyo na matatizo na inayokwenda na wakati.
Yumkini wanasiasa wengi wa vyama mbadala wanaonekama kama watu waliochanganyikiwa, wenye matatizo yasiyokwisha, masikini na watu wenye njaa kali sio kwa sababu vyama mbadala vinataka hivyo ila kwa sababu chama tawala na serikali vinafanya makusudi ili waonekane hivyo. Hii ni tofauti kabisa na huko Ulaya na nchi nyingine zilizoendelea kidemokrasia ambako viongozi wa vyama mbadala hawachukuliwi tofauti na wale wa vyama tawala kwa kiasi hicho.
Ni dhahiri basi kwamba endapo vyama mbadala vitapata mikopo au misaada ya kufanikisha mambo hayo hapo juu hawatashindwa kuwajulisha wananchi kwamba vyama vingi ni kitu kizuri kwao na sio jambo baya kama vile vyama tawala Afrika vinavyofanya lionekane kwa hivi sasa.
Mapendekezo yangu ni kwamba pawe na:
MFUKO WA KUWAJENGEA VYAMA MBADALA AU UPINZANI MISINGI IMARA YA USHINDANI WA KISIASA KATIKA NCHI ZA KIAFRIKA KAMA INAVYOFANYIKA HUKO ULAYA KWA MSAADA WA BW. GEORGE SOROS.
Mfuko huo utoe mikopo ya riba nafuu ili angalau vyama mbadala vijenge ofisi moja kubwa katika ngazi ya mkoa na moja kila wilaya na kisha ndogo ndogo kwa kila tarafa.
Ofisi zote zipatiwe vifaa na zana muhimu za kazi.
Wakopeshwe fedha za uendeshaji kwa miaka 3 na kisha baada ya hapo baada ya kufundisha jinsi ya kukodisha baadhi ya vyumba katika majengo yao mbinu za ujasiriamali jamii ili waweze kuendelea na kazi ya kujenga na kupanua vyama vyao wao wenyewe.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
Kubwa zaidi ni kukosa uwezo wa kuwa na ofisi katika kila wilaya, mji na kijiji; pia kukosa uwezo wa kuwa na vyombo vya usafiri vinavyofaa na kutosheleza mahitaji yao; hali kadhalika, kuwa na fedha za kutosha kuwalipa baadhi ya watendaji wao ili washughulike na kazi moja tu ya kukijenga chama na uwezo wake wa kuchangia maendeleo ya nchi na watu wake.
Kwa sababu hii ninashauri watu wote ikiwemo wafadhili toka nchi za nje kwamba wakati umefika sasa wa kusaidia vyama mbadala kuwa na msingi bora na imara wa kuanza kushirikisha kikamilifu na kwa dhati katika siasa za vyama vingi nchini.
Ninapendekeza msaada huu usiwe ni sadaka bali ni mkopo wa riba nafuu na utakaolipwa baada ya miaka 20 au zaidi. Mikopo hiyo iwawezeshe wanasiasa na vyama vya siasa mbadala kujenga ofisi ambazo pia zitakuwa na vyumba au ghorofa za kukodishwa ili kuviingizia pato kila mwaka; vyombo vya usafiri na fedha za mbegu za kusimika vyema mizizi ya vyama hivyo hasa huko wilayani na vijijini.
Uhalali wa vyama mbadala kusaidiwa katika hili unatokana na ukweli huu hapa chini:
Vyama tawala vingi vilikuwa na miaka 35 au zaidi ya kujilimbikizia ukwasi na mali za kila aina wakati vyama mbadala havina zaidi ya miaka 10 toka vianze kutafuta wapi pa kuanzia. Isitoshe vyama tawala vinavibana vyama mbadala kwa kila hali ili visijenge na visiwe na uwezo kama wao wakijua fika kwamba kwa kuwaachia wapinzani kuwa na nguvu basi utakuwa ni msiba kwao. Kwa hiyo hatuwezi kutarajia serikali ya chama tawala fulani kusaidia kuimarisha chama cha upinzani waziwazi. Ingawa hili halizuii mtu mmoja mmoja katika chama tawala kusaidia chama hiki au kile mbadala kwa sababu moja au nyingine.
Aidha vyama vingi tawala kwa kupitia kisingizio cha ujamaa na utafa vilipora mali za wananchi na kuzifanya mali za chama. Hadi wa leo hakuna chama chochote tawala kilichokiri hili na kuzirudisha mali hizo ila pale ambapo chama hicho kimeondolewa madarakani na mahakama au wananchi wenyewe kudai na kunyakua kilichokuwa chao.
Vyama vingi tawala Afrika vimejenga nyufa na mianya makusudi ili kuiba fedha toka Hazina, bima, pensheni, mfuko wa usalama wa jamii, wizarani, serikali za mitaa na mashirika kama hayo kwa namna ambayo chama hakihusishwi kabisa na wizi huo ingawa kwa yakini mwizi ni chama na sio hao wanaotumiwa na wanasiasa na makuwadi wao wa fedha haramu wanazoibiwa wananchi wakiwemo wanyonge kama wazee, mayatima, wagonjwa, wanavijiji, walemavu na wengine kama hao.
Kwa kutumia mamlaka za kodi aidha vyama tawala katika nchi nyingi huwafanya wafanyabiashara na wenyeviwanda na wawekezaji ama kwa kupenda au kushawishiwa kiujanja au kulazimishwa au kwa kutoa rushwa kuvipatia fedha vyama hivyo kwa mihadi kwamba mali zao zitaongezeka pale chama kinaporudi madarakani.
Fedha nyingi ambazo vyama tawala vinapata hazitumiwi ili kuwaelewesha wananchi vijijini kwamba vyama vingi na demokrasia ni jambo zuri kwa nchi zetu bali hutumika kwa kazi kinyume cha hiyo. Aghalabu fedha hizo hutumika kuwaghilibu wananchi kwamba watakuwa maskini zaidi, wataingia katika matatizo makubwa na pengine hata watauawa wakichagua chama kingine kutawala nchi.
Ni vyama mbadala vichache sana ambavyo watumishi wake wana mishahara au uhakika wa kipato jambo ambalo ni tofauti kwa upande wa vyama tawala. Uhakika huu kwa vyama tawala unawapa watumishi wake jeuri, kiburi, tamaa na ulafi wa kupata zaidi na dharau ya kuwaburuza wananchi. Wakati unyonge huu unawapa watumishi wa vyama mbadala matende ya kuthubutu na kujaribu yale yanayoweza kuendeleza na kuimarisha upinzani nchini.
Hoja hizo hapo juu ni tosha kuonesha kwanini wazo la kuvisaidia vyama mbadala viwe na miguu yake vyenyewe ni suala muhimu na yakini ndio stata ya upinzani wa kweli katika nchi nyingi za Kiafrika.
Ili kukuza na kuimarisha demokrasia Afrika ni muhimu mambo haya yafanyike:
. Vyama mbadala viwezeshwa kuwa na majengo ya ofisi tarafani,wilayani, vijijini, kata, mitaani ili sio tu kuwa na makazi maalum yanayotambulika na kuheshimika lakini pia vyanzo vya mapato ya kila mwaka ya uhakika ili kuondokana na tamaa ya rushwa au misaada inayoua demokrasia badala ya kuijenga.
. Ni muhimu pia kwa kutambua ukubwa na upana wa nchi hii kwa vyama mbadala kupewa misaada na mikopo itakayowawezesha angalau kuwa na vyombo vya usafiri ambavyo vinaweza pia kukodishwa na kuingizia mapato chama wakati visipohitajika kwa shughuli za kichama.
. Ni muhimu watu kama Westminster Foundation for Democracy, George Soros Foundation, USIS na Umoja wa Mataifa kuangalia uwezekano wa kutoa mikopo au ruzuku katika miaka ya mwanzo ili angalau sehemu nyeti ya wafanyakazi wa vyama mbadala vya kisiasa kuwa wanalipwa mishahara.
. Hili liende sambamba na wahisani kusaidia kujenga uwezo wa menejimenti na utawala ili waweze kusimamia mambo yao kisayansi na sio kisanii.
. Hili linaweza kufanyika vizuri zaidi kama kila chama kitakuwa na mpango wa kuandaa 'Strategic Planning' yake kwa shughuli za ndani za kichama na ile ya kukikuza na kukiimarisha chama kitaifa.
Pamoja na mambo mengine Mpango huo wa Kimkakati utavisadia vyama hivyo kuwa na miundo na mifumo ya vyama isiyo na matatizo na inayokwenda na wakati.
Yumkini wanasiasa wengi wa vyama mbadala wanaonekama kama watu waliochanganyikiwa, wenye matatizo yasiyokwisha, masikini na watu wenye njaa kali sio kwa sababu vyama mbadala vinataka hivyo ila kwa sababu chama tawala na serikali vinafanya makusudi ili waonekane hivyo. Hii ni tofauti kabisa na huko Ulaya na nchi nyingine zilizoendelea kidemokrasia ambako viongozi wa vyama mbadala hawachukuliwi tofauti na wale wa vyama tawala kwa kiasi hicho.
Ni dhahiri basi kwamba endapo vyama mbadala vitapata mikopo au misaada ya kufanikisha mambo hayo hapo juu hawatashindwa kuwajulisha wananchi kwamba vyama vingi ni kitu kizuri kwao na sio jambo baya kama vile vyama tawala Afrika vinavyofanya lionekane kwa hivi sasa.
Mapendekezo yangu ni kwamba pawe na:
MFUKO WA KUWAJENGEA VYAMA MBADALA AU UPINZANI MISINGI IMARA YA USHINDANI WA KISIASA KATIKA NCHI ZA KIAFRIKA KAMA INAVYOFANYIKA HUKO ULAYA KWA MSAADA WA BW. GEORGE SOROS.
Mfuko huo utoe mikopo ya riba nafuu ili angalau vyama mbadala vijenge ofisi moja kubwa katika ngazi ya mkoa na moja kila wilaya na kisha ndogo ndogo kwa kila tarafa.
Ofisi zote zipatiwe vifaa na zana muhimu za kazi.
Wakopeshwe fedha za uendeshaji kwa miaka 3 na kisha baada ya hapo baada ya kufundisha jinsi ya kukodisha baadhi ya vyumba katika majengo yao mbinu za ujasiriamali jamii ili waweze kuendelea na kazi ya kujenga na kupanua vyama vyao wao wenyewe.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
Saturday, June 27, 2009
DEMOKRASIA, UNDUGU NA UBAGUZI MPYA
Maana ya Undugu na Ubaguzi Mpya
Maana ya Undugu kwa muktadha huu ni pale mwanasiasa anapotumia nafasi aliyo nayo [akijua wake au chake haviwezi kukataliwa na wajumbe au wabunge-maana yeye ndiye anayewahakikishia kuwepo kwao na maslahi wanayopata, na kwa nafasi hiyo yeye kashika mpini na wanachama na wananchi kwa ujumla wameshika makali. ] kuwapa nafasi za kazi katika chama au serikali ndugu, watoto, wake, jamaa au marafiki zake. Undugu unapokithiri unamloga kiongozi kiasi cha kumfanya atake pia awe na sifa za kifalme falme, ikiwemo pia kurithisha uongozi kwa mwanae au yule amtakaye yeye na siyo yule wanayemtaka wanachama au wananchi. Na akiona anayemtaka hatakiwi anaweza akafanya yote yale ya kuwazaini na kuwatisha watu wake mpaka wakubali kumkubalia matakwa yake. Ingawa imekwishatokea pale watendaji wa chini wanapogundulika na viongozi wa juu kumpandikiza asiyetakikana kwa huyo aliyepandikizwa kuombwa kumuachia yule anayekubalika.
Wakati maana ya Ubaguzi wa aina mpya katika nchi nyingi za Kiafrika, Kiarabu na Kiasia
ni kuachiwa kuzuka kwa ubaguzi kati ya wananchi walio wanachama wa chama tawala na wale wasio wanachama wake. Hawa wanaweza kuwa wanachama wa vyama vingine vya kisiasa au wananchi ambao hawaoni umuhimu wa kuwa wanachama wa chama chochote cha kisiasa kwa kuwa wao malengo yao makubwa ni ya kiuchumi na kijamii na siasa kwao ni kikwazo na sio msaada au tajamali.
Kwa kuwa chama tawala ndicho kinachoshika serikali basi kinachotokea ni kuwa wanachama wake hupewa vyeo vyote katika nchi hata kama uwezo wao katika hilo ni mdogo au hawana uwezo kabisa. Inakuwa nadra sana kwa asiye mwanachama wa chama tawala kupewa nafasi yoyote ya maana katika kuchangia maendeleo ya nchi na watu wake. Huu ndio ubaguzi mpya. Na kadri demokrasia inavyokuwa dhaifu katika nchi ndivyo ubaguzi huo unavyoshamiri katika nchi ambayo badala ya kwenda mbele kidemokrasia na kimaendeleo huwa inarudi kinyume nyume.
Afrika ilipinga vikali kuwepo kwa ubaguzi wa rangi huko Afrika Kusini. Hii leo nchi zenye tabia za kufanya baadhi ya watu wao watumwa zinatazamwa kwa jicho la hasira. Katika nchi mbalimbali za Kiafrika ubaguzi wa kijinsia uko mashakani. Wanawake sasa sio tu wanasemwa ni huru lakini wanaonekana kuwa huru kuliko huko nyuma. Wasiojiweza na walemavu nao hawakuachwa nyuma. Wote wanajua sasa kwamba wana haki sawa na raia au watu wengine nchini mwao. Haya yote yanaonesha kuwa Waafrika kwa asili yao hawakubali na hawapendi ubaguzi.
La ajabu ni kuwa ujio wa siasa za mfumo wa vyama vingi umekuja na aina mpya ya ubaguzi au 'apartheid' ya kisiasa kama sio ki-chama.
Watu wengi bado hawajaujua kwa undani ubaguzi huu unavyokwenda. Katika makala haya tutajaribu kuonesha jinsi ubaguzi huu ulivyo na unavyoendeshwa.
Ubaguzi wa kichama au kisiasa Afrika unajionesha kwa sura au njia mbalimbali. Kubwa kati ya hizo ni ule ubaguzi unaofanyika katika masuala ya nafasi za kazi,
mikopo na masuala ya fedha,misaada, ujenzi wa miundo-mbinu, elimu. afya, uongozi na fursa nyingine za kiuchumi na kijamii.
Aidha ubaguzi huo upo pia katika kuchagua wafanyakazi kwa ajili ya nafasi za ukatibu mkuu, balozi za nchi za nje, wakuu wa mikoa na wilaya, wakuu wa mashirika, wakuu wa tume au kamisheni mbalimbali, wakuu wa polisi, wakuu wa vyuo, wakuu wa mahospitali, wakuu wa mabenki au taasisi za fedha za umma na wakuu wa serikali za mitaa.
Vilevile kuna ubaguzi pia katika nafasi za masomo ya nje na uteuzi wa wajumbe wa bodi na tume mbalimbali nchini na wakuu wa vyombo vya habari vya serikali/umma.
Kwa upande mwingine wazee, wazazi, vijana
na wanawake aghalabu wa chama tawala huonekana kupendelewa na kupewa haki, fursa na neema zaidi kuliko wale wasio wanachama.
Katika utendaji kazi za serikali aghalabu utakuta mambo yanakuwa ni rahisi na nafuu zaidi kwa wale walio wanachama wa chama tawala kuliko kwa wale wasio wanachama wa chama hicho. Na hata pale serikali inapponesha kuvumiliwa mfumo wa vyama vingi, wapinzani hulazimika kujificha kwa sababu moja au nyingine.
Sio kwamba chama husika hakijui inachokifanya. Inajua vizuri sana. Hufanya hivyo ili kuhakikisha kuwa kinaendelea kujenga mapenzi kati yake na makundi hayo ili uchaguzi unapofika iwe ni rahisi chama hicho kuchaguliwa kuliko chama kingine.
Kwa kufanya hivyo chama tawala hujenga ukuta kati ya wanachama wake na wanachama wa vyama vingine.
Hili linakuwa ni rahsi kufanyika kwa sababu katika Afrika mpaka kati ya serikali na chama tawala huonekana kwa shida sana. Kwa nchi nyingi mpaka huo ni kitu kisichokuwepo.
Kwa kuwa Gavana wa Benki anakuwa ni mtu wao inakuwa ni rahisi kumuamuru kuiba fedha hazina na kuwapa makuwadi na walanguzi wa chama ambao aghalabu huwa hawazifikishi zote. Ni asilimia ndogo tu hatimaye inayotiririkia kwenye kibakuli cha chama husika.
Kwa kuwa Mkuu wa Idara ya Kodi ya Nchi fulani ni mtu wao inakuwa ni rahisi kiongozi wa chama kuamrisha mtu au kampuni fulani idaiwe kodi isipostahili au kodi kubwa kwa lengo la kumkomoa tu mtu huyo au kampuni hiyo kwa kutumia mabavu ya kisiasa.
Katika nchi nyingi kuna wazawa wengi tu wanaoweza kuwekeza katika nchi zao pengine uwekezaji wao ukashinda hata ule wa nje. Lakini kwa sababu ya vitendo vya uonevu na dhuluma wanayofanyiwa na chama tawala huamua kutofanya chochote na kuziweka tu fedha zao au kutanua kwani wanaona ni ujinga mtu kuingizwa matatani kwa sababu ya fedha zake mwenyewe.
Ubaguzi upo kila mahala, lakini kwa sababu za nafasi tuoneshe tu mifano michache ambayo yeyote yule anaweza kuipanua ikafikia kote kule anakotaka.
Katika nafasi za kazi kwa mfano kwa ajili ya mashirika ya umma, balozi za nje na mashirika ya kimaeneo na kimataifa ni dhahiri kuwa wanachama wa chama tawala ndio wanaochaguliwa zaidi sikuzote na hutokea kwa bahati mbaya tu akachaguliwa mtu ambaye sio kada wa chama tawala.
Matokeo ya hili ni kwamba mara nyingi unakuta watu wasiokuwa na uwezo wanapewa kazi au nafasi ambazo hawaziwezi na mwisho kuishia kuharibu kazi na kuziangusha taasisi wanazotakiwa kuziendesha. Hivi leo vipaji na uwezo wa Waafrika walio wengi wakiwemo Watanzania vimezikwa au vinafichwa na havitambuliki kutokana na ubaguzi wa kichama unaoendelea.
Katika nafasi za masomo ingia katika Wizara yoyote ya Elimu katika nchi mbalimbali za Afrika ufanye utafiti na utagundua watu wanaopewa nafasi nzuri za masomo ya juu ni watoto wa wanasiasa au makatibu wakuu wa wizara husika na watu kama hao na watumishi katika wizara hizo.
Katika nchi za Kiafrika vyama tawala vilitumia nafasi ile kabla ya kuwepo kwa mfumo wa vyama vingi kupora majumba, viwanja vya michezo, viwanja na rasilimali zingine na kuzifanya ni zao. Apartheid ya kisiasa katika baadhi ya nchi imekuzwa sana pale chama tawala kilivyopora au kunyakua kinachostahili kuwa cha wote, baadhi ya vitu vilivyoporwa ni pamoja na:
-redio,
-magazeti,
-televisheni,
-viwanja vya michezo
-kumbi za mikutano au jamii
-maeneo ya maegesho
-vijiwe
-shule
-vyuo
-biashara-ardhi na viwanja vilivyopimwa.
Hii ilikuwa bahati yao. Baya kwa hivi sasa ni kwa chama tawala kukataa kurudisha kile kilicho haki ya wananchi wote na kisha kuvinyima vyama mbadala nafasi ya kuwa na mali kama ilizonazo.
Wazee, wazazi, vijana na wanawake wa taifa au ?
Hili la wazazi, wazee, vijana na wanawake wa chama fulani kupata upendeleo sio tu linaleta ubaguzi wa kichama na kisiasa lakini pia linaigawa nchi katika makundi ya wazazi, wazee, vijana na wanawake wa chama tawala na wazazi, wazee, vijana na wanawake ama wasio na chama cha kuwapendelea na kuwasaidia au wale wa vyama mbadala. Huu ni mwanzo wa wanasiasa hapo baadaye kuyatumia makundi hayo kusababisha fujo, ghasia na uvunjaji amani wa aina nyingine hapa nchini.
Kwa maoni yangu, chini ya mfumo wa vyama vingi ni bora kama makundi ya wazazi, wazee, vijana na wanawake yatakuwa ni makundi huru yasiyo na mshkamano na chama chochote cha kisiasa. Au makundi hayo basi yaonekane ni ya kichama na yasipewe kiujanja ujanja sura ya kwamba ni jumuiya za kitaifa. Vinginevyo, makundi hayo yasibague kati ya wanachama wa chama tawala na wale wa vyama vingine au wasio wanachama. Na misaada inapokuja isipitishwa kijanja kusaidia jumuiya hizo kama vile ni za kitaifa kumbe ni za chama kimoja tu cha kisiasa.
Sababu kubwa za kuwepo kwa ubaguzi wa kisiasa au kichama ni ule ukweli kwamba rasilimali na hasa fedha ambazo chama tawala inaweza kuwa nazo wakati wote ni kidogo. Licha ya hivyo kama ilivyo kwa taasisi nyingine yoyote wakubwa hujipendelea kwanza wao na kisha makombo yanayobakia ndio hupewa wanachama.
Makombo hayo pia ni dhahiri hayatoshi. Na kutokana na hili hata wanachama wenyewe ndani ya chama sioi wote wanaopata na kama wanapata hawapati kwa usawa. Sikuzote kuna wanaopata zaidi ya wengine.
Ikifikia hapa ni dhahiri kuona kuwa endapo chama tawala kitafanya ujanja na kikapata fedha kwa njia halali au za kiwiziwizi bado kiasi kinachopatikana hakitoshi kuwagawiwa na wasio wanachama. Hapa ndipo ubaguzi unapoanza na kisha kuendelea siku zote chama hicho kitakavyokuwa madarakani.
Kwa hiyo hatimaye ubaguzi ulioanza kisiasa au kichama huanza kuingia kuwa ubaguzi wa kijamii (matabaka ya wanaopendelewa na wasiopendelewa) kisha ubaguzi wa kijamii huwa ubaguzi wa kiuchumi (walio nacho hupewa zaidi na wasio nacho hunyang'anywa hata kile kidogo walicho nacho) na kisha kukomalia kuwa ubaguzi wa kiraia na kimaeneo ambao huzaa makundi ya watu ambao kufa kupona hukipigia chama fulani tu kura lakini sio chama kingine.
Ubaguzi wa kichama au kisiasa kama ulivyokuwa ubaguzi wa rangi huko Afrika Kusini sio kitu chema na hakiashirii kuendelea kwa umoja, amani na mshikamano wa kitaifa bali kinyume chake. Chama chochote ambacho huwagawa wananchi kati ya wale ambao ni wanachama wake na wale ambao sio wanachama wake wakati kikiwa serikalini sio chama kinachostahili kuwa madarakani hata siku moja.
Apartheid ya kisiasa inaanzishwa na kuendelezwa Afrika kwa malengo ya chama fulani kupata wafuasi watumainiwa na wasiokitupa chama hadi pale hao wanachama wanapotupwa. Hili linaingiza gharama isiyoonekana kiuchumi ya kuwafadhili watu wasiochangia lolote katika ukuaji wa uchumi wa nchi husika.
Kutokana na kuwa rasilimali ikiwemo fedha ni chache na adimu vyama tawala katika nchi nyingi vinaona ni rahisi kugawa wananchi kati ya wananchi wake na wananchi wasio wananchi wake. Baada ya hapo inakuwa ni rahisi kuwatumia watu hao ili kufanikisha malengo yake ya kisiasa. Aghalabu, wananchi wanaokubalika na chama tawala kutokana na ama kuwa wanachama au wapiganaji wake kisiasa ndio wanaopata misaada mbalimbali inayotolewa kwa watu wote. Katika baadhi ya nchi imefikia kwamba hata wakati wa maafa, watumishi wa serikali au wafuasi wa chama tawala wanaopewa majukumu ya misaada hubagua kati ya wenzetu na wengine. Hawa wenzetu ndio wanaofikiriwa na kupata kwanza, wakati wengine huachwa bila huruma wala msaada wowote. Katika tathmini ya mali iliyoharibika 'mwenzetu' sio tu analipwa zaidi lakini juu ya hivyo huweza akapewa na mkopo usiorudishwa pia.
Rushwa ya kisiaasa.
Apartheid ya kisiasa ni rushwa kama zilivyo rushwa nyingine. Wapenda demokrasia wote wanapaswa kuipiga vita kwa ukucha na jino. Ni rushwa mbaya zaidi maana inatumia umasikini na unyonge wa mwananchi kumlazimisha raia kujiunga na chama fulani au kukipigia chama fulani kura hata kama yeye moyoni hakipendi na hakitaki chama hicho.
Nimewahi kuzungumza huko nyuma kwamba rushwa mbalimbali tunazoziona katika nchi yetu asili na chanzo chake ni wanasiasa. Rushwa ikishapangisha kwenye ghorofa ya juu kabisa ya nchi kupitia chama tawala basi inakuwa ni vigumu sana kuipiga rushwa vita katika ghorofa za chini. Na hii ndiyo hali iliyopo katika nchi nyingi za Kiafrika. Rushwa imo katika chama tawala na chama tawala kinapona na kubakia madarakani kutokana na rushwa na sasa inakuwa ni kazi kuwa na uhakika kwamba kinaweza kurudi tena madarakani bila kupewa na chenyewe kutoa rushwa.
Faida za apartheid ya kisiasa
Zaidi ya manufaa ambayo viongozi na chama fulani hupata apartheid ya kisiasa haina faida kwa wananchi walio wengi na nchi husika.
Hasara za Apartheid ya kisiasa
Hasara ya kwanza ni kuwagawa wananchi kati ya wanachama na wasio wanachama. Jambo hili huongeza jeuri, kiburi na ujibari wa wanachama wa chama tawala dhidi ya wananchi wenzao.
Katika hali kama hii kuna kuwa hakuna amani, kuaminiana wala mshikamano kati ya wananchi.
PIli, apartheid ya kisiasa huwanyang'anya walio wengi kipato na kipato hicho kupewa watu wasiostahili kukipata. Matokeo yake ni kuwa na wanasiasa uchwara ambao fedha huwalewesha wakajihusisha na uchafu wa kila aina na kusahau majukumu yao kama viongozi na wasimamizi wa maendeleo ya watu na nchi yao.
Tatu, vyombo vya dola hulazimika kupendelea kabila moja (wanachama) dhidi ya makabila mengine (wasio wanachama) na hatari ya hili ni kwamba dhuluma na unyanyasaji ukizidi nchi 'inarwandishiwa'.
Nne, katika jamii yoyote asilimia ya watu walio na akili ya kuleta maendeleo ya watu wote ni chini ya asilimia nne. Hawa wamegawanyika sio kwa kufuata uzawa, kabila, makazi au jinsia bali kwa namna isiyoeleweka na isiyotambulika. Lakini katika kundi lolote la watu ukilichunguza utakuta halina zaidi ya asilimia hiyo nne, aghalabu, idadi huwa chini ya hapo. Katika Afrika asilimia hii inasemekana kushuka chini hadi 2 kama sio moja tu.
Unapojenga apartheid ya kisiasa, kwa bahati mbaya wewe ukawa na 'wajinga' zaidi kuliko wale 'wenye akili' ndio unajenga safu za uongozi usiokubali kukosolewa, ambao ukifanya madudu bado unaona umefanya sawa tu na unaoamini siku zote wao ni bora na safi zaidi kuliko watu wengine na kinachotokea ni wao kuonewa tu wivu na wale waliokosa. Kiburi na dharau hii ya kutupwa haiwezi kamwe kujenga taifa bora na imara.
Huko Afrika Mashariki kwa mfano katika kisiwa cha Zanzibar wananchi wengi waliojaliwa akili na ujasiriamali wametengwa na waliomo serikalini. Na katika kijinchi hicho inavyoelekea wenye majaliwa ni chini ya asilimia 2 na wote hawa wamewekwa nje ya serikali. Matokeo ya hili yako wazi kwa yeyote mwenye macho kwenda kusikia na kuona hao waliobeba jukumu la uongozi katika sehemu hiyo ya Afrika Mashariki. Laiti isingelikuwa kubebwa na Tanzania bara, Wazanzibari wanaofanya kazi nje, biashara za kiajabuajabu na misaada toka nje leo wanavisiwa hao wangelikuwa wakitembelea magoti.
Wengi wa wanaojifanya ni wanachama wa chama hiki au kile Afrika wanafanya hivyo kutokana na njaa au uoga.
Aghalabu kwa kuwa mara nyingi chama tawala huonekana kwamba ndio walioshika mpini, basi wananchi walioshika makali wanaogopa wasikikaidi kisha kikavuta mpini huo kwa hasara yao. Hili halina dawa nyingine bali kuhakikisha kuwa wanaoshika mpini ni wananchi na sio chama chochote kile cha kisiasa kwa kuimarisha na kukuza demokrasia inayofanya kazi Afrika.
Kama tulivyokataa apartheid na ubaguzi wa aina nyingine hapa Afrika lazima wapendwa Uafrika na Waafrika wa kweli hapa duniani wakatae kabisa ubaguzi wa kichama. Lazima tulee familia, koo, mitaa, kata, tarafa, wilaya na mikoa ambayo sisi sote bila kujali ni wanachama wa chama fulani tunachukuliana kama watoto wenye sifa na tabia tofauti ambazo ni lazima tuviumiliane kama tunataka tuishi kwa amani na upendo.
Wanaochgia kasi ya kukua kwa ukabila wa kichama ni 'washangiliaji' na wala sio watendaji na wazalishaji mali wa kutegemewa na watu na nchi zetu.
Nini kifanyike ?
Jambo la kwanza la kufanya kabla ya kuchukua hatua zinazofaa kuirejesha hali kama ilivyokuwa kabla ya leo ni pamoja na kujiuliza:
Je, kuna chama chochote mtaani, wilayani au mkoani kinachoweza kuanzisha jambo la manufaa bila kukwaza na serikali ?
Je, kuna wanachama wa chama chochote isipokuwa chama tawala wanaoweza kukutana au kufanya maandamano bila kuingiliwa na vyombo vya dola ?
Je, mfanyabiashara akikiunga mkono au kukipigia debe chama kingine isipokuwa chama tawala biashara na mali zake zitakuwa salama ?
Je, chama chochote cha siasa kinaruhusiwa kujenga viwanja vya michezo, shule, hospitali na majengo mengine bila bughudha ?
Je, vyama vya upinzani vinaruhusiwa kuwa na vyombo vyao vya habari ?
Je, nini kinatokea kama chombo fulani cha habari kinaunga mkono au kuwatangaza zaidi upinzani kuliko chama tawala ?
Je, usipokuwa mwanacha wa chama tawala ajira yako na kupanda kwako cheo na maslahi yako yanakuwa sawa na wale wa chama tawala ?
Je, watoto na wake wa wasiokuwa katika chama tawala wanapata jamala na nyenzo sawa na wale wa chama tawala ?
Majibu kwa maswali haya yatatoa njia na mbinu za kushughulikia ukabila au ubaguzi wa kichama katika nchi zetu kwa namna bora na ya uhakika zaidi.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
Maana ya Undugu kwa muktadha huu ni pale mwanasiasa anapotumia nafasi aliyo nayo [akijua wake au chake haviwezi kukataliwa na wajumbe au wabunge-maana yeye ndiye anayewahakikishia kuwepo kwao na maslahi wanayopata, na kwa nafasi hiyo yeye kashika mpini na wanachama na wananchi kwa ujumla wameshika makali. ] kuwapa nafasi za kazi katika chama au serikali ndugu, watoto, wake, jamaa au marafiki zake. Undugu unapokithiri unamloga kiongozi kiasi cha kumfanya atake pia awe na sifa za kifalme falme, ikiwemo pia kurithisha uongozi kwa mwanae au yule amtakaye yeye na siyo yule wanayemtaka wanachama au wananchi. Na akiona anayemtaka hatakiwi anaweza akafanya yote yale ya kuwazaini na kuwatisha watu wake mpaka wakubali kumkubalia matakwa yake. Ingawa imekwishatokea pale watendaji wa chini wanapogundulika na viongozi wa juu kumpandikiza asiyetakikana kwa huyo aliyepandikizwa kuombwa kumuachia yule anayekubalika.
Wakati maana ya Ubaguzi wa aina mpya katika nchi nyingi za Kiafrika, Kiarabu na Kiasia
ni kuachiwa kuzuka kwa ubaguzi kati ya wananchi walio wanachama wa chama tawala na wale wasio wanachama wake. Hawa wanaweza kuwa wanachama wa vyama vingine vya kisiasa au wananchi ambao hawaoni umuhimu wa kuwa wanachama wa chama chochote cha kisiasa kwa kuwa wao malengo yao makubwa ni ya kiuchumi na kijamii na siasa kwao ni kikwazo na sio msaada au tajamali.
Kwa kuwa chama tawala ndicho kinachoshika serikali basi kinachotokea ni kuwa wanachama wake hupewa vyeo vyote katika nchi hata kama uwezo wao katika hilo ni mdogo au hawana uwezo kabisa. Inakuwa nadra sana kwa asiye mwanachama wa chama tawala kupewa nafasi yoyote ya maana katika kuchangia maendeleo ya nchi na watu wake. Huu ndio ubaguzi mpya. Na kadri demokrasia inavyokuwa dhaifu katika nchi ndivyo ubaguzi huo unavyoshamiri katika nchi ambayo badala ya kwenda mbele kidemokrasia na kimaendeleo huwa inarudi kinyume nyume.
Afrika ilipinga vikali kuwepo kwa ubaguzi wa rangi huko Afrika Kusini. Hii leo nchi zenye tabia za kufanya baadhi ya watu wao watumwa zinatazamwa kwa jicho la hasira. Katika nchi mbalimbali za Kiafrika ubaguzi wa kijinsia uko mashakani. Wanawake sasa sio tu wanasemwa ni huru lakini wanaonekana kuwa huru kuliko huko nyuma. Wasiojiweza na walemavu nao hawakuachwa nyuma. Wote wanajua sasa kwamba wana haki sawa na raia au watu wengine nchini mwao. Haya yote yanaonesha kuwa Waafrika kwa asili yao hawakubali na hawapendi ubaguzi.
La ajabu ni kuwa ujio wa siasa za mfumo wa vyama vingi umekuja na aina mpya ya ubaguzi au 'apartheid' ya kisiasa kama sio ki-chama.
Watu wengi bado hawajaujua kwa undani ubaguzi huu unavyokwenda. Katika makala haya tutajaribu kuonesha jinsi ubaguzi huu ulivyo na unavyoendeshwa.
Ubaguzi wa kichama au kisiasa Afrika unajionesha kwa sura au njia mbalimbali. Kubwa kati ya hizo ni ule ubaguzi unaofanyika katika masuala ya nafasi za kazi,
mikopo na masuala ya fedha,misaada, ujenzi wa miundo-mbinu, elimu. afya, uongozi na fursa nyingine za kiuchumi na kijamii.
Aidha ubaguzi huo upo pia katika kuchagua wafanyakazi kwa ajili ya nafasi za ukatibu mkuu, balozi za nchi za nje, wakuu wa mikoa na wilaya, wakuu wa mashirika, wakuu wa tume au kamisheni mbalimbali, wakuu wa polisi, wakuu wa vyuo, wakuu wa mahospitali, wakuu wa mabenki au taasisi za fedha za umma na wakuu wa serikali za mitaa.
Vilevile kuna ubaguzi pia katika nafasi za masomo ya nje na uteuzi wa wajumbe wa bodi na tume mbalimbali nchini na wakuu wa vyombo vya habari vya serikali/umma.
Kwa upande mwingine wazee, wazazi, vijana
na wanawake aghalabu wa chama tawala huonekana kupendelewa na kupewa haki, fursa na neema zaidi kuliko wale wasio wanachama.
Katika utendaji kazi za serikali aghalabu utakuta mambo yanakuwa ni rahisi na nafuu zaidi kwa wale walio wanachama wa chama tawala kuliko kwa wale wasio wanachama wa chama hicho. Na hata pale serikali inapponesha kuvumiliwa mfumo wa vyama vingi, wapinzani hulazimika kujificha kwa sababu moja au nyingine.
Sio kwamba chama husika hakijui inachokifanya. Inajua vizuri sana. Hufanya hivyo ili kuhakikisha kuwa kinaendelea kujenga mapenzi kati yake na makundi hayo ili uchaguzi unapofika iwe ni rahisi chama hicho kuchaguliwa kuliko chama kingine.
Kwa kufanya hivyo chama tawala hujenga ukuta kati ya wanachama wake na wanachama wa vyama vingine.
Hili linakuwa ni rahsi kufanyika kwa sababu katika Afrika mpaka kati ya serikali na chama tawala huonekana kwa shida sana. Kwa nchi nyingi mpaka huo ni kitu kisichokuwepo.
Kwa kuwa Gavana wa Benki anakuwa ni mtu wao inakuwa ni rahisi kumuamuru kuiba fedha hazina na kuwapa makuwadi na walanguzi wa chama ambao aghalabu huwa hawazifikishi zote. Ni asilimia ndogo tu hatimaye inayotiririkia kwenye kibakuli cha chama husika.
Kwa kuwa Mkuu wa Idara ya Kodi ya Nchi fulani ni mtu wao inakuwa ni rahisi kiongozi wa chama kuamrisha mtu au kampuni fulani idaiwe kodi isipostahili au kodi kubwa kwa lengo la kumkomoa tu mtu huyo au kampuni hiyo kwa kutumia mabavu ya kisiasa.
Katika nchi nyingi kuna wazawa wengi tu wanaoweza kuwekeza katika nchi zao pengine uwekezaji wao ukashinda hata ule wa nje. Lakini kwa sababu ya vitendo vya uonevu na dhuluma wanayofanyiwa na chama tawala huamua kutofanya chochote na kuziweka tu fedha zao au kutanua kwani wanaona ni ujinga mtu kuingizwa matatani kwa sababu ya fedha zake mwenyewe.
Ubaguzi upo kila mahala, lakini kwa sababu za nafasi tuoneshe tu mifano michache ambayo yeyote yule anaweza kuipanua ikafikia kote kule anakotaka.
Katika nafasi za kazi kwa mfano kwa ajili ya mashirika ya umma, balozi za nje na mashirika ya kimaeneo na kimataifa ni dhahiri kuwa wanachama wa chama tawala ndio wanaochaguliwa zaidi sikuzote na hutokea kwa bahati mbaya tu akachaguliwa mtu ambaye sio kada wa chama tawala.
Matokeo ya hili ni kwamba mara nyingi unakuta watu wasiokuwa na uwezo wanapewa kazi au nafasi ambazo hawaziwezi na mwisho kuishia kuharibu kazi na kuziangusha taasisi wanazotakiwa kuziendesha. Hivi leo vipaji na uwezo wa Waafrika walio wengi wakiwemo Watanzania vimezikwa au vinafichwa na havitambuliki kutokana na ubaguzi wa kichama unaoendelea.
Katika nafasi za masomo ingia katika Wizara yoyote ya Elimu katika nchi mbalimbali za Afrika ufanye utafiti na utagundua watu wanaopewa nafasi nzuri za masomo ya juu ni watoto wa wanasiasa au makatibu wakuu wa wizara husika na watu kama hao na watumishi katika wizara hizo.
Katika nchi za Kiafrika vyama tawala vilitumia nafasi ile kabla ya kuwepo kwa mfumo wa vyama vingi kupora majumba, viwanja vya michezo, viwanja na rasilimali zingine na kuzifanya ni zao. Apartheid ya kisiasa katika baadhi ya nchi imekuzwa sana pale chama tawala kilivyopora au kunyakua kinachostahili kuwa cha wote, baadhi ya vitu vilivyoporwa ni pamoja na:
-redio,
-magazeti,
-televisheni,
-viwanja vya michezo
-kumbi za mikutano au jamii
-maeneo ya maegesho
-vijiwe
-shule
-vyuo
-biashara-ardhi na viwanja vilivyopimwa.
Hii ilikuwa bahati yao. Baya kwa hivi sasa ni kwa chama tawala kukataa kurudisha kile kilicho haki ya wananchi wote na kisha kuvinyima vyama mbadala nafasi ya kuwa na mali kama ilizonazo.
Wazee, wazazi, vijana na wanawake wa taifa au ?
Hili la wazazi, wazee, vijana na wanawake wa chama fulani kupata upendeleo sio tu linaleta ubaguzi wa kichama na kisiasa lakini pia linaigawa nchi katika makundi ya wazazi, wazee, vijana na wanawake wa chama tawala na wazazi, wazee, vijana na wanawake ama wasio na chama cha kuwapendelea na kuwasaidia au wale wa vyama mbadala. Huu ni mwanzo wa wanasiasa hapo baadaye kuyatumia makundi hayo kusababisha fujo, ghasia na uvunjaji amani wa aina nyingine hapa nchini.
Kwa maoni yangu, chini ya mfumo wa vyama vingi ni bora kama makundi ya wazazi, wazee, vijana na wanawake yatakuwa ni makundi huru yasiyo na mshkamano na chama chochote cha kisiasa. Au makundi hayo basi yaonekane ni ya kichama na yasipewe kiujanja ujanja sura ya kwamba ni jumuiya za kitaifa. Vinginevyo, makundi hayo yasibague kati ya wanachama wa chama tawala na wale wa vyama vingine au wasio wanachama. Na misaada inapokuja isipitishwa kijanja kusaidia jumuiya hizo kama vile ni za kitaifa kumbe ni za chama kimoja tu cha kisiasa.
Sababu kubwa za kuwepo kwa ubaguzi wa kisiasa au kichama ni ule ukweli kwamba rasilimali na hasa fedha ambazo chama tawala inaweza kuwa nazo wakati wote ni kidogo. Licha ya hivyo kama ilivyo kwa taasisi nyingine yoyote wakubwa hujipendelea kwanza wao na kisha makombo yanayobakia ndio hupewa wanachama.
Makombo hayo pia ni dhahiri hayatoshi. Na kutokana na hili hata wanachama wenyewe ndani ya chama sioi wote wanaopata na kama wanapata hawapati kwa usawa. Sikuzote kuna wanaopata zaidi ya wengine.
Ikifikia hapa ni dhahiri kuona kuwa endapo chama tawala kitafanya ujanja na kikapata fedha kwa njia halali au za kiwiziwizi bado kiasi kinachopatikana hakitoshi kuwagawiwa na wasio wanachama. Hapa ndipo ubaguzi unapoanza na kisha kuendelea siku zote chama hicho kitakavyokuwa madarakani.
Kwa hiyo hatimaye ubaguzi ulioanza kisiasa au kichama huanza kuingia kuwa ubaguzi wa kijamii (matabaka ya wanaopendelewa na wasiopendelewa) kisha ubaguzi wa kijamii huwa ubaguzi wa kiuchumi (walio nacho hupewa zaidi na wasio nacho hunyang'anywa hata kile kidogo walicho nacho) na kisha kukomalia kuwa ubaguzi wa kiraia na kimaeneo ambao huzaa makundi ya watu ambao kufa kupona hukipigia chama fulani tu kura lakini sio chama kingine.
Ubaguzi wa kichama au kisiasa kama ulivyokuwa ubaguzi wa rangi huko Afrika Kusini sio kitu chema na hakiashirii kuendelea kwa umoja, amani na mshikamano wa kitaifa bali kinyume chake. Chama chochote ambacho huwagawa wananchi kati ya wale ambao ni wanachama wake na wale ambao sio wanachama wake wakati kikiwa serikalini sio chama kinachostahili kuwa madarakani hata siku moja.
Apartheid ya kisiasa inaanzishwa na kuendelezwa Afrika kwa malengo ya chama fulani kupata wafuasi watumainiwa na wasiokitupa chama hadi pale hao wanachama wanapotupwa. Hili linaingiza gharama isiyoonekana kiuchumi ya kuwafadhili watu wasiochangia lolote katika ukuaji wa uchumi wa nchi husika.
Kutokana na kuwa rasilimali ikiwemo fedha ni chache na adimu vyama tawala katika nchi nyingi vinaona ni rahisi kugawa wananchi kati ya wananchi wake na wananchi wasio wananchi wake. Baada ya hapo inakuwa ni rahisi kuwatumia watu hao ili kufanikisha malengo yake ya kisiasa. Aghalabu, wananchi wanaokubalika na chama tawala kutokana na ama kuwa wanachama au wapiganaji wake kisiasa ndio wanaopata misaada mbalimbali inayotolewa kwa watu wote. Katika baadhi ya nchi imefikia kwamba hata wakati wa maafa, watumishi wa serikali au wafuasi wa chama tawala wanaopewa majukumu ya misaada hubagua kati ya wenzetu na wengine. Hawa wenzetu ndio wanaofikiriwa na kupata kwanza, wakati wengine huachwa bila huruma wala msaada wowote. Katika tathmini ya mali iliyoharibika 'mwenzetu' sio tu analipwa zaidi lakini juu ya hivyo huweza akapewa na mkopo usiorudishwa pia.
Rushwa ya kisiaasa.
Apartheid ya kisiasa ni rushwa kama zilivyo rushwa nyingine. Wapenda demokrasia wote wanapaswa kuipiga vita kwa ukucha na jino. Ni rushwa mbaya zaidi maana inatumia umasikini na unyonge wa mwananchi kumlazimisha raia kujiunga na chama fulani au kukipigia chama fulani kura hata kama yeye moyoni hakipendi na hakitaki chama hicho.
Nimewahi kuzungumza huko nyuma kwamba rushwa mbalimbali tunazoziona katika nchi yetu asili na chanzo chake ni wanasiasa. Rushwa ikishapangisha kwenye ghorofa ya juu kabisa ya nchi kupitia chama tawala basi inakuwa ni vigumu sana kuipiga rushwa vita katika ghorofa za chini. Na hii ndiyo hali iliyopo katika nchi nyingi za Kiafrika. Rushwa imo katika chama tawala na chama tawala kinapona na kubakia madarakani kutokana na rushwa na sasa inakuwa ni kazi kuwa na uhakika kwamba kinaweza kurudi tena madarakani bila kupewa na chenyewe kutoa rushwa.
Faida za apartheid ya kisiasa
Zaidi ya manufaa ambayo viongozi na chama fulani hupata apartheid ya kisiasa haina faida kwa wananchi walio wengi na nchi husika.
Hasara za Apartheid ya kisiasa
Hasara ya kwanza ni kuwagawa wananchi kati ya wanachama na wasio wanachama. Jambo hili huongeza jeuri, kiburi na ujibari wa wanachama wa chama tawala dhidi ya wananchi wenzao.
Katika hali kama hii kuna kuwa hakuna amani, kuaminiana wala mshikamano kati ya wananchi.
PIli, apartheid ya kisiasa huwanyang'anya walio wengi kipato na kipato hicho kupewa watu wasiostahili kukipata. Matokeo yake ni kuwa na wanasiasa uchwara ambao fedha huwalewesha wakajihusisha na uchafu wa kila aina na kusahau majukumu yao kama viongozi na wasimamizi wa maendeleo ya watu na nchi yao.
Tatu, vyombo vya dola hulazimika kupendelea kabila moja (wanachama) dhidi ya makabila mengine (wasio wanachama) na hatari ya hili ni kwamba dhuluma na unyanyasaji ukizidi nchi 'inarwandishiwa'.
Nne, katika jamii yoyote asilimia ya watu walio na akili ya kuleta maendeleo ya watu wote ni chini ya asilimia nne. Hawa wamegawanyika sio kwa kufuata uzawa, kabila, makazi au jinsia bali kwa namna isiyoeleweka na isiyotambulika. Lakini katika kundi lolote la watu ukilichunguza utakuta halina zaidi ya asilimia hiyo nne, aghalabu, idadi huwa chini ya hapo. Katika Afrika asilimia hii inasemekana kushuka chini hadi 2 kama sio moja tu.
Unapojenga apartheid ya kisiasa, kwa bahati mbaya wewe ukawa na 'wajinga' zaidi kuliko wale 'wenye akili' ndio unajenga safu za uongozi usiokubali kukosolewa, ambao ukifanya madudu bado unaona umefanya sawa tu na unaoamini siku zote wao ni bora na safi zaidi kuliko watu wengine na kinachotokea ni wao kuonewa tu wivu na wale waliokosa. Kiburi na dharau hii ya kutupwa haiwezi kamwe kujenga taifa bora na imara.
Huko Afrika Mashariki kwa mfano katika kisiwa cha Zanzibar wananchi wengi waliojaliwa akili na ujasiriamali wametengwa na waliomo serikalini. Na katika kijinchi hicho inavyoelekea wenye majaliwa ni chini ya asilimia 2 na wote hawa wamewekwa nje ya serikali. Matokeo ya hili yako wazi kwa yeyote mwenye macho kwenda kusikia na kuona hao waliobeba jukumu la uongozi katika sehemu hiyo ya Afrika Mashariki. Laiti isingelikuwa kubebwa na Tanzania bara, Wazanzibari wanaofanya kazi nje, biashara za kiajabuajabu na misaada toka nje leo wanavisiwa hao wangelikuwa wakitembelea magoti.
Wengi wa wanaojifanya ni wanachama wa chama hiki au kile Afrika wanafanya hivyo kutokana na njaa au uoga.
Aghalabu kwa kuwa mara nyingi chama tawala huonekana kwamba ndio walioshika mpini, basi wananchi walioshika makali wanaogopa wasikikaidi kisha kikavuta mpini huo kwa hasara yao. Hili halina dawa nyingine bali kuhakikisha kuwa wanaoshika mpini ni wananchi na sio chama chochote kile cha kisiasa kwa kuimarisha na kukuza demokrasia inayofanya kazi Afrika.
Kama tulivyokataa apartheid na ubaguzi wa aina nyingine hapa Afrika lazima wapendwa Uafrika na Waafrika wa kweli hapa duniani wakatae kabisa ubaguzi wa kichama. Lazima tulee familia, koo, mitaa, kata, tarafa, wilaya na mikoa ambayo sisi sote bila kujali ni wanachama wa chama fulani tunachukuliana kama watoto wenye sifa na tabia tofauti ambazo ni lazima tuviumiliane kama tunataka tuishi kwa amani na upendo.
Wanaochgia kasi ya kukua kwa ukabila wa kichama ni 'washangiliaji' na wala sio watendaji na wazalishaji mali wa kutegemewa na watu na nchi zetu.
Nini kifanyike ?
Jambo la kwanza la kufanya kabla ya kuchukua hatua zinazofaa kuirejesha hali kama ilivyokuwa kabla ya leo ni pamoja na kujiuliza:
Je, kuna chama chochote mtaani, wilayani au mkoani kinachoweza kuanzisha jambo la manufaa bila kukwaza na serikali ?
Je, kuna wanachama wa chama chochote isipokuwa chama tawala wanaoweza kukutana au kufanya maandamano bila kuingiliwa na vyombo vya dola ?
Je, mfanyabiashara akikiunga mkono au kukipigia debe chama kingine isipokuwa chama tawala biashara na mali zake zitakuwa salama ?
Je, chama chochote cha siasa kinaruhusiwa kujenga viwanja vya michezo, shule, hospitali na majengo mengine bila bughudha ?
Je, vyama vya upinzani vinaruhusiwa kuwa na vyombo vyao vya habari ?
Je, nini kinatokea kama chombo fulani cha habari kinaunga mkono au kuwatangaza zaidi upinzani kuliko chama tawala ?
Je, usipokuwa mwanacha wa chama tawala ajira yako na kupanda kwako cheo na maslahi yako yanakuwa sawa na wale wa chama tawala ?
Je, watoto na wake wa wasiokuwa katika chama tawala wanapata jamala na nyenzo sawa na wale wa chama tawala ?
Majibu kwa maswali haya yatatoa njia na mbinu za kushughulikia ukabila au ubaguzi wa kichama katika nchi zetu kwa namna bora na ya uhakika zaidi.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
Sunday, June 21, 2009
DEMOKRASIA NA VYOMBO VYA DOLA
Maana ya Vyombo vya Dola
Vyombo vya Dola ni vyombo vyote ambavyo huwepo ili kulinda amani ya wote au amani ya wachache kulingana na hali itakavyokuwa ili mradi anayetoa amri ya mwisho kwa vyombo hivyo ndiye mkuu wa nchi. Katika demokrasia halisi vyombo vya dola hutumika kuwalinda wananchi wote na havitumiki kuwalinda wachache au wakubwa fulani tu katika nchi. Katika demokrasia finyu au chipukizi au demokrasia inayoorojeshwa au kuwekwa pembeni kabisa vyombo vya dola hutumika kuwadhibiti wananchi ili watawala wasibughudhiwe katika mabaya au mazuri wanayowafanyia watu wao. Kwa maneno mengine, vyombo vya dola vinaweza kutumika kuimarisha haki, uhuru na demokrasia ya watu au kinyume cha hivyo.
Katika demokrasia ya kweli ni muhali kwa wanajeshi au askari polisi au mgambo au makundi mengine ya kiulinzi yaliyoidhinishwa na bunge kuwaelekezea mtutu wananchi.
Vyombo vya dola havitumiki kuleta fujo na madhara kwa wananchi bali kuepusha mambo hayo, hata kama inabidi, polisi au askari kuteseka au kuumia au hata kufa.
Urithi wa mkoloni uliokubalika
Urithi ambao Mwafrika kiongozi aliukubali kwa mikono miwili ni ule wa vyombo vya dola. Aidha kwa kuhofia udhaifu wao na uwezo wao wa kuwatimizia watu wao mahitaji na matakwa yao viongozi wengi wa Afrika wameendelea kuvitumia vyombo vya dola kwa kazi ileile iliyofanywa wakati wa mkoloni nayo ni ile ya kumdhibiti mwananchi ili aibiwe, anyonywe, adhalilishwe, adhulumiwe na asifurukute kwenda upande wowote anaoweza kujichomoa.
Katika Afrika hili linakuwa rahisi kwa sababu karibu polisi na walinzi wote hulipwa mshahara mdogo sana ambao unawaingiza katika vishawishi vya aina nyingi. Vishawishi hivyo ni pamoja vile vya rushw ya fedha na rushwa za kisiasa na kiuongozi.
Kwa kuwa mkuu wa nchi ndiye anayetoa fadhila kwa fulani kuwa mkuu wa polisi au majeshi na kadhalika msururu wote wa watumishi katika vyombo vya dola huelekeza utii wao sio kwa raia ila kwa rais wa nchi na watu wake maalum au vyombo vyake vingine. Katika hali kama hii walio wengi katika vyombo vya dola kama tulivyoona kule Zimbabwe, Kenya, Liberia, Misri na kadhalika ni rahisi sana kutumiwa kwa maslahai yasiyo ya wananchi.
Kila nchi huwatumia polisi ili kudhibiti uhalifu na kuhakikisha usalama wa raia na mali zao. Aidha polisi hutumika ili kuhakikisha kuna ustaarabu na utaratibu unaokubalika wakati wa maingiliano ya watu katika shughuli zao mbalimbali za kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni.
Majukumu mengine waliyonayo polisi zaidi ya kupambana na uhalifu ni pamoja na: upatanishi kati ya wagombanao, usalama barabarani na kutoa msaada wakati wa maafa.
Majukumu haya yanatekelezwa kwa viwango tofauti katika nchi mbalimbali kulingana na uchanga au ukomavu wa demokrasia ya nchi.
Polisi kama kiungo muhimu katika demokrasia
Polisi ni kiungo muhimu katika ujenzi wa demokrasia. Ili mradi kiungo hicho kinatimiza yafuatayo:
1. Kufanya kazi kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi na sio kwa kufuata amri au matakwa ya kiongozi mbabe au chama chenye kuendekeza udikteta;
2. Kuingilia kati maisha ya raia pale tu ambapo ni lazima kabisa lakini kwa umakini na uangalifu ili kutosababisha hasara ya maisha au mali; na
3. Wanawajibika kwa wananchi wote na sio kwa kikundi fulani cha watu katika nchi.
Hata hivyo sio kweli kuwa ni polisi tu wanaoweza kuepusha ghasia au fujo ili pawepo na utulivu, mshikamano na amani katika jamii. Yapo mambo kadhaa ambayo kwa pamoja na mchango wa polisi ndio yanayoweza kuihakikishia nchi umoja na amani ya kudumu. Mambo hayo ni pamoja na:
. jamii kuwa na maadili na tabia zinazokubalika katika maingiliano yake,kwa maneno mengine, hili linalazimisha watu kutambua kwa dhahiri na bayana ni nini ni uovu na nini ni wema, nini ni dhuluma na nini ni haki, nini ni ukweli na nini ni uongo;
. shauku ya kila mtu kutaka kuthaminiwa na kuheshimiwa na wanajamii wenzake,
. ushirikiano na kusaidiana kwa wanajamii, na
. haja ya ulinzi na kupambana na mazingira yanayoizunguka jamii.
Polisi ni muhimu kwa sababu wao peke yao kisheria ndio wanaoruhusiwa tu kutumia nguvu na kuwanyima watu uhuru wao.
Uwezo huu wa polisi unaweza kukubalika na watu fulani katika jamii (kwa kuwa polisi wanawalinda au kuwasaidia) lakini ndio huohuo unaoweza kutafsiriwa kwamba ni mabavu na uonevu na kundi linaloamini linanyimwa uhuru au haki zao za kimsingi.
Uwezo huo wa polisi kwa kweli pia unatoa mwanywa wa polisi kufanya kile wanachokitaka hata ikiwa ni kinyume cha sheria.
Utekelezaji wa kazi za upolisi katika jamii yoyote ya kidemokrasia huhitaji mizania linganifu wakati wote. Maana ukweli ni kuwa polisi wanaweza wakawa ama msaada mkubwa au hatari kubwa kwa demokrasia ya nchi fulani.
Uwezo wa polisi kutumia nguvu, kutoa adhabu za papo kwa hapo, kufuatilia na kuwapeleleza watu kwa siri hivi hivi au kwa kutumia teknolojia, kuwasimamisha, kuwasachi na kuwakamata watu kunaweza kutumika kusaidia udikteta ulioko madarakani kirahisi tu.
Polisi ni neno linalotokana na neno 'polity' ambalo huko Ulaya miaka 500 iliyopita lilitumiwa kuonesha aina ya serikali inayosimamiwa na chombo cha kisiasa. Chombo hicho kilihusishwa zaidi na maisha, afya na mali za watu. Nchi hazikuwa na polisi tunaowajua leo. Waliofanya kazi hizo walikuwa ni askari au watu maalum wa kuteuliwa na viongozi.
Katika karne ya 18 polisi wakawa wanajihusisha zaidi na masuala ya ndani na usalama wa watu.
Polepole, polisi ikageuka na kukengeuka baada ya dhana ya nchi huru zanye mipaka kuibuka kuwa taasisi ya kulinda mipaka ya nchi, usalama wa ndani na kudhibiti kisheria maingiliano ya watu katika maisha yao ya kila siku.
Nchi zinahitaji polisi wa kidemokrasia sio kikoloni
Hivi leo tunazungumzia jinsi ya kuwa na jeshi la polisi linaloendana na kanuni za kidemokrasia. Polisi wa kidemokrasia wana sifa zipi? Ni rahisi kwa kweli kueleza au kufafanua polisi wasio na mwelekeo wa kidemokrasia wakoje. Hii ni kwa sababu ni wale wote wanaovunja karibu kila msingi na kanuni ya demokrasia. Hata hivyo, tutajitahidi kuelezea kwa kifupi hapa ni namna gani polisi wa kidemokrasia wanatakiwa kuwa.
Polisi wa kidemokrasia kwa kawaida huwa na sifa hizi: hufanya kazi kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi na sio kwa matakwa ya mkuu wa nchi au wanasiasa. Polisi hutumiwa nguvu na uwezo wao kwa umakini, uangalifu na kwa kuwajali sana wananchi. Mahalani, Uingereza, kwa ridhaa ya wananchi, hairuhusu polisi wake kutembea na silaha. Watu hutii polisi kwa kuwaheshimu kutokana na jukumu lao kijamii na sio kwa kutishwa.
Kazi za polisi wa kidemokrasia hujulikana kutokana na jinsi wanavyofanya kazi zao na namna wanavyofikia malengo yao. Mambo kama utesaji, kuua watuhumiwa papo kwa hapo, kuteka watu nyara au kuwakamata na kuwajeruhi watoto, ndugu au jamaa wa mtuhimiwa huwa hayakubaliki na hukatazwa kisheria.
Masuala kama kutumia nguvu au kumnyima mtu uhuru wake au kuwahoji watuhumiwa hufanyika kwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa na kwa ruhusa kutoka kiongozi au mamlaka husika.
Kwa ufupi polisi huwa na haki tu ya kumkamata mtuhumiwa lakini hawana haki ya kuchukua sheria mkononi mwao. Jambo ambalo sasa mara kwa mara linaonekana la kawaida katika jamii yetu.
Ni wajibu wa polisi wa kidemokrasia kuhakikisha sikuzote kuwa mtawala na mtawaliwa, tajiri na masikini, mnyonge na mwenye nguvu hakuna anayekuwa juu ya katiba na sheria za nchi.
Sio lazima polisi wa demokrasia nchini mwetu wafanane na wale wa nchi nyingine. Lakini ni lazima kwa polisi kuhakikisha kuwa wanawajibika kwa walipa kodi na sio kwa watawala au wale ambao kuwepo kwao kama wao kunategemea kodi anayolpa mwananchi. Baada ya hapa mengine yanakuwa ni rahisi.
Kukua na kukomaa kwa demokrasia kunategemea sana jinsi jeshi la polisi linavyolelewa katika nchi husika.
Vyama tawala visihodhi polisi
Viongozi wa chama tawala katika nchi husika wanaweza wakalilea jeshi la polisi kama vile ni jeshi la kulinda chama tawala na viongozi wake. Au wanaweza wakalilea jeshi hilo kama lenye kuwajibika kwa wananchi wote bila kujali wanatokea chama gani.
Dhuluma, uonevu, wizi na ubabe katika siasa, aghalabu, hutokea pale ambapo jeshi la polisi linalelewa kwa namna ile ya kwanza.
Hili huzaa hali ya polisi kuona kwamba chama tawala, viongozi na wanachama wake kwamba wao sikuzote ndio wenye haki, wenye kusema ukweli na walio safi kuliko wanajamii wengine na makundi au vyama vyao vya kisiasa na visivyo vya kisiasa. Tatizo linakuja pale ambapo chama husika kinakuwa ndio mwizi au jambazi na wengine ndio wanaoibiwa au kudhulumiwa. Polisi wa nchi atasimama wapi ?
Katika hali kama hii wananchi wasiokiunga chama tawala mkono na hususan wanachma na viongozi wa vyama mbadala huonekna sikuzote ni wakorofi, wabishi na wavunja sheria.
Uhusiano wa polisi na chama tawala kwa hiyo huwa ni wawenzetu na ule wa jeshi hilo na wasio wanachama wa chama tawala huwa ni uhusiano na wahalifu au wahalifu watarajiwa.
Haya yote yanaonesha upo umuhimu wa kurejea vipengele katika katiba ya nchi (na kama tutakuwa na katiba mpya ni vyema zaidi) ili kuweka uhusiano wa polisi na viongozi kwa upnade mmoja na polisi na wananchi kwa upande mwingine bayana. Katika marejeo hayo izingatiwe kuwa ni kosa kwa polisi kutumiwa na chama chohcote cha kisiasa, kikiwemo, pia chama tawala. Na endapo hili linakiukwa basi wananchi wawe na haki ya kulishtaki jeshi hilo kwa kuvunja katiba na sheria za nchi.
Nani kumteua polisi mkuu
Jeshi la polisi, hata hvyo, haliwezi kubadilika kama wakuu wa polisi wataendelea kuchaguliwa na rais na sio bunge au Jaji mkuu kama jaji huyo ndiye anayechaguliwa na bunge. Uoga wa makamanda wengi kuwa wanaweza wakatemwa na chama tawala kama wasipokipendelea chama hicho na kuvionea vyama mbadala utatoweka mara moja kama kamanda huyo atakuwa hawezi kufukuzwa kazi na rais au waziri mkuu au kiongozi mwingine wa serikali.
Katika miaka hii ambayo tunazungumzia pia kuwa na wizara chache na wizara zilizo nyingi kugeuzwa kuwa ni wakala, kamisheni, tume au taasisi maalum ni muhimu pia kuangalia ni jinsi gani jeshi hilo linaweza kugeuzwa kuwa la kukuza na kupanua demokrasia zaidi na sio jeshi la kukwaza na kuidhofisha.
Hili litahitaji jeshi letu kutokuendelea kuwa la kupokea amri za kikoloni, kibabe na kidhulumati na kutumia mabavu badala ya busara na hekima ili kujenga udugu na mshikamano muafaka katika jamii husika. Jambo ambalo husaidia wananchi kujipolisi wao wenyewe.
Aidha, hili litasaidia kuzika tabia iliyozika ya baadhi ya vyama vya siasa Afrika kujijenga kwa kuruhusu baadhi ya wanajamii kuvunja sheria za nchi na kuwalinda.
Masharti ya matumizi bora ya polisi
Ili haya yote yafanikiwe ni muhimu mambo kadhaa kufanyika:
Kwanza, lazima pawe na jitihada zinazoonekana kufanyika na kuendelezwa wakati wote na kuzuia polisi kutumiwa na chama cha kisiasa hata kama kikiwa ni chama tawala wakati huo. Katika misingi ya utawala wa kisheria hakuna chama kinachostahili kuwa juu ya sheria katika demokrasia. Vyote lazima viwe chini ya sheria. Kazi nyeti zaidi itakuwa ni kwa jeshi hilo kujua namna ya kutenga kati ya mambo ya serikali na yale ya chama au vyama tawala vya wakati huo. Na pasiwe na raia yeyote anayeweza kuonewa au kunyanyaswa kwa kuwa amefuata sheria za nchi nukta baada ya nukta.
Polisi nao wanapaswa kuwa chini ya sheria- ikiwa ni sehemu muhimu ya uwajibikaji katika mfumo wa vyama vingi. Hili lisipofanyika ni rahisi kutoa mwanya kwa watu wezi, wauaji, wauza madawa na kama hao kujipenyeza ndani ya jeshi hilo na kuunda dola ndani ya dola au serikali ndani ya serikali. Angalia kinachofanyika sasa Algeria, Arbezeijan, Kenya, Kongo, Burundi, Ethiopia, Misri, Moldovia, Burma, Mexico, Colombia na Zimbabwe.
Kurejesha imani ya wananchi kwa jeshi la polisi kama ilivyokuwa katika siku za mwanzo za uhuru itatupasa tuyasuke upya majeshi yetu ya polisi. Polisi na wananchi laizma wawe ni pande mbili zinazotegemeana kwa faid aya jamhuri nzima. Pasiwe na upand unaougeuza upande mwingine kuwa ni buzi la kuchuna mchana kweupe!
Ili uhuru, usawa na haki viimarike katika nchi ni muhimu sana kwa jeshi la polisi kuonekana kama ni walinda haki na watu sio tu wanaokubalika bali wanaothaminiwa sana na jamii. Mfumo unaowafanya wananchi walione jeshi la polisi kama ni jeshi la watu wabaya na wasioaminika haliwezi kujenga jamii bora na nchi inayoheshimika. Na mara nyingi hali hutokea pale jeshi hilo linapogeuzwa kuwa ni jeshi la 'wanyama wakali' waliokusanywa kumlinda mmiliki wao hata kama mmiliki huyo akiwa jambazi.
Ndio kusema kwamba jeshi la polisi linastahili kurudishwa chuoni. Huko watajifunza kuwa demokrasia sio tu jambo zuri kwa nchi bali kwao pia na kwa wananchi wenzao.
Itapaswa wajue kwamba raia ni dada, kaka, baba, mama, bibi na babu zao. Na chochote wanachokifanya kiwe kizuri au kibaya hakiwezi kutoka nje ya mduara ambao wote tunacheza humo.
Wito wa polisi katika nchi inayotaka kujenga demokrasia inayofanya kazi kikwelikweli ni lazima uwe -'usalama na ulinzi kwa wote bila kubagua.'
Kukua na kuimarika demokrasia na polisi
Zipo njia mbalimbali ambazo nchi inaweza ikatumia ili kukuza na kupanua demokrasia. Njia hizo ni pamoja kwa haraka haraka na masuala kama:
. Kutenganisha kazi zao na masuala ya kisiasa.
. Kutokubali kuingizwa katika hali au mitego inayoweza kusababisha wao kuwa ndio waanzishaji fujo mahala fulani. Hii ni pamoja na kukataa kuingia kwenye maeneo ya shule na vyuo. Tabia iliyozuka siku za karibuni kuruhusu mkuu wa shule kuwaita polisi au wanajeshi kuvamia vyuo sio uamuzi wa busara wala hekima. Kila shule au chuo kinastahili kuwa na walinzi wake wanaotenda haki kwa wote bila kujali nafasi au cheo cha mtu katika taasisi husika;
. Kurahisisha na sio kuzuia kufanyika kwa mikutano na maandamano ya wananchi. Ni kosa la katiba na kisheria kuwazuia wananchi popote pale nchini kufanya mikutano au maandamano;
. Kuhakikisha kuna mwingiliano kati ya mapolisi na raia kupitia mambo mbalimbali kama vile michezo, starehe, uwekezaji na shughuli za maendeleo ya kijamii.
. Kusaidia makundi ya kijamii ikiwemo vyama vya kisiasa kuendesha mambo yao katika hali ya utulivu na usalama.
. Kutokubali kuwepo kwa wezi, makuwadi, vibaka, dhulumati, wala rushwa, walevi, wazinzi, matapeli na wababishaji katika jeshi hilo.
Ikiwa hayo hapo juu yatafnyika bila shaka kutakuwa na uhusiano mzuri kati ya polisi na jamii. Uhusiano mzuri kati ya polisi na jamii huchangia kwa kiasi kikubwa kuchanua na kustawi kwa demokrasia na shughuli zote zinazoendana na ujenzi wake.
Aidha Polisi wanastahili pia kufanya kazi kwa ushirikiano na ukaribu zaidi na mahakama, bunge na viongozi wa kijamii ili kukuza na kupanua demokrasia wakati wote.
Polisi ni watumishi sio mabwana
Aidha serikali na wakuu wa polisi wakati mwingine hujisahau na kudhani kuwa wao ni mabwana na wananchi ni watwana. Katika demokrasia inayofanya kazi sawasawa yeyote anayejisahau kwamba ni mtumishi wa wananchi anapaswa kuondolewa mara moja na nafasi yake kuchukuliwa na yule anayetambua ukweli huu kuwa watumishi wa serikali wakiwmo polisi ni watumishi wa wananchi na sio mabwana wao. Hili la polisi kuwa watumishi na sio mabwana ni jambo muhimu sana. Ni pale ambapo aghalabu polisi wamepewa vichwa na viongozi kisha wakajiona wao ndio mabwana kwa sababu wana silaha na nguvu za dola ndipo ambapo nchi zimechafuka na kutokea uvunjaji haki wa kutisha na hata mauaji ya kimbari. Tuliepuke hili kwa kuwakumbusha polisi wetu sikuzote kuwa wao ni watumishi wa watu na sio mabwana.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
Vyombo vya Dola ni vyombo vyote ambavyo huwepo ili kulinda amani ya wote au amani ya wachache kulingana na hali itakavyokuwa ili mradi anayetoa amri ya mwisho kwa vyombo hivyo ndiye mkuu wa nchi. Katika demokrasia halisi vyombo vya dola hutumika kuwalinda wananchi wote na havitumiki kuwalinda wachache au wakubwa fulani tu katika nchi. Katika demokrasia finyu au chipukizi au demokrasia inayoorojeshwa au kuwekwa pembeni kabisa vyombo vya dola hutumika kuwadhibiti wananchi ili watawala wasibughudhiwe katika mabaya au mazuri wanayowafanyia watu wao. Kwa maneno mengine, vyombo vya dola vinaweza kutumika kuimarisha haki, uhuru na demokrasia ya watu au kinyume cha hivyo.
Katika demokrasia ya kweli ni muhali kwa wanajeshi au askari polisi au mgambo au makundi mengine ya kiulinzi yaliyoidhinishwa na bunge kuwaelekezea mtutu wananchi.
Vyombo vya dola havitumiki kuleta fujo na madhara kwa wananchi bali kuepusha mambo hayo, hata kama inabidi, polisi au askari kuteseka au kuumia au hata kufa.
Urithi wa mkoloni uliokubalika
Urithi ambao Mwafrika kiongozi aliukubali kwa mikono miwili ni ule wa vyombo vya dola. Aidha kwa kuhofia udhaifu wao na uwezo wao wa kuwatimizia watu wao mahitaji na matakwa yao viongozi wengi wa Afrika wameendelea kuvitumia vyombo vya dola kwa kazi ileile iliyofanywa wakati wa mkoloni nayo ni ile ya kumdhibiti mwananchi ili aibiwe, anyonywe, adhalilishwe, adhulumiwe na asifurukute kwenda upande wowote anaoweza kujichomoa.
Katika Afrika hili linakuwa rahisi kwa sababu karibu polisi na walinzi wote hulipwa mshahara mdogo sana ambao unawaingiza katika vishawishi vya aina nyingi. Vishawishi hivyo ni pamoja vile vya rushw ya fedha na rushwa za kisiasa na kiuongozi.
Kwa kuwa mkuu wa nchi ndiye anayetoa fadhila kwa fulani kuwa mkuu wa polisi au majeshi na kadhalika msururu wote wa watumishi katika vyombo vya dola huelekeza utii wao sio kwa raia ila kwa rais wa nchi na watu wake maalum au vyombo vyake vingine. Katika hali kama hii walio wengi katika vyombo vya dola kama tulivyoona kule Zimbabwe, Kenya, Liberia, Misri na kadhalika ni rahisi sana kutumiwa kwa maslahai yasiyo ya wananchi.
Kila nchi huwatumia polisi ili kudhibiti uhalifu na kuhakikisha usalama wa raia na mali zao. Aidha polisi hutumika ili kuhakikisha kuna ustaarabu na utaratibu unaokubalika wakati wa maingiliano ya watu katika shughuli zao mbalimbali za kijamii, kiuchumi, kisiasa na kiutamaduni.
Majukumu mengine waliyonayo polisi zaidi ya kupambana na uhalifu ni pamoja na: upatanishi kati ya wagombanao, usalama barabarani na kutoa msaada wakati wa maafa.
Majukumu haya yanatekelezwa kwa viwango tofauti katika nchi mbalimbali kulingana na uchanga au ukomavu wa demokrasia ya nchi.
Polisi kama kiungo muhimu katika demokrasia
Polisi ni kiungo muhimu katika ujenzi wa demokrasia. Ili mradi kiungo hicho kinatimiza yafuatayo:
1. Kufanya kazi kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi na sio kwa kufuata amri au matakwa ya kiongozi mbabe au chama chenye kuendekeza udikteta;
2. Kuingilia kati maisha ya raia pale tu ambapo ni lazima kabisa lakini kwa umakini na uangalifu ili kutosababisha hasara ya maisha au mali; na
3. Wanawajibika kwa wananchi wote na sio kwa kikundi fulani cha watu katika nchi.
Hata hivyo sio kweli kuwa ni polisi tu wanaoweza kuepusha ghasia au fujo ili pawepo na utulivu, mshikamano na amani katika jamii. Yapo mambo kadhaa ambayo kwa pamoja na mchango wa polisi ndio yanayoweza kuihakikishia nchi umoja na amani ya kudumu. Mambo hayo ni pamoja na:
. jamii kuwa na maadili na tabia zinazokubalika katika maingiliano yake,kwa maneno mengine, hili linalazimisha watu kutambua kwa dhahiri na bayana ni nini ni uovu na nini ni wema, nini ni dhuluma na nini ni haki, nini ni ukweli na nini ni uongo;
. shauku ya kila mtu kutaka kuthaminiwa na kuheshimiwa na wanajamii wenzake,
. ushirikiano na kusaidiana kwa wanajamii, na
. haja ya ulinzi na kupambana na mazingira yanayoizunguka jamii.
Polisi ni muhimu kwa sababu wao peke yao kisheria ndio wanaoruhusiwa tu kutumia nguvu na kuwanyima watu uhuru wao.
Uwezo huu wa polisi unaweza kukubalika na watu fulani katika jamii (kwa kuwa polisi wanawalinda au kuwasaidia) lakini ndio huohuo unaoweza kutafsiriwa kwamba ni mabavu na uonevu na kundi linaloamini linanyimwa uhuru au haki zao za kimsingi.
Uwezo huo wa polisi kwa kweli pia unatoa mwanywa wa polisi kufanya kile wanachokitaka hata ikiwa ni kinyume cha sheria.
Utekelezaji wa kazi za upolisi katika jamii yoyote ya kidemokrasia huhitaji mizania linganifu wakati wote. Maana ukweli ni kuwa polisi wanaweza wakawa ama msaada mkubwa au hatari kubwa kwa demokrasia ya nchi fulani.
Uwezo wa polisi kutumia nguvu, kutoa adhabu za papo kwa hapo, kufuatilia na kuwapeleleza watu kwa siri hivi hivi au kwa kutumia teknolojia, kuwasimamisha, kuwasachi na kuwakamata watu kunaweza kutumika kusaidia udikteta ulioko madarakani kirahisi tu.
Polisi ni neno linalotokana na neno 'polity' ambalo huko Ulaya miaka 500 iliyopita lilitumiwa kuonesha aina ya serikali inayosimamiwa na chombo cha kisiasa. Chombo hicho kilihusishwa zaidi na maisha, afya na mali za watu. Nchi hazikuwa na polisi tunaowajua leo. Waliofanya kazi hizo walikuwa ni askari au watu maalum wa kuteuliwa na viongozi.
Katika karne ya 18 polisi wakawa wanajihusisha zaidi na masuala ya ndani na usalama wa watu.
Polepole, polisi ikageuka na kukengeuka baada ya dhana ya nchi huru zanye mipaka kuibuka kuwa taasisi ya kulinda mipaka ya nchi, usalama wa ndani na kudhibiti kisheria maingiliano ya watu katika maisha yao ya kila siku.
Nchi zinahitaji polisi wa kidemokrasia sio kikoloni
Hivi leo tunazungumzia jinsi ya kuwa na jeshi la polisi linaloendana na kanuni za kidemokrasia. Polisi wa kidemokrasia wana sifa zipi? Ni rahisi kwa kweli kueleza au kufafanua polisi wasio na mwelekeo wa kidemokrasia wakoje. Hii ni kwa sababu ni wale wote wanaovunja karibu kila msingi na kanuni ya demokrasia. Hata hivyo, tutajitahidi kuelezea kwa kifupi hapa ni namna gani polisi wa kidemokrasia wanatakiwa kuwa.
Polisi wa kidemokrasia kwa kawaida huwa na sifa hizi: hufanya kazi kwa mujibu wa katiba na sheria za nchi na sio kwa matakwa ya mkuu wa nchi au wanasiasa. Polisi hutumiwa nguvu na uwezo wao kwa umakini, uangalifu na kwa kuwajali sana wananchi. Mahalani, Uingereza, kwa ridhaa ya wananchi, hairuhusu polisi wake kutembea na silaha. Watu hutii polisi kwa kuwaheshimu kutokana na jukumu lao kijamii na sio kwa kutishwa.
Kazi za polisi wa kidemokrasia hujulikana kutokana na jinsi wanavyofanya kazi zao na namna wanavyofikia malengo yao. Mambo kama utesaji, kuua watuhumiwa papo kwa hapo, kuteka watu nyara au kuwakamata na kuwajeruhi watoto, ndugu au jamaa wa mtuhimiwa huwa hayakubaliki na hukatazwa kisheria.
Masuala kama kutumia nguvu au kumnyima mtu uhuru wake au kuwahoji watuhumiwa hufanyika kwa kufuata sheria na taratibu zilizowekwa na kwa ruhusa kutoka kiongozi au mamlaka husika.
Kwa ufupi polisi huwa na haki tu ya kumkamata mtuhumiwa lakini hawana haki ya kuchukua sheria mkononi mwao. Jambo ambalo sasa mara kwa mara linaonekana la kawaida katika jamii yetu.
Ni wajibu wa polisi wa kidemokrasia kuhakikisha sikuzote kuwa mtawala na mtawaliwa, tajiri na masikini, mnyonge na mwenye nguvu hakuna anayekuwa juu ya katiba na sheria za nchi.
Sio lazima polisi wa demokrasia nchini mwetu wafanane na wale wa nchi nyingine. Lakini ni lazima kwa polisi kuhakikisha kuwa wanawajibika kwa walipa kodi na sio kwa watawala au wale ambao kuwepo kwao kama wao kunategemea kodi anayolpa mwananchi. Baada ya hapa mengine yanakuwa ni rahisi.
Kukua na kukomaa kwa demokrasia kunategemea sana jinsi jeshi la polisi linavyolelewa katika nchi husika.
Vyama tawala visihodhi polisi
Viongozi wa chama tawala katika nchi husika wanaweza wakalilea jeshi la polisi kama vile ni jeshi la kulinda chama tawala na viongozi wake. Au wanaweza wakalilea jeshi hilo kama lenye kuwajibika kwa wananchi wote bila kujali wanatokea chama gani.
Dhuluma, uonevu, wizi na ubabe katika siasa, aghalabu, hutokea pale ambapo jeshi la polisi linalelewa kwa namna ile ya kwanza.
Hili huzaa hali ya polisi kuona kwamba chama tawala, viongozi na wanachama wake kwamba wao sikuzote ndio wenye haki, wenye kusema ukweli na walio safi kuliko wanajamii wengine na makundi au vyama vyao vya kisiasa na visivyo vya kisiasa. Tatizo linakuja pale ambapo chama husika kinakuwa ndio mwizi au jambazi na wengine ndio wanaoibiwa au kudhulumiwa. Polisi wa nchi atasimama wapi ?
Katika hali kama hii wananchi wasiokiunga chama tawala mkono na hususan wanachma na viongozi wa vyama mbadala huonekna sikuzote ni wakorofi, wabishi na wavunja sheria.
Uhusiano wa polisi na chama tawala kwa hiyo huwa ni wawenzetu na ule wa jeshi hilo na wasio wanachama wa chama tawala huwa ni uhusiano na wahalifu au wahalifu watarajiwa.
Haya yote yanaonesha upo umuhimu wa kurejea vipengele katika katiba ya nchi (na kama tutakuwa na katiba mpya ni vyema zaidi) ili kuweka uhusiano wa polisi na viongozi kwa upnade mmoja na polisi na wananchi kwa upande mwingine bayana. Katika marejeo hayo izingatiwe kuwa ni kosa kwa polisi kutumiwa na chama chohcote cha kisiasa, kikiwemo, pia chama tawala. Na endapo hili linakiukwa basi wananchi wawe na haki ya kulishtaki jeshi hilo kwa kuvunja katiba na sheria za nchi.
Nani kumteua polisi mkuu
Jeshi la polisi, hata hvyo, haliwezi kubadilika kama wakuu wa polisi wataendelea kuchaguliwa na rais na sio bunge au Jaji mkuu kama jaji huyo ndiye anayechaguliwa na bunge. Uoga wa makamanda wengi kuwa wanaweza wakatemwa na chama tawala kama wasipokipendelea chama hicho na kuvionea vyama mbadala utatoweka mara moja kama kamanda huyo atakuwa hawezi kufukuzwa kazi na rais au waziri mkuu au kiongozi mwingine wa serikali.
Katika miaka hii ambayo tunazungumzia pia kuwa na wizara chache na wizara zilizo nyingi kugeuzwa kuwa ni wakala, kamisheni, tume au taasisi maalum ni muhimu pia kuangalia ni jinsi gani jeshi hilo linaweza kugeuzwa kuwa la kukuza na kupanua demokrasia zaidi na sio jeshi la kukwaza na kuidhofisha.
Hili litahitaji jeshi letu kutokuendelea kuwa la kupokea amri za kikoloni, kibabe na kidhulumati na kutumia mabavu badala ya busara na hekima ili kujenga udugu na mshikamano muafaka katika jamii husika. Jambo ambalo husaidia wananchi kujipolisi wao wenyewe.
Aidha, hili litasaidia kuzika tabia iliyozika ya baadhi ya vyama vya siasa Afrika kujijenga kwa kuruhusu baadhi ya wanajamii kuvunja sheria za nchi na kuwalinda.
Masharti ya matumizi bora ya polisi
Ili haya yote yafanikiwe ni muhimu mambo kadhaa kufanyika:
Kwanza, lazima pawe na jitihada zinazoonekana kufanyika na kuendelezwa wakati wote na kuzuia polisi kutumiwa na chama cha kisiasa hata kama kikiwa ni chama tawala wakati huo. Katika misingi ya utawala wa kisheria hakuna chama kinachostahili kuwa juu ya sheria katika demokrasia. Vyote lazima viwe chini ya sheria. Kazi nyeti zaidi itakuwa ni kwa jeshi hilo kujua namna ya kutenga kati ya mambo ya serikali na yale ya chama au vyama tawala vya wakati huo. Na pasiwe na raia yeyote anayeweza kuonewa au kunyanyaswa kwa kuwa amefuata sheria za nchi nukta baada ya nukta.
Polisi nao wanapaswa kuwa chini ya sheria- ikiwa ni sehemu muhimu ya uwajibikaji katika mfumo wa vyama vingi. Hili lisipofanyika ni rahisi kutoa mwanya kwa watu wezi, wauaji, wauza madawa na kama hao kujipenyeza ndani ya jeshi hilo na kuunda dola ndani ya dola au serikali ndani ya serikali. Angalia kinachofanyika sasa Algeria, Arbezeijan, Kenya, Kongo, Burundi, Ethiopia, Misri, Moldovia, Burma, Mexico, Colombia na Zimbabwe.
Kurejesha imani ya wananchi kwa jeshi la polisi kama ilivyokuwa katika siku za mwanzo za uhuru itatupasa tuyasuke upya majeshi yetu ya polisi. Polisi na wananchi laizma wawe ni pande mbili zinazotegemeana kwa faid aya jamhuri nzima. Pasiwe na upand unaougeuza upande mwingine kuwa ni buzi la kuchuna mchana kweupe!
Ili uhuru, usawa na haki viimarike katika nchi ni muhimu sana kwa jeshi la polisi kuonekana kama ni walinda haki na watu sio tu wanaokubalika bali wanaothaminiwa sana na jamii. Mfumo unaowafanya wananchi walione jeshi la polisi kama ni jeshi la watu wabaya na wasioaminika haliwezi kujenga jamii bora na nchi inayoheshimika. Na mara nyingi hali hutokea pale jeshi hilo linapogeuzwa kuwa ni jeshi la 'wanyama wakali' waliokusanywa kumlinda mmiliki wao hata kama mmiliki huyo akiwa jambazi.
Ndio kusema kwamba jeshi la polisi linastahili kurudishwa chuoni. Huko watajifunza kuwa demokrasia sio tu jambo zuri kwa nchi bali kwao pia na kwa wananchi wenzao.
Itapaswa wajue kwamba raia ni dada, kaka, baba, mama, bibi na babu zao. Na chochote wanachokifanya kiwe kizuri au kibaya hakiwezi kutoka nje ya mduara ambao wote tunacheza humo.
Wito wa polisi katika nchi inayotaka kujenga demokrasia inayofanya kazi kikwelikweli ni lazima uwe -'usalama na ulinzi kwa wote bila kubagua.'
Kukua na kuimarika demokrasia na polisi
Zipo njia mbalimbali ambazo nchi inaweza ikatumia ili kukuza na kupanua demokrasia. Njia hizo ni pamoja kwa haraka haraka na masuala kama:
. Kutenganisha kazi zao na masuala ya kisiasa.
. Kutokubali kuingizwa katika hali au mitego inayoweza kusababisha wao kuwa ndio waanzishaji fujo mahala fulani. Hii ni pamoja na kukataa kuingia kwenye maeneo ya shule na vyuo. Tabia iliyozuka siku za karibuni kuruhusu mkuu wa shule kuwaita polisi au wanajeshi kuvamia vyuo sio uamuzi wa busara wala hekima. Kila shule au chuo kinastahili kuwa na walinzi wake wanaotenda haki kwa wote bila kujali nafasi au cheo cha mtu katika taasisi husika;
. Kurahisisha na sio kuzuia kufanyika kwa mikutano na maandamano ya wananchi. Ni kosa la katiba na kisheria kuwazuia wananchi popote pale nchini kufanya mikutano au maandamano;
. Kuhakikisha kuna mwingiliano kati ya mapolisi na raia kupitia mambo mbalimbali kama vile michezo, starehe, uwekezaji na shughuli za maendeleo ya kijamii.
. Kusaidia makundi ya kijamii ikiwemo vyama vya kisiasa kuendesha mambo yao katika hali ya utulivu na usalama.
. Kutokubali kuwepo kwa wezi, makuwadi, vibaka, dhulumati, wala rushwa, walevi, wazinzi, matapeli na wababishaji katika jeshi hilo.
Ikiwa hayo hapo juu yatafnyika bila shaka kutakuwa na uhusiano mzuri kati ya polisi na jamii. Uhusiano mzuri kati ya polisi na jamii huchangia kwa kiasi kikubwa kuchanua na kustawi kwa demokrasia na shughuli zote zinazoendana na ujenzi wake.
Aidha Polisi wanastahili pia kufanya kazi kwa ushirikiano na ukaribu zaidi na mahakama, bunge na viongozi wa kijamii ili kukuza na kupanua demokrasia wakati wote.
Polisi ni watumishi sio mabwana
Aidha serikali na wakuu wa polisi wakati mwingine hujisahau na kudhani kuwa wao ni mabwana na wananchi ni watwana. Katika demokrasia inayofanya kazi sawasawa yeyote anayejisahau kwamba ni mtumishi wa wananchi anapaswa kuondolewa mara moja na nafasi yake kuchukuliwa na yule anayetambua ukweli huu kuwa watumishi wa serikali wakiwmo polisi ni watumishi wa wananchi na sio mabwana wao. Hili la polisi kuwa watumishi na sio mabwana ni jambo muhimu sana. Ni pale ambapo aghalabu polisi wamepewa vichwa na viongozi kisha wakajiona wao ndio mabwana kwa sababu wana silaha na nguvu za dola ndipo ambapo nchi zimechafuka na kutokea uvunjaji haki wa kutisha na hata mauaji ya kimbari. Tuliepuke hili kwa kuwakumbusha polisi wetu sikuzote kuwa wao ni watumishi wa watu na sio mabwana.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
Saturday, June 13, 2009
DEMOKRASIA, VYAMA NA HAZINA
Marx na Demokrasia.
YULE mkomunisti maarufu duniani mwenye asili ya Kijerumani, Profesa Karl Marx aliwahi kusema kwamba : " Mfumo wa Kidemokrasia sio mfumo endelevu. Huweza kudumu tu hadi pale viongozi wanapogundua kwamba wanaweza kupora Hazina na wasifanywe lolote na umma. Basi watakapopora Hazina ndio unakuwa mwisho wa demokrasia.'
Hata hivyo, demokrasia anayozungumzia Marx hapa sio ile ambayo wananchi ndio wameshika mpini. Hii ni demokrasia ambayo wananchi wameshika makali na viongozi ndio walioshika mpini.
Anayoizungumzia Marx ni demokrasia ambayo viongozi wachache na chama tawala ndivyo vyenye sauti na uwezo wa kifedha na mwingineo na watumia majaliwa yao hayo kuzuia kuwepo kwa demokrasia ya kweli inayoendeshwa kwa nguvu za wananchi.
Ni demokrasia ambayo haina mashiko ya kikatiba, nguzo zingine za kitaifa haziheshimiwi na zinaburuzwa na serikali, wanasiasa wanawatumia watumishi wa serikali kukidhi matakwa na mahitaji yao na siyo yale ya wananchi na wanaoamua kuwepo au kutokuwepo kwa mabadiliko sio wananchi bali wanasiasa wachache.
Binafsi yangu ili mradi wananchi wenye nchi wana uwezo na nguvu ya kuwawajibisha viongozi wao jambo kama hilo la kufilisiwa kwa hazina haliwezi kutokea na viongozi wasiwajibishwe. Na huu ndio uzuri na ubora wa demokrasia. Humzawadia anayeijenga na kuiimarisha na kumwadhibu anayetaka kuiharibu ikiwa kila kitu kinakwenda sawa na wananchi ndio watawala (kwa tasihili ya kufanya maamuzi ya kuwaondoa au kuwaweka watu wengine madarakani ) na sio chama au kikundi cha watu wachache katika nchi.
Katika demokrasia ya kweli inayosimamiwa na wananchi watu hawamuheshimu wala hawamwogopi mtu au chama fulani eti kwa kuwa kimeshika madaraka.
Mtu na chama chochote kile huheshimiwa na kuthaminiwa kutokana na jitihada zake za kutetea mamlaka ya wananchi dhidi ya watawala wao, uwajibikaji wa viongozi kwa wananchi na kulindwa kwa maslahi ya walio wengi dhidi ya vitimbi vya watu wa chache katika nchi.
Katika demokrasia ya kweli hakuna kiongozi yeyote au mtumishi yeyote toka ngazi ya chini hadi juu ambaye analindwa anapokiuka misingi ya sheria na katiba ya nchi.
Kiongozi au chama kinachopora au kuwalaghai au kuwatapeli wananchi kwa namna yoyote ile ni adui wa demokrasia na maendeleo ya watu.
Demokrasia haiwezi kukua wala kuendelezwa katika nchi yoyote ile ambayo viongozi, vyama vya kisiasa na taasisi chache zina njia lukuki za kupata fedha kirahisi na viongozi na vyama vingine vingi vinazuiwa, vinatiliwa ngumu au mikwara, vinanyimwa, havipewi au havipati fursa kama hiyo. Wakati mwingine viongozi wengine na vyama vingine vinazuiwa hata fursa za kuendesha shughuli halali za kujiingizia mapato ili kuendesha mambo yao bila kutegemea sehemu nyingine.
Katika nchi nyingi za Kiafrika vyama tawala hutumia nafasi waliyo nayo kuchota fedha toka Hazina na mabenki; wakusanyaji kodi, makadirio hewa yaliyoko kwenye bajeti na kadhalika; kudanganya kwa kalamu katika masuala ya ununuzi wa vifaa ghali vinavyodaiwa kuhitajika kitaifa hata kama ' watu watakula manyasi' au na serikali na kisha kulipwa fedha nyingi zaidi kuliko bei halali ya chombo husika; kutangaza hali ya njaa na kisha kuuza chakula cha njaa na kuweka mfukoni pesa ipatikanayo; kuchota toka Mifuko ya Pensheni, Hifadhi za Jamii, Bima mbalimbali na mashirika mengine ya umma fedha kwa matumizi ya chama cha kisiasa kinyume na sheria za nchi.
Aghalabu panapotokea kisingizio kama kile cha Ugaidi au 'udobi wa fedha' wajanja huitumia fursa hiyo pia kama njia ya kuwapatia viongozi wezi na walafi na chama husika fedha. Hakuna anayejali kama fedha hiyo ni ya jumuiya fulani au mtu fulani na kamwe haikutumwa kwa ajili ya matumizi mabaya. Baadhi ya waumini hapa nchini bado wana majeraha na maumivu ya fedha zao kukamatwa na kishwa kuliwa kwa namna isiyofahamika huku maendeleo yao katika kila nyanja yakibaki nyuma kutokana na kitendo hicho.
Je, haya hutokea kwa sababu chama cha siasa husika kinahitaji sana fedha za matumizi ya kawaida?
Hapana haya yote, aghalabu, hayafanyiki kwa kukidhi fedha za matumizi ya kila siku bali fedha kwa ajili ya kuhonga na kuwarubuni wananchi ili wakipigie tena kura chama husika. Hii ni rushwa tunayoweza kuitwa mama wa Rushwa zote. Ni rushwa hii ndiyo inayokuwa gugu lenye sumu kali na lisiloruhusu kabisa demokrasia kukua, kuota mizizi mirefu na kupanuka kwa mapana na marefu.
Mbio za chama chochote cha siasa zinazoelekea katika kujilimbikizia fedha kutoka vyanzo vyenye mashaka ni mbio za kuzuia na kupiga vita kukua na kuimarika kwa demokrasia katika nchi yoyote ile duniani. Katika baadhi ya nchi vyama vya kisiasa vinavyotawala vimekuwa vikiiba ili kuhonga wanasiasa wa vyama vya upinzani ili kuvivuruga na kukipa nafasi chama tawala kuendelea kubaki madarakani.
Wanasiasa ni wajasiriamali dhaifu
Historia ya nchi nyingi za Kiafrika zinaonesha kuwa wanasiasa wetu wanajua tu maneno au siasa lakini hawajui lolote kuhusu biashara na jinsi ya kuzalisha mali kwa kutumia akili na mtaji wako mwenyewe. Hii ni tofauti na China na Cuba ambako viongozi wa Kikomunisti sio haba wamekusuru kujua siasa wanayoikubali na vilevile kuwa werevu kuhusu biashara na kubwa zaidi kujua namna ya kuwaachia watumishi wa umma kuendesha biashara tulizoshindwa sisi kuendesha kwa kutumia mashirika ya umma kwa namna ambayo nchi hiyo leo inashindana na nchi zilizokuwa zikifuata moja kwa moja siasa za kibepari katika uchumi.
Kwa kuwa viongozi wetu wa siasa hawajui na hawawezi kufanya biashara wamekuwa wakitafuta njia za mkato kwa kufanya biashara za kijanja kwa kuwatumia watu ambao tayari ni wafanyabiashara au walanguzi wa hiki au kile.
Hata hivyo, bado kunabakia tatizo. Kweli mtu anakuwa na biashara kwa kumtumia mtu fulani. Lakini mwanasiasa huyo au mtumishi huyo wa umma anashindwa kufuatilia biashara yake kikamilifu. Matokeo yake anadanganywa na hata wakati mwingine kuzikwa na mwisho wa yote asiambulie lolote.
Rasilimali watu katika nchi nyingi za Kiafrika imeharibiwa na wanasiasa na viongozi wengine kutokana na kujifunza zaidi mabaya na sio mazuri ya wakubwa wao. Hili sio jambo la ajabu. Kama kiongozi wako ni mwizi na mwongo uwezekano wa wewe kuwa kinyume cha hivyo ni mdogo sana. Na ndivyo ilivyo sasa katika nchi nyingi za Kiafrika ambako utakuta kuna piramidi ya wezi toka chini hadi juu. Na wakati mwingine wa chini huiba zaidi kuliko wale wa juu kabisa.
Tofauti na China tumeshindwa kuamini kuwa kwa kufanya kazi ndani ya mashirika ya umma wote tunaweza kuwa na hali bora ya maisha. Na tunapozifanya hizi kama watu binafsi tunaishia kulizwa na walio wajanja zaidi yetu.
Hebu tuvute hatua moja nyuma. Je, hivi kweli inawezekana kila mtu akawa mwanasiasa na wakati huo huo mfanyabiashara?
Jibu ni ndio. Lakini wanaoweza kufanikiwa katika yote mawili ni wachache sana. Na mifano ipo tosha duniani. Wengi wetu tukijaribu hivyo tunaishia kuwa tatizo kwetu wenyewe, kwa watu wetu na nchi yetu.
Kwa hatua ya maendeleo tuliyofikia hivi sasa ninashauri kwamba yeyote anayechaguliwa kama mbunge na kisha kuteuliwa kama waziri aache kusimamia moja kwa moja shughuli zake binafsi za kiuchumi na biashara, na ili kuleta imani kubwa zaidi kwa watu na nchi yao akaacha kabisa shughuli hizo.
Kwa upande wa serikali ni lazima mawaziri wetu walipwe mishahara na mafao mazuri wakati wa kustaafu ili wasiwe na kishawishi cha kutafuta fedha kwa njia nyingine. Yeyote atakayevunja mwiko huu basi tusiwe na subira wala huruma naye.
Kwa namna hii mawaziri watakuwa wakiishi, kufanya kazi, kulala na kuamka wakifikiria tu majukumu yao ya kujenga serikali na nchi bora zaidi kupitia wizara zao na sio kitu kingine.
Siasa, wafanyabiashara na matajiri
Nchi inapokuwa na mawaziri wenye viwanda, mashamba makubwa, biashara kubwa, makampuni ya uwakili au makampuni ya ukaguzi haiwezi kuwa na watumishi safi na bora ambao hawatachanganya shughuli zao na zile za serikali. Itakuwa ni bora zaidi kwa hiyo kuwa na watu wanaompa Kaizari chake na Muumba naye akapewa chake.
Kutokana na hili upo umuhimu wa kuendelea kutenga shughuli za chama na serikali kwa namna ambayo kila mmoja kati yao atakuwa anatumia chake na sio cha mwingine.
Tathmini ya serikali na usimamizi wa fedha
Usimamizi wa masuala ya fedha katika nchi nyingi hapa Afrika hauridhishi. Hali hii haisababishwi na kukosa wahasibu na wataalamu wengine wa mambo ya fedha. La hasha. Hili hutokea kwa sababu wataalamu hao hawaruhusiwi na wemye serikali, wanasiasa na makuwadi wao kufanya kazi kwa kuzingatia utaalamu wao na kanuni na taratibu za kazi zao.
Kama wangeruhusiwa kufanya hivyo basi ni dhahiri lisingelikuwa jambo la kawaida kila serikali mpya inayoingia madarakani kukuta mfuko wa hazina ni mtupu.
Njia mojawapo kwa hiyo ya kukuza na kuimarisha demokrasia Afrika ni kuhakikisha kuwa masuala ya usimamizi wa fedha yanatengwa na kazi za serikali na chama tawala. Aidha wataalamu wa mambo ya fedha ni lazima waachiwe uhuru wa kufanya kazi zao kwa mujibu wa utaalamu na kanuni zao za utendaji kazi.
Tunaweza kuchelewa katika mengine lakini sio katika kuwa na serikali kwa teknohama kwa upande wa uhasibu na fedha. Katika dunia ya leo ni lazima mahesabu ya mapato na matumizi ya serikali yafuatiliwe kila mwisho wa siku. Iwe ni mwiko kwa watumishi wa serikali wanaohusika na mambo ya fedha kuondoka kazini bila kufunga mahesabu ya kila siku kama inavyofanyika katika benki.
Wakuu wa nchi na fedha
Baadhi ya wakuu wa nchi wamekuwa ni wavivu wa kufuatlia masuala ya fedha na kukaimu kazi hizo wakati mwingine kwa wasaidizi wao ambao si wenye uchungu na fedha na maendeleo ya watu na nchi yao na wala pia si waaminifu.
Kwa mfano nyakati zingine makuwadi au walanguzi wanaotumiwa na viongozi hao wamekuwa wakiwaamrisha wasimamizi wa masuala ya fedha na mawaziri wa hazina kufanya mambo ambayo kiongozi mwenyewe wa nchi hana habari nayo licha ya kuyaruhusu au kutoa kibali chake. Na haya mara nyingi yamekuwa yakifanyika kwa kisingizio cha kukipatia chama tawala fedha za kukirejesha tena madarakani.
Aghalabu wengi wamekuwa wakiridhika na ripoti za kupikwa. Ili mradi wao wanapata mishahara na maruputupu yao, wanajengewa nyumba nzuri kila sehemu ya nchi huku wake na watoto wao nao wakinufaika na matunda haramu ya walanguzi hao na wanakuwa hawana ari ya kufuatilia kila shilingi inayoingia na kutoka katika mfuko wa hazina. Matokeo yake meli ya nchi inaweza kuzama huku nahodha kalala na hana habari na kinachoendelea.
Rais asiwe tu Amiri Jeshi bali pia Amiri wa Hazina
Dawa yangu kwa hili sikuzote imekuwa ni kushauri kwamba kama vile Rais wa nchi anavyokuwa ni jemadari wa majeshi yetu basi Rais huyo ni lazima pia awe Jemadari wa masuala ya fedha. Hili likiimanisha kwamba hakuna lolote kuhusu matumizi makubwa ya fedha linaloweza kufanyika bila ruhusa na ridhaa ya kimaandishi ya mkuu wa nchi.
Hii ni akili ya kawaida tu. Maana kati yetu sote hapa hakuna aliyewahi kuona kampuni ambayo Meneja wake mkuu au Mkurugenzi Mkuu au mwenye Kampuni anakubali kuwaachia wasaidizi wake masuala yote yanayohusu mapato na matumizi ya kampuni. Kampuni yenye watu wa aina hiyo ni dhahiri watahitajika kupimwa akili zao.
Umefika wakati wa Waafrika kuzitaka serikali zao kuwa bayana katika kuonesha ni kina nani wanahusika na masuala ya fedha kwa namna ambayo kila hatua inafuatiliwa, kuchunguzwa na kudhibitiwa na hatua nyingine.
Haiwezekani kufuatana na kanuni za uhasibu na ukaguzi, mathalani, kwa mtu mmoja kuwa ndiye huyohuyo anayepokea fedha, anayeandika risiti, anayehifadhi fedha, anayehakikisha fedha iko sawa na anayepeleka na kutoa fedha benki.
Aidha haiwezekani kwa waziri wa fedha au gavana wa benki kutoa fedha eti kwa kuwa Rais ndiye katuma tena kwa maneno bila barua yoyote wala kuzungumza na mkuu huyo kwa simu za mkononi ambazo hata mkulima kijijini anayo leo. Hivi kweli unaweza kuendesha nchi kwa kutuma kwa maneno bila maandishi yoyote au kuandika hilo nyuma ya bahasha chafu kama una nia nzuri na watu na nchi yako ?
Siasa, Serikali na Teknohama
Katika miaka hii ya teknolojia zinarahisisha na kuongeza udhibiti mzuri wa fedha ni muhimu pia kuangalia
ni jinsi gani kwa kuwa na Serikali-T au serikali ya Teknohama kifedha inavyoweza kuanzishwa na kuendelezwa kwa ajili ya kuwa na mtandao hai kati ya Benki Kuu, Wizara, Taasisi Kubwa za Fedha na Ikulu husika.
Demokrasia halisi inakuwepo pale ambapo:
-kuna mfumo unaoruhusu mwingiliano wa watu wote wakati wote;
-viongozi na taasisi za serikali kufikiwa wakati wote;
-hulka ya kisiasa inayokubali mawazo mbadala kushindana wakati wote;
-na wakati huohuo kuruhusu ushiriki wa walio wengi hadi kufikia maamuzi ya mwisho kuhusu malengo ya kuchumi, kijamii na kiutamaduni.
Demokrasia hutenga wanasiasa a mangimeza
Vilevile, demokrasia hustawi pale ambapo miingiliano ya vionogzi wa serikali na watumishi wa serikali haiwayumbishi kundi la pili kichama au kisiasa na wanakuwa huru kufanya maamuzi yao kwa mujibu wa taaluma zao. Watumishi hawa ni pamoja na wale wa Hazina na Benki Kuu ya nchi.
Miingiliano hii hufanyika katika ngazi mbalimbali kipekee wakati huohuo.
Miingiliano hii hutawaliwa na mazungumzo au mijadala isiyokwisha juu ya fani au nyanja mbalimbali za maisha.
Suala lingine muhimu katika mada hii ni ulazima wa kuwa na sheria na taratibu wazi za uwajibikaji katika michakato ya vyama kujipatia fedha za kuendesha kazi zao za kawaida na zile za kuendesha kampeni za uchaguzi kwa nyakati mbalimbali.
Kama suala hili linakuwa gizani kwa maana kwamba hatujui jinsi vyama vinavyopata fedha zao, kiasi wanachopata na watu au taasisi zinazovipa vyama fedha basi ni rahisi nchi hii kuuzwa bila wananchi wake kujua.
Demokrasia badala ya kuchangia kukua kiuchumi kwa nchi itakuwa inachangia kuingiza nchi katika madeni ya kiajabu ajabu ambayo sio tu yatazuia nchi kupata maendeleo ya kiuchumi na kijamii lakini vile yatakuwa ndio chanzo cha kuua amani, utulivu na mshikamano katika nchi.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
YULE mkomunisti maarufu duniani mwenye asili ya Kijerumani, Profesa Karl Marx aliwahi kusema kwamba : " Mfumo wa Kidemokrasia sio mfumo endelevu. Huweza kudumu tu hadi pale viongozi wanapogundua kwamba wanaweza kupora Hazina na wasifanywe lolote na umma. Basi watakapopora Hazina ndio unakuwa mwisho wa demokrasia.'
Hata hivyo, demokrasia anayozungumzia Marx hapa sio ile ambayo wananchi ndio wameshika mpini. Hii ni demokrasia ambayo wananchi wameshika makali na viongozi ndio walioshika mpini.
Anayoizungumzia Marx ni demokrasia ambayo viongozi wachache na chama tawala ndivyo vyenye sauti na uwezo wa kifedha na mwingineo na watumia majaliwa yao hayo kuzuia kuwepo kwa demokrasia ya kweli inayoendeshwa kwa nguvu za wananchi.
Ni demokrasia ambayo haina mashiko ya kikatiba, nguzo zingine za kitaifa haziheshimiwi na zinaburuzwa na serikali, wanasiasa wanawatumia watumishi wa serikali kukidhi matakwa na mahitaji yao na siyo yale ya wananchi na wanaoamua kuwepo au kutokuwepo kwa mabadiliko sio wananchi bali wanasiasa wachache.
Binafsi yangu ili mradi wananchi wenye nchi wana uwezo na nguvu ya kuwawajibisha viongozi wao jambo kama hilo la kufilisiwa kwa hazina haliwezi kutokea na viongozi wasiwajibishwe. Na huu ndio uzuri na ubora wa demokrasia. Humzawadia anayeijenga na kuiimarisha na kumwadhibu anayetaka kuiharibu ikiwa kila kitu kinakwenda sawa na wananchi ndio watawala (kwa tasihili ya kufanya maamuzi ya kuwaondoa au kuwaweka watu wengine madarakani ) na sio chama au kikundi cha watu wachache katika nchi.
Katika demokrasia ya kweli inayosimamiwa na wananchi watu hawamuheshimu wala hawamwogopi mtu au chama fulani eti kwa kuwa kimeshika madaraka.
Mtu na chama chochote kile huheshimiwa na kuthaminiwa kutokana na jitihada zake za kutetea mamlaka ya wananchi dhidi ya watawala wao, uwajibikaji wa viongozi kwa wananchi na kulindwa kwa maslahi ya walio wengi dhidi ya vitimbi vya watu wa chache katika nchi.
Katika demokrasia ya kweli hakuna kiongozi yeyote au mtumishi yeyote toka ngazi ya chini hadi juu ambaye analindwa anapokiuka misingi ya sheria na katiba ya nchi.
Kiongozi au chama kinachopora au kuwalaghai au kuwatapeli wananchi kwa namna yoyote ile ni adui wa demokrasia na maendeleo ya watu.
Demokrasia haiwezi kukua wala kuendelezwa katika nchi yoyote ile ambayo viongozi, vyama vya kisiasa na taasisi chache zina njia lukuki za kupata fedha kirahisi na viongozi na vyama vingine vingi vinazuiwa, vinatiliwa ngumu au mikwara, vinanyimwa, havipewi au havipati fursa kama hiyo. Wakati mwingine viongozi wengine na vyama vingine vinazuiwa hata fursa za kuendesha shughuli halali za kujiingizia mapato ili kuendesha mambo yao bila kutegemea sehemu nyingine.
Katika nchi nyingi za Kiafrika vyama tawala hutumia nafasi waliyo nayo kuchota fedha toka Hazina na mabenki; wakusanyaji kodi, makadirio hewa yaliyoko kwenye bajeti na kadhalika; kudanganya kwa kalamu katika masuala ya ununuzi wa vifaa ghali vinavyodaiwa kuhitajika kitaifa hata kama ' watu watakula manyasi' au na serikali na kisha kulipwa fedha nyingi zaidi kuliko bei halali ya chombo husika; kutangaza hali ya njaa na kisha kuuza chakula cha njaa na kuweka mfukoni pesa ipatikanayo; kuchota toka Mifuko ya Pensheni, Hifadhi za Jamii, Bima mbalimbali na mashirika mengine ya umma fedha kwa matumizi ya chama cha kisiasa kinyume na sheria za nchi.
Aghalabu panapotokea kisingizio kama kile cha Ugaidi au 'udobi wa fedha' wajanja huitumia fursa hiyo pia kama njia ya kuwapatia viongozi wezi na walafi na chama husika fedha. Hakuna anayejali kama fedha hiyo ni ya jumuiya fulani au mtu fulani na kamwe haikutumwa kwa ajili ya matumizi mabaya. Baadhi ya waumini hapa nchini bado wana majeraha na maumivu ya fedha zao kukamatwa na kishwa kuliwa kwa namna isiyofahamika huku maendeleo yao katika kila nyanja yakibaki nyuma kutokana na kitendo hicho.
Je, haya hutokea kwa sababu chama cha siasa husika kinahitaji sana fedha za matumizi ya kawaida?
Hapana haya yote, aghalabu, hayafanyiki kwa kukidhi fedha za matumizi ya kila siku bali fedha kwa ajili ya kuhonga na kuwarubuni wananchi ili wakipigie tena kura chama husika. Hii ni rushwa tunayoweza kuitwa mama wa Rushwa zote. Ni rushwa hii ndiyo inayokuwa gugu lenye sumu kali na lisiloruhusu kabisa demokrasia kukua, kuota mizizi mirefu na kupanuka kwa mapana na marefu.
Mbio za chama chochote cha siasa zinazoelekea katika kujilimbikizia fedha kutoka vyanzo vyenye mashaka ni mbio za kuzuia na kupiga vita kukua na kuimarika kwa demokrasia katika nchi yoyote ile duniani. Katika baadhi ya nchi vyama vya kisiasa vinavyotawala vimekuwa vikiiba ili kuhonga wanasiasa wa vyama vya upinzani ili kuvivuruga na kukipa nafasi chama tawala kuendelea kubaki madarakani.
Wanasiasa ni wajasiriamali dhaifu
Historia ya nchi nyingi za Kiafrika zinaonesha kuwa wanasiasa wetu wanajua tu maneno au siasa lakini hawajui lolote kuhusu biashara na jinsi ya kuzalisha mali kwa kutumia akili na mtaji wako mwenyewe. Hii ni tofauti na China na Cuba ambako viongozi wa Kikomunisti sio haba wamekusuru kujua siasa wanayoikubali na vilevile kuwa werevu kuhusu biashara na kubwa zaidi kujua namna ya kuwaachia watumishi wa umma kuendesha biashara tulizoshindwa sisi kuendesha kwa kutumia mashirika ya umma kwa namna ambayo nchi hiyo leo inashindana na nchi zilizokuwa zikifuata moja kwa moja siasa za kibepari katika uchumi.
Kwa kuwa viongozi wetu wa siasa hawajui na hawawezi kufanya biashara wamekuwa wakitafuta njia za mkato kwa kufanya biashara za kijanja kwa kuwatumia watu ambao tayari ni wafanyabiashara au walanguzi wa hiki au kile.
Hata hivyo, bado kunabakia tatizo. Kweli mtu anakuwa na biashara kwa kumtumia mtu fulani. Lakini mwanasiasa huyo au mtumishi huyo wa umma anashindwa kufuatilia biashara yake kikamilifu. Matokeo yake anadanganywa na hata wakati mwingine kuzikwa na mwisho wa yote asiambulie lolote.
Rasilimali watu katika nchi nyingi za Kiafrika imeharibiwa na wanasiasa na viongozi wengine kutokana na kujifunza zaidi mabaya na sio mazuri ya wakubwa wao. Hili sio jambo la ajabu. Kama kiongozi wako ni mwizi na mwongo uwezekano wa wewe kuwa kinyume cha hivyo ni mdogo sana. Na ndivyo ilivyo sasa katika nchi nyingi za Kiafrika ambako utakuta kuna piramidi ya wezi toka chini hadi juu. Na wakati mwingine wa chini huiba zaidi kuliko wale wa juu kabisa.
Tofauti na China tumeshindwa kuamini kuwa kwa kufanya kazi ndani ya mashirika ya umma wote tunaweza kuwa na hali bora ya maisha. Na tunapozifanya hizi kama watu binafsi tunaishia kulizwa na walio wajanja zaidi yetu.
Hebu tuvute hatua moja nyuma. Je, hivi kweli inawezekana kila mtu akawa mwanasiasa na wakati huo huo mfanyabiashara?
Jibu ni ndio. Lakini wanaoweza kufanikiwa katika yote mawili ni wachache sana. Na mifano ipo tosha duniani. Wengi wetu tukijaribu hivyo tunaishia kuwa tatizo kwetu wenyewe, kwa watu wetu na nchi yetu.
Kwa hatua ya maendeleo tuliyofikia hivi sasa ninashauri kwamba yeyote anayechaguliwa kama mbunge na kisha kuteuliwa kama waziri aache kusimamia moja kwa moja shughuli zake binafsi za kiuchumi na biashara, na ili kuleta imani kubwa zaidi kwa watu na nchi yao akaacha kabisa shughuli hizo.
Kwa upande wa serikali ni lazima mawaziri wetu walipwe mishahara na mafao mazuri wakati wa kustaafu ili wasiwe na kishawishi cha kutafuta fedha kwa njia nyingine. Yeyote atakayevunja mwiko huu basi tusiwe na subira wala huruma naye.
Kwa namna hii mawaziri watakuwa wakiishi, kufanya kazi, kulala na kuamka wakifikiria tu majukumu yao ya kujenga serikali na nchi bora zaidi kupitia wizara zao na sio kitu kingine.
Siasa, wafanyabiashara na matajiri
Nchi inapokuwa na mawaziri wenye viwanda, mashamba makubwa, biashara kubwa, makampuni ya uwakili au makampuni ya ukaguzi haiwezi kuwa na watumishi safi na bora ambao hawatachanganya shughuli zao na zile za serikali. Itakuwa ni bora zaidi kwa hiyo kuwa na watu wanaompa Kaizari chake na Muumba naye akapewa chake.
Kutokana na hili upo umuhimu wa kuendelea kutenga shughuli za chama na serikali kwa namna ambayo kila mmoja kati yao atakuwa anatumia chake na sio cha mwingine.
Tathmini ya serikali na usimamizi wa fedha
Usimamizi wa masuala ya fedha katika nchi nyingi hapa Afrika hauridhishi. Hali hii haisababishwi na kukosa wahasibu na wataalamu wengine wa mambo ya fedha. La hasha. Hili hutokea kwa sababu wataalamu hao hawaruhusiwi na wemye serikali, wanasiasa na makuwadi wao kufanya kazi kwa kuzingatia utaalamu wao na kanuni na taratibu za kazi zao.
Kama wangeruhusiwa kufanya hivyo basi ni dhahiri lisingelikuwa jambo la kawaida kila serikali mpya inayoingia madarakani kukuta mfuko wa hazina ni mtupu.
Njia mojawapo kwa hiyo ya kukuza na kuimarisha demokrasia Afrika ni kuhakikisha kuwa masuala ya usimamizi wa fedha yanatengwa na kazi za serikali na chama tawala. Aidha wataalamu wa mambo ya fedha ni lazima waachiwe uhuru wa kufanya kazi zao kwa mujibu wa utaalamu na kanuni zao za utendaji kazi.
Tunaweza kuchelewa katika mengine lakini sio katika kuwa na serikali kwa teknohama kwa upande wa uhasibu na fedha. Katika dunia ya leo ni lazima mahesabu ya mapato na matumizi ya serikali yafuatiliwe kila mwisho wa siku. Iwe ni mwiko kwa watumishi wa serikali wanaohusika na mambo ya fedha kuondoka kazini bila kufunga mahesabu ya kila siku kama inavyofanyika katika benki.
Wakuu wa nchi na fedha
Baadhi ya wakuu wa nchi wamekuwa ni wavivu wa kufuatlia masuala ya fedha na kukaimu kazi hizo wakati mwingine kwa wasaidizi wao ambao si wenye uchungu na fedha na maendeleo ya watu na nchi yao na wala pia si waaminifu.
Kwa mfano nyakati zingine makuwadi au walanguzi wanaotumiwa na viongozi hao wamekuwa wakiwaamrisha wasimamizi wa masuala ya fedha na mawaziri wa hazina kufanya mambo ambayo kiongozi mwenyewe wa nchi hana habari nayo licha ya kuyaruhusu au kutoa kibali chake. Na haya mara nyingi yamekuwa yakifanyika kwa kisingizio cha kukipatia chama tawala fedha za kukirejesha tena madarakani.
Aghalabu wengi wamekuwa wakiridhika na ripoti za kupikwa. Ili mradi wao wanapata mishahara na maruputupu yao, wanajengewa nyumba nzuri kila sehemu ya nchi huku wake na watoto wao nao wakinufaika na matunda haramu ya walanguzi hao na wanakuwa hawana ari ya kufuatilia kila shilingi inayoingia na kutoka katika mfuko wa hazina. Matokeo yake meli ya nchi inaweza kuzama huku nahodha kalala na hana habari na kinachoendelea.
Rais asiwe tu Amiri Jeshi bali pia Amiri wa Hazina
Dawa yangu kwa hili sikuzote imekuwa ni kushauri kwamba kama vile Rais wa nchi anavyokuwa ni jemadari wa majeshi yetu basi Rais huyo ni lazima pia awe Jemadari wa masuala ya fedha. Hili likiimanisha kwamba hakuna lolote kuhusu matumizi makubwa ya fedha linaloweza kufanyika bila ruhusa na ridhaa ya kimaandishi ya mkuu wa nchi.
Hii ni akili ya kawaida tu. Maana kati yetu sote hapa hakuna aliyewahi kuona kampuni ambayo Meneja wake mkuu au Mkurugenzi Mkuu au mwenye Kampuni anakubali kuwaachia wasaidizi wake masuala yote yanayohusu mapato na matumizi ya kampuni. Kampuni yenye watu wa aina hiyo ni dhahiri watahitajika kupimwa akili zao.
Umefika wakati wa Waafrika kuzitaka serikali zao kuwa bayana katika kuonesha ni kina nani wanahusika na masuala ya fedha kwa namna ambayo kila hatua inafuatiliwa, kuchunguzwa na kudhibitiwa na hatua nyingine.
Haiwezekani kufuatana na kanuni za uhasibu na ukaguzi, mathalani, kwa mtu mmoja kuwa ndiye huyohuyo anayepokea fedha, anayeandika risiti, anayehifadhi fedha, anayehakikisha fedha iko sawa na anayepeleka na kutoa fedha benki.
Aidha haiwezekani kwa waziri wa fedha au gavana wa benki kutoa fedha eti kwa kuwa Rais ndiye katuma tena kwa maneno bila barua yoyote wala kuzungumza na mkuu huyo kwa simu za mkononi ambazo hata mkulima kijijini anayo leo. Hivi kweli unaweza kuendesha nchi kwa kutuma kwa maneno bila maandishi yoyote au kuandika hilo nyuma ya bahasha chafu kama una nia nzuri na watu na nchi yako ?
Siasa, Serikali na Teknohama
Katika miaka hii ya teknolojia zinarahisisha na kuongeza udhibiti mzuri wa fedha ni muhimu pia kuangalia
ni jinsi gani kwa kuwa na Serikali-T au serikali ya Teknohama kifedha inavyoweza kuanzishwa na kuendelezwa kwa ajili ya kuwa na mtandao hai kati ya Benki Kuu, Wizara, Taasisi Kubwa za Fedha na Ikulu husika.
Demokrasia halisi inakuwepo pale ambapo:
-kuna mfumo unaoruhusu mwingiliano wa watu wote wakati wote;
-viongozi na taasisi za serikali kufikiwa wakati wote;
-hulka ya kisiasa inayokubali mawazo mbadala kushindana wakati wote;
-na wakati huohuo kuruhusu ushiriki wa walio wengi hadi kufikia maamuzi ya mwisho kuhusu malengo ya kuchumi, kijamii na kiutamaduni.
Demokrasia hutenga wanasiasa a mangimeza
Vilevile, demokrasia hustawi pale ambapo miingiliano ya vionogzi wa serikali na watumishi wa serikali haiwayumbishi kundi la pili kichama au kisiasa na wanakuwa huru kufanya maamuzi yao kwa mujibu wa taaluma zao. Watumishi hawa ni pamoja na wale wa Hazina na Benki Kuu ya nchi.
Miingiliano hii hufanyika katika ngazi mbalimbali kipekee wakati huohuo.
Miingiliano hii hutawaliwa na mazungumzo au mijadala isiyokwisha juu ya fani au nyanja mbalimbali za maisha.
Suala lingine muhimu katika mada hii ni ulazima wa kuwa na sheria na taratibu wazi za uwajibikaji katika michakato ya vyama kujipatia fedha za kuendesha kazi zao za kawaida na zile za kuendesha kampeni za uchaguzi kwa nyakati mbalimbali.
Kama suala hili linakuwa gizani kwa maana kwamba hatujui jinsi vyama vinavyopata fedha zao, kiasi wanachopata na watu au taasisi zinazovipa vyama fedha basi ni rahisi nchi hii kuuzwa bila wananchi wake kujua.
Demokrasia badala ya kuchangia kukua kiuchumi kwa nchi itakuwa inachangia kuingiza nchi katika madeni ya kiajabu ajabu ambayo sio tu yatazuia nchi kupata maendeleo ya kiuchumi na kijamii lakini vile yatakuwa ndio chanzo cha kuua amani, utulivu na mshikamano katika nchi.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
Thursday, June 11, 2009
DEMOKRASIA, WANANCHI NA VYOMBO VYA HABARI
Maana ya Vyombo Huru vya Habari
Vyombo huru vya habari ni vyombo vyote vya mawasiliano ya umma na vinginevyo visivyofanya kazi kwa matashi ya mtu au kikundi fulani cha watu na vyenye kujali ukweli na uwazi katika kupasha habari na kuelimisha watu na vilevile kutoa fursa kwa watu hao kutathmini na kuona uhakika na umakini wa habari husika na kisha kufikia maamuzi kutokana na jinsi wao wenyewe walivyoamini ukweli na uwazi ni upi.
Vinatambua kwa yakini kuwa hatari kubwa zaidi ipo katika kuficha ukweli na kuwaachia baadhi ya watu kugeuza urongo kuwa ukweli.
Wanatambua kwa yakini linalohusu wananchi wote wa nchi hii ni kubwa kuliko chama au mtu yeyote. Na wanaamini wajibu wao kwanza ni kwa wananchi na sio chama au mtu fulani.
Hawakubali kurubuniwa na mtu au chama fulani, na siku zote wafanyakazi wake hujitahidi kuwa na elimu na maarifa zaidi kuliko wanasiasa au wanajamii wengine
Vyombo hivyo vinaweza kuwa redio, televisheni, magazeti au tovuti na swahiba zao. Vinaweza kumilikiwa na chama au serikali au watu binafsi. Uhuru hautokani na umilikaji wa chombo bali uhuru watendaji na waandishi wa habari walionao katika kufanya kazi zao kama taaluma zao zinavyotaka bila ya kuyumbishwa na mmilikaji.
Kwa sababu hii chombo cha habari
kinachomilikiwa na serikali au chama tawala hakiwezi kuaminiwa na kuthaminiwa kama hakiripoti ukweli na badala yake kinawasaidia walioko madarakani kuficha ukweli au kudai kuwa urongo ndio ukweli.
Kwa mantiki hii kuna vyombo vya serikali na chama vinavyoweza kuwa huru na vinavoripoti ukweli. Na wakati huo huo kunaweza kuwa na vyombo binafsi ambavyo sio huru na vinavyoficha ukweli au kuwakanganya wasomaji au wasikilizaji au watazamaji wake. Ingawa kwa kawaida hapa Afrika vyombo vingi vinavyomilikiwa na serikali (kwa kisingizio kuwa ni vya umma) au vyama vya kisiasa ni vyombo ambavyo ni vigumu kuwa huru.
Vyombo vya Habari ni uti wa mgongo wa demokrasia. Ndivyo vinavyotoa habari za kisiasa zinazowashawishi watu kuwa wapiga kura walioiva kimaamuzi. Hutufahamisha juu ya matatizo yaliyoko sehemu fulani na kupendekeza jinsi ya kuyashughulikia. Aidha ni walinzi dhidi ya maovu na mabaya yanayoweza kufanywa na wale wenye uwezo au vyeo. Hali kadhalika, vyombo vya habari vinaruhusu au kuwanyima wananchi kuendesha kwa uhuru kamili mijadala mbalimbali na kutoa fursa kwa wote kujifunza juu ya kile kinachohitajika kufanywa au kuzuiliwa kisiendelee au kisitokee. Katika enzi hizi ambazo baadhi ya vyombo vya habari vina nguvu kubwa upo pia uwezekano wa vyombo fulani kuweka ajenda wanayotaka wananchi na serikali kuizungumzia.
Ujio wa Tovuti na Blogi na sera zilizopitwa na wakati
Ujio wa Tovuti na hususan Blogi, vidaka picha kwenye kamera na ujumbe wa matini au maneno mafupi vimetoa chagamoto ya kuwepo kwa waandishi wananchi na vyombo vya habari vya wananchi ambavyo vina uwezo na uhuru mkubwa zaidi wa kuzungumzia hata yale ambayo wanasiasa na serikali wasingelipenda kuyasikia au kuona yanajulikana na watu wengine.
Kwa maneno mengine, kuwepo kwa simu za mkononi sasa hivi kunamuwezesha mwananchi kuwa na chombo binafsi cha habari na pengine anachokiamini zaidi kuliko chombo kingine chochote. Katika hali kama hii itakuwa ni kazi kweli kuwadanganya wananchi wote kwa wakati wote, ingawa, baadhi ya vyombo vitaweza kuwadanganya watu fulani kwa muda fulani. Kwa maneno mengine, kazi ya kusambaza uongo kwa vyombo vya habari na hasa vile vya chama na serikali iliyoko madarakani sasa inafikia ukomo wake.
Ni haki yetu sote kama wananchi kwa hiyo kudai kuwa lazima vyombo vya habari viwe na hulka, maadili na viwango fulani vya kufikiwa wakati wote wa utendaji kazi yao kwa kuzingatia majukumu yalyoorodheshwa hapo juu. Katika demokrasia haya ni matarajio ya msingi na halali kabisa toka kwa wananchi.
Gurevitch and Blumler (1990) wameainisha vizuri ni nini majukumu ya vyombo vya habari katika nchi ya kidemokrasia. Majukumu hayo ni pamoja na: kuangalia na kuzungumzia maendeleo ya kisiasa na kijamii; kuonesha mada moto za wakati uliopo; kuasisi majukwaa ya kuzungumzia masuala mbalimbali kutoka mitazamo na misimamo tofuati; kuwawajibisha viongozi kutokana na jinsi wanavyotumia uwezo, mali na vyeo walivyo navyo; kutoa hamasa, msisitizo, vishawishi kwa wananchi kusoma, kujifunza na kuelewa masuala mbalimbali; kuchagua; na kushiriki katika mchakato mzima wa siasa nchini; kuhimiza na kuchochea ushindani katika kila nyanja ya maisha na kuzuia kwa ukucha na jino hatua zozote zinazodhamiria kuvinyang'anya vyombo vya habari haki ya kuwa huru.
Uhuru wa Vyombo vya Habari na Demokrasia
Demokrasia katika nchi yoyote ile inakuwa pana na ya kina au finyu na ya juu kulingana na upana au kina cha uhuru wa vyombo vya habari katika nchi husika.
Kwa kujua au kutokujua viongozi wanaweza kubomoa au kujenga demokrasia kwa kutumia vizuri au vibaya vyombo vya habari. Pale vyombo vya habari vinapotumika kuwapa sauti wananchi wazungumze wao badala tu ya wao kuwasikiliza kinachosemwa na viongozi wa serikali au wa kisiasa demokrasia hujengwa. Pale vinapotumika kuwa 'laudispika' za viongozi demokrasia husinyaa na kupwaya.
Pale vyombo vya habari vinapokuwa mstari wa mbele kuwafungua watu macho na masikio juu ya udhaifu na makosa mbalimbali ya kiutawala na kiutendaji demokrasia hukua na kupanuka. Vinginevyo, huzuka jamii ya mbumbumbu wasiofikiri wala kufanya mchakato wa hoja na mawazo mbalimbali kabla ya kufanya maamuzi muhimu.
Nchi yetu haina miaka mingi toka kuanza kukubali vyombo huru vya habari. Hata hivyo dalili zilizopo hivi sasa zinaonesha tuna nafasi nzuri ya kuwa na vyombo vya habari vinavyochangia kukua na kupanuka kwa demokrasia kuliko vile vinavyohujumu demokrasia.
Hata hivyo, vyombo vya habari vinavyomilikiwa na serikali na vyama vya kisiasa au viongozi na wafanyabiashara binafsi havioneshi kuikubali ajenda ya demokrasia. Vingi kati yao vinaelekea kuwa na ajenda za kuhuisha maiti; kuita kilichooza kizima na kuita harufu mbaya harufu ya karafuu na marashi.
Hapa nchini na hata huko nje, inaelezwa kwamba, vyombo vya habari havitekelezi wajibu na majukumu yake kikamilifu. Aidha, baadhi ya vyombo vya habari ama vinatumiwa na wanasiasa au wale wenye kuvimiliki kwa malengo yao binafsi na sio kwa maslahi ya umma.
Katika hali ambayo waandishi wa habari wa vyombo vya umma na vile vya binafsi wanahofia ajira yao kama watakwenda kinyume na matakwa ya wenye vyombo hivyo kwa uhalali au kiutapeli, wao hujikuta ni mateka katika harakati binafsi au za kichama za waajiri wao.
Wachambuzi wa masuala ya vyombo vya habari wanasema kwamba vyombo vya habari ambavyo aidha vinasimamiwa na serikali au kuendeshwa kibiashara na matajiri wachache wa ndani na nje vimekuwa wakati mwingine vyombo vinavyopiga vita demokrasia kwa kujua au kutokujua.
Maudhui katika vyombo vilivyo vingi sio ya kuhabarisha na kuelimisha bali kustarehesha na kupumbaza. Umbeya, kashfa, uzushi, ngono na magomvi ndivyo vinavyopewa kipaumbele zaidi kuliko kitu kingine.
Habari nyingi za kisiasa ni za kushabikia mambo yazuykayo na yapitayo baada ya muda au za kuwahusu watu fulani kiwasifu au kutosheleza kiu yao ya kuonekana au kusikika katika jamii na sio habari zenye fikra mpya, mawazo mbadala, au utundu na ubunifu wa watu hao katika kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya wananchi au kuwaelekeza na kuwaongoza watu katika kutumia fursa za kiuchumi, kisiasa au kijamii zilizopo.
Nchi hazina mijadala muhimu ya kimaendeleo
Kutokana na kutokuwepo na mijadala na midahalo ya maana katika jamii panazuka matangazo ya propaganda yenye kauli mbiu na misemo isiyo na uzito wala maana yoyote katika maisha ya mwananchi. Matokeo yake wapiga kura wanachoshwa na kukatishwa tamaa na hali hii na kuwafanya waone siasa na wanasiasa kama vitu visivyo na maana katika maisha yao. Wengi huacha kabisa kupiga kura wakiwa na hakika kwamba wanajua tayari matokeo yatakuwaje.
Hali iliyofikisha Ulaya hivi leo kushuhudia chini ya asilimia 40 ya wanaostahili kupiga kura ndio tu wakijiandikisha kupiga kura na chini ya hapo kushiriki chaguzi mbalimbali ni somo zuri kwa wanasiasa wetu na waandishi wa habari kuhusu wapi wanaweza kuzifikisha nchi zao kama wakiendelea kama wanavyofanya sasa.
Vyombo vya habari huchangamkia kashfa katika maisha binafsi ya watu na kusahau kabisa kutathmini na kuhakiki sera na mapendekezo ya wanasiasa husika na yale yanayoweza kwa yakini kuleta mabadiliko katika maisha ya kiuchumi na kijamii ya wananchi.
Vyombo vya habari hukurupuka na kufanya ajali au athari ndogondogo kuwa mambo makubwa ya kututisha wakati yale yanayoweza kuwa baa au maafa makubwa yanasahaulika.
Ili kukidhi njaa yao ya fedha za kujiendesha vyombo vingi vya habari vimeamua kufumbia macho hatari za viwanda na bidhaa mbalimbali nchini japo vina hatari kubwa kwa maisha ya wanadamu. Hili ni kwa sababu tu kuwepo kwa vyombo hivyo kwa sasa kunategemea zaidi mapato kutokana na matangazo ya biashara kuliko vyanzo vingine au mauzo mengineyo.
Hata hivyo tunapozungumzia hapa demokrasia na vyombo vya habari hatuwezi kuzungumzia kila kitu.
Tutajikita zaidi katika kuona ni jinsi gani vyombo hivyo vinaweza kukuza na kupanua demokrasia au kuviza na kuifanya demokrasia kusinyaa.
Tathmini fupi ya vyombo mbalimbali
Tathmini ya haraka haraka inaonesha magazeti binafsi kwa hivi sasa yanafanya kazi nzuri zaidi katika kuelimisha watu na kukuza na kuendeleza demokrasia. Hata hivyo, redio na televisheni nyingi bado ziko nyuma katika kazi ya kuchangia kukua na kuendelea kwa demokrasia nchini. Redio na Televisheni zilizopo zinaonekana ama kuwa ubao wa matangazo wa watawala au vyombo vya kuwapumbaza wananchi wasipate muda wa kutafakari, kuchambua na kutoa changamoto za maendeleo yao ya kijamii na kiuchumi.
Awali watu waliamini kuwa kuwepo kwa redio na televisheni nyingi nchini kungeongeza ubora wa vipindi na maudhui ya vipindi. Kinachotokea ni kuwa sasa redio na televisheni nyingi ambazo hazijafikisha hata miaka kumi zimechoka na vipindi vyao ni rojo kuliko pale nchi ilipokuwa na televisheni na redio moja tu.
Katika miaka hii ya mtikisiko wa kiuchumi bila shaka hali itaendelea kuwa mbaya zaidi. Lawama ni kwa wamilikaji wote ambao wameamua aghalabu kuwekeza zaidi kwenye vitu badala ya kuwekeza kwenye watu.
Udhaifu uliopo
Vyombo vya habari vinakabiliwa na matatizo mengi ikiwemo gharama za uendeshaji na uzalishaji, barabara mbovu, mawasiliano mabovu na ghali, umeme usioaminika, rasilimali watu duni, kodi kubwa, shikinizo za kisiasa na kadhalika.
Haya yote yanachangia katika udhaifu wa vyombo vya habari kuvifikia nchi nzima na kutumuka kikamilifu kama vyombo vya kuchochea mapinduzi ya kidemokrasia hadi vijijini.
Hili linachangia pia kwa vyombo vya habari vilivyopo kutokuwa na uhuru wa kimtaji na kifedha na hivyo kuishia kutumiwa na wachache kwenye jamii wenye ubavu wa kifedha au kisiasa. Katika hali kama hii itakuwa muhali kwa vyombo vya habari kuwa mtetezi wa umma na mpiganiaji uhuru, haki na demokrasia wa kweli kwa niaba ya wananchi.
Changamoto zilizopo
Kutokana na matatizo hayo hapo juu upo umuhimu wa kutoa changamoto la kuhamasisha magazeti ya jamii yakiwemo yale ya vijiji, miji, wilaya, mkoa na kando ili kukabili vizuizi vilivyopo hivi sasa katika vyombo vya habari na hasa magazeti kuwafikia watu kwa wakati na vile vile kuwa na habari zinazowahusu zaidi kuliko habari za maeneo na watu wengine.
Hali kadhalika, ni muhimu kwa wapenda demokrasia ndani na nje ya nchi kuvipa jamala vyombo vya habari ili viondokane na uhitaji na uwezekano wa kutumiwa kutokana na ukata wao.
Mengine ni kuangalia uwezekano wa tovuti kufika vijijini katika lugha ya kiswahili; kutangaza na kuonesha umuhimu wa elimu ya uraia na haki za kikatiba za mwananchi; kutangazia watu kuwa mfumo wa vyama vingi ni bora kuliko mfumo wa chama kimoja au demokrasia ni bora kuliko udikteta.
Hili linaenda pamoja na kuitumia teknolojia ya kisasa kufanya simu za mkononi ziendelee kuwa vyanzo nafuu vya habari za uhakika na kuaminika.
Tunayazungumzia yote haya tukitambua kuwa mawasiliano ni nishati pekee inayotoa nguvu na uwezo kwa jamii yoyote au nchi yoyote kubuni, kufikiria, kutafakari, kuamua na kutekeleza na kisha kutathmini na kuendeleza mambo mbalimbali yanayoifanya jamii au nchi kuwa siku zote katika mwendo wa kimaendeleo badala ya kukwama katika dimbwi la matatizo na kuchanganyikiwa kiuchumi na kijamii.
Hii ina maana demokrasia sio tu inachangia siasa na utawala bora bali pia nchi kuwa mstari wa mbele pia katika uchumi, sayansi, teknolojia, utamaduni, michezo na aina nyingine za maendeleo ya mwanadamu.
Kwa hiyo vyombo vya habari vikichangia maendeleo ya haki za binadamu, uhuru na demokrasia kwa watu wa sehemu fulani vinakuwa pia vinachangia maendeleo makubwa ya nchi na ulimwengu kwa ujumla.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
Vyombo huru vya habari ni vyombo vyote vya mawasiliano ya umma na vinginevyo visivyofanya kazi kwa matashi ya mtu au kikundi fulani cha watu na vyenye kujali ukweli na uwazi katika kupasha habari na kuelimisha watu na vilevile kutoa fursa kwa watu hao kutathmini na kuona uhakika na umakini wa habari husika na kisha kufikia maamuzi kutokana na jinsi wao wenyewe walivyoamini ukweli na uwazi ni upi.
Vinatambua kwa yakini kuwa hatari kubwa zaidi ipo katika kuficha ukweli na kuwaachia baadhi ya watu kugeuza urongo kuwa ukweli.
Wanatambua kwa yakini linalohusu wananchi wote wa nchi hii ni kubwa kuliko chama au mtu yeyote. Na wanaamini wajibu wao kwanza ni kwa wananchi na sio chama au mtu fulani.
Hawakubali kurubuniwa na mtu au chama fulani, na siku zote wafanyakazi wake hujitahidi kuwa na elimu na maarifa zaidi kuliko wanasiasa au wanajamii wengine
Vyombo hivyo vinaweza kuwa redio, televisheni, magazeti au tovuti na swahiba zao. Vinaweza kumilikiwa na chama au serikali au watu binafsi. Uhuru hautokani na umilikaji wa chombo bali uhuru watendaji na waandishi wa habari walionao katika kufanya kazi zao kama taaluma zao zinavyotaka bila ya kuyumbishwa na mmilikaji.
Kwa sababu hii chombo cha habari
kinachomilikiwa na serikali au chama tawala hakiwezi kuaminiwa na kuthaminiwa kama hakiripoti ukweli na badala yake kinawasaidia walioko madarakani kuficha ukweli au kudai kuwa urongo ndio ukweli.
Kwa mantiki hii kuna vyombo vya serikali na chama vinavyoweza kuwa huru na vinavoripoti ukweli. Na wakati huo huo kunaweza kuwa na vyombo binafsi ambavyo sio huru na vinavyoficha ukweli au kuwakanganya wasomaji au wasikilizaji au watazamaji wake. Ingawa kwa kawaida hapa Afrika vyombo vingi vinavyomilikiwa na serikali (kwa kisingizio kuwa ni vya umma) au vyama vya kisiasa ni vyombo ambavyo ni vigumu kuwa huru.
Vyombo vya Habari ni uti wa mgongo wa demokrasia. Ndivyo vinavyotoa habari za kisiasa zinazowashawishi watu kuwa wapiga kura walioiva kimaamuzi. Hutufahamisha juu ya matatizo yaliyoko sehemu fulani na kupendekeza jinsi ya kuyashughulikia. Aidha ni walinzi dhidi ya maovu na mabaya yanayoweza kufanywa na wale wenye uwezo au vyeo. Hali kadhalika, vyombo vya habari vinaruhusu au kuwanyima wananchi kuendesha kwa uhuru kamili mijadala mbalimbali na kutoa fursa kwa wote kujifunza juu ya kile kinachohitajika kufanywa au kuzuiliwa kisiendelee au kisitokee. Katika enzi hizi ambazo baadhi ya vyombo vya habari vina nguvu kubwa upo pia uwezekano wa vyombo fulani kuweka ajenda wanayotaka wananchi na serikali kuizungumzia.
Ujio wa Tovuti na Blogi na sera zilizopitwa na wakati
Ujio wa Tovuti na hususan Blogi, vidaka picha kwenye kamera na ujumbe wa matini au maneno mafupi vimetoa chagamoto ya kuwepo kwa waandishi wananchi na vyombo vya habari vya wananchi ambavyo vina uwezo na uhuru mkubwa zaidi wa kuzungumzia hata yale ambayo wanasiasa na serikali wasingelipenda kuyasikia au kuona yanajulikana na watu wengine.
Kwa maneno mengine, kuwepo kwa simu za mkononi sasa hivi kunamuwezesha mwananchi kuwa na chombo binafsi cha habari na pengine anachokiamini zaidi kuliko chombo kingine chochote. Katika hali kama hii itakuwa ni kazi kweli kuwadanganya wananchi wote kwa wakati wote, ingawa, baadhi ya vyombo vitaweza kuwadanganya watu fulani kwa muda fulani. Kwa maneno mengine, kazi ya kusambaza uongo kwa vyombo vya habari na hasa vile vya chama na serikali iliyoko madarakani sasa inafikia ukomo wake.
Ni haki yetu sote kama wananchi kwa hiyo kudai kuwa lazima vyombo vya habari viwe na hulka, maadili na viwango fulani vya kufikiwa wakati wote wa utendaji kazi yao kwa kuzingatia majukumu yalyoorodheshwa hapo juu. Katika demokrasia haya ni matarajio ya msingi na halali kabisa toka kwa wananchi.
Gurevitch and Blumler (1990) wameainisha vizuri ni nini majukumu ya vyombo vya habari katika nchi ya kidemokrasia. Majukumu hayo ni pamoja na: kuangalia na kuzungumzia maendeleo ya kisiasa na kijamii; kuonesha mada moto za wakati uliopo; kuasisi majukwaa ya kuzungumzia masuala mbalimbali kutoka mitazamo na misimamo tofuati; kuwawajibisha viongozi kutokana na jinsi wanavyotumia uwezo, mali na vyeo walivyo navyo; kutoa hamasa, msisitizo, vishawishi kwa wananchi kusoma, kujifunza na kuelewa masuala mbalimbali; kuchagua; na kushiriki katika mchakato mzima wa siasa nchini; kuhimiza na kuchochea ushindani katika kila nyanja ya maisha na kuzuia kwa ukucha na jino hatua zozote zinazodhamiria kuvinyang'anya vyombo vya habari haki ya kuwa huru.
Uhuru wa Vyombo vya Habari na Demokrasia
Demokrasia katika nchi yoyote ile inakuwa pana na ya kina au finyu na ya juu kulingana na upana au kina cha uhuru wa vyombo vya habari katika nchi husika.
Kwa kujua au kutokujua viongozi wanaweza kubomoa au kujenga demokrasia kwa kutumia vizuri au vibaya vyombo vya habari. Pale vyombo vya habari vinapotumika kuwapa sauti wananchi wazungumze wao badala tu ya wao kuwasikiliza kinachosemwa na viongozi wa serikali au wa kisiasa demokrasia hujengwa. Pale vinapotumika kuwa 'laudispika' za viongozi demokrasia husinyaa na kupwaya.
Pale vyombo vya habari vinapokuwa mstari wa mbele kuwafungua watu macho na masikio juu ya udhaifu na makosa mbalimbali ya kiutawala na kiutendaji demokrasia hukua na kupanuka. Vinginevyo, huzuka jamii ya mbumbumbu wasiofikiri wala kufanya mchakato wa hoja na mawazo mbalimbali kabla ya kufanya maamuzi muhimu.
Nchi yetu haina miaka mingi toka kuanza kukubali vyombo huru vya habari. Hata hivyo dalili zilizopo hivi sasa zinaonesha tuna nafasi nzuri ya kuwa na vyombo vya habari vinavyochangia kukua na kupanuka kwa demokrasia kuliko vile vinavyohujumu demokrasia.
Hata hivyo, vyombo vya habari vinavyomilikiwa na serikali na vyama vya kisiasa au viongozi na wafanyabiashara binafsi havioneshi kuikubali ajenda ya demokrasia. Vingi kati yao vinaelekea kuwa na ajenda za kuhuisha maiti; kuita kilichooza kizima na kuita harufu mbaya harufu ya karafuu na marashi.
Hapa nchini na hata huko nje, inaelezwa kwamba, vyombo vya habari havitekelezi wajibu na majukumu yake kikamilifu. Aidha, baadhi ya vyombo vya habari ama vinatumiwa na wanasiasa au wale wenye kuvimiliki kwa malengo yao binafsi na sio kwa maslahi ya umma.
Katika hali ambayo waandishi wa habari wa vyombo vya umma na vile vya binafsi wanahofia ajira yao kama watakwenda kinyume na matakwa ya wenye vyombo hivyo kwa uhalali au kiutapeli, wao hujikuta ni mateka katika harakati binafsi au za kichama za waajiri wao.
Wachambuzi wa masuala ya vyombo vya habari wanasema kwamba vyombo vya habari ambavyo aidha vinasimamiwa na serikali au kuendeshwa kibiashara na matajiri wachache wa ndani na nje vimekuwa wakati mwingine vyombo vinavyopiga vita demokrasia kwa kujua au kutokujua.
Maudhui katika vyombo vilivyo vingi sio ya kuhabarisha na kuelimisha bali kustarehesha na kupumbaza. Umbeya, kashfa, uzushi, ngono na magomvi ndivyo vinavyopewa kipaumbele zaidi kuliko kitu kingine.
Habari nyingi za kisiasa ni za kushabikia mambo yazuykayo na yapitayo baada ya muda au za kuwahusu watu fulani kiwasifu au kutosheleza kiu yao ya kuonekana au kusikika katika jamii na sio habari zenye fikra mpya, mawazo mbadala, au utundu na ubunifu wa watu hao katika kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya wananchi au kuwaelekeza na kuwaongoza watu katika kutumia fursa za kiuchumi, kisiasa au kijamii zilizopo.
Nchi hazina mijadala muhimu ya kimaendeleo
Kutokana na kutokuwepo na mijadala na midahalo ya maana katika jamii panazuka matangazo ya propaganda yenye kauli mbiu na misemo isiyo na uzito wala maana yoyote katika maisha ya mwananchi. Matokeo yake wapiga kura wanachoshwa na kukatishwa tamaa na hali hii na kuwafanya waone siasa na wanasiasa kama vitu visivyo na maana katika maisha yao. Wengi huacha kabisa kupiga kura wakiwa na hakika kwamba wanajua tayari matokeo yatakuwaje.
Hali iliyofikisha Ulaya hivi leo kushuhudia chini ya asilimia 40 ya wanaostahili kupiga kura ndio tu wakijiandikisha kupiga kura na chini ya hapo kushiriki chaguzi mbalimbali ni somo zuri kwa wanasiasa wetu na waandishi wa habari kuhusu wapi wanaweza kuzifikisha nchi zao kama wakiendelea kama wanavyofanya sasa.
Vyombo vya habari huchangamkia kashfa katika maisha binafsi ya watu na kusahau kabisa kutathmini na kuhakiki sera na mapendekezo ya wanasiasa husika na yale yanayoweza kwa yakini kuleta mabadiliko katika maisha ya kiuchumi na kijamii ya wananchi.
Vyombo vya habari hukurupuka na kufanya ajali au athari ndogondogo kuwa mambo makubwa ya kututisha wakati yale yanayoweza kuwa baa au maafa makubwa yanasahaulika.
Ili kukidhi njaa yao ya fedha za kujiendesha vyombo vingi vya habari vimeamua kufumbia macho hatari za viwanda na bidhaa mbalimbali nchini japo vina hatari kubwa kwa maisha ya wanadamu. Hili ni kwa sababu tu kuwepo kwa vyombo hivyo kwa sasa kunategemea zaidi mapato kutokana na matangazo ya biashara kuliko vyanzo vingine au mauzo mengineyo.
Hata hivyo tunapozungumzia hapa demokrasia na vyombo vya habari hatuwezi kuzungumzia kila kitu.
Tutajikita zaidi katika kuona ni jinsi gani vyombo hivyo vinaweza kukuza na kupanua demokrasia au kuviza na kuifanya demokrasia kusinyaa.
Tathmini fupi ya vyombo mbalimbali
Tathmini ya haraka haraka inaonesha magazeti binafsi kwa hivi sasa yanafanya kazi nzuri zaidi katika kuelimisha watu na kukuza na kuendeleza demokrasia. Hata hivyo, redio na televisheni nyingi bado ziko nyuma katika kazi ya kuchangia kukua na kuendelea kwa demokrasia nchini. Redio na Televisheni zilizopo zinaonekana ama kuwa ubao wa matangazo wa watawala au vyombo vya kuwapumbaza wananchi wasipate muda wa kutafakari, kuchambua na kutoa changamoto za maendeleo yao ya kijamii na kiuchumi.
Awali watu waliamini kuwa kuwepo kwa redio na televisheni nyingi nchini kungeongeza ubora wa vipindi na maudhui ya vipindi. Kinachotokea ni kuwa sasa redio na televisheni nyingi ambazo hazijafikisha hata miaka kumi zimechoka na vipindi vyao ni rojo kuliko pale nchi ilipokuwa na televisheni na redio moja tu.
Katika miaka hii ya mtikisiko wa kiuchumi bila shaka hali itaendelea kuwa mbaya zaidi. Lawama ni kwa wamilikaji wote ambao wameamua aghalabu kuwekeza zaidi kwenye vitu badala ya kuwekeza kwenye watu.
Udhaifu uliopo
Vyombo vya habari vinakabiliwa na matatizo mengi ikiwemo gharama za uendeshaji na uzalishaji, barabara mbovu, mawasiliano mabovu na ghali, umeme usioaminika, rasilimali watu duni, kodi kubwa, shikinizo za kisiasa na kadhalika.
Haya yote yanachangia katika udhaifu wa vyombo vya habari kuvifikia nchi nzima na kutumuka kikamilifu kama vyombo vya kuchochea mapinduzi ya kidemokrasia hadi vijijini.
Hili linachangia pia kwa vyombo vya habari vilivyopo kutokuwa na uhuru wa kimtaji na kifedha na hivyo kuishia kutumiwa na wachache kwenye jamii wenye ubavu wa kifedha au kisiasa. Katika hali kama hii itakuwa muhali kwa vyombo vya habari kuwa mtetezi wa umma na mpiganiaji uhuru, haki na demokrasia wa kweli kwa niaba ya wananchi.
Changamoto zilizopo
Kutokana na matatizo hayo hapo juu upo umuhimu wa kutoa changamoto la kuhamasisha magazeti ya jamii yakiwemo yale ya vijiji, miji, wilaya, mkoa na kando ili kukabili vizuizi vilivyopo hivi sasa katika vyombo vya habari na hasa magazeti kuwafikia watu kwa wakati na vile vile kuwa na habari zinazowahusu zaidi kuliko habari za maeneo na watu wengine.
Hali kadhalika, ni muhimu kwa wapenda demokrasia ndani na nje ya nchi kuvipa jamala vyombo vya habari ili viondokane na uhitaji na uwezekano wa kutumiwa kutokana na ukata wao.
Mengine ni kuangalia uwezekano wa tovuti kufika vijijini katika lugha ya kiswahili; kutangaza na kuonesha umuhimu wa elimu ya uraia na haki za kikatiba za mwananchi; kutangazia watu kuwa mfumo wa vyama vingi ni bora kuliko mfumo wa chama kimoja au demokrasia ni bora kuliko udikteta.
Hili linaenda pamoja na kuitumia teknolojia ya kisasa kufanya simu za mkononi ziendelee kuwa vyanzo nafuu vya habari za uhakika na kuaminika.
Tunayazungumzia yote haya tukitambua kuwa mawasiliano ni nishati pekee inayotoa nguvu na uwezo kwa jamii yoyote au nchi yoyote kubuni, kufikiria, kutafakari, kuamua na kutekeleza na kisha kutathmini na kuendeleza mambo mbalimbali yanayoifanya jamii au nchi kuwa siku zote katika mwendo wa kimaendeleo badala ya kukwama katika dimbwi la matatizo na kuchanganyikiwa kiuchumi na kijamii.
Hii ina maana demokrasia sio tu inachangia siasa na utawala bora bali pia nchi kuwa mstari wa mbele pia katika uchumi, sayansi, teknolojia, utamaduni, michezo na aina nyingine za maendeleo ya mwanadamu.
Kwa hiyo vyombo vya habari vikichangia maendeleo ya haki za binadamu, uhuru na demokrasia kwa watu wa sehemu fulani vinakuwa pia vinachangia maendeleo makubwa ya nchi na ulimwengu kwa ujumla.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
Wednesday, June 10, 2009
DEMOKRASIA NA WAGOMBEA HURU
Mgombea huru ni mtu gani ?
Mgombea huru ni raia yeyote katika nchi fulani anayegombea nafasi yoyote ile ya uongozi bila kuwa mwanachama wa chama fulani.
Katiba kwa kawaida huainisha wajibu na haki za watu kwa misingi ya matamko mbalimbali ya Haki za binadamu na nyinginezo na kisha hutoa haki kwa kila mtu katika misingi ya usawa, ikiwemo ile haki ya kupigiwa na kupiga kura. Baadhi ya nchi hapa Afrika , hata hivyo, zimeamua kuwadhulumu wananchi wao kwa kuwanyima watu wao haki ya kupigiwa kura kwa visingizio vya aina mbalimbali . Ni haki ya wananchi kudai na kuona kwamba wanakuwa na uhuru wa kupigiwa na kupiga kura. Na sio waruhusiwe tu na pengine kulazimishwa kupiga kura lakini wasiwe na haki ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi toka chin hadi juu katika nchi yao.
Uamuzi wa mtu kuwa mgombea huru husababishwa na mambo mbalimbali. Hufanya hivyo, aghalabu, kwa sababu anaamini kwamba viongozi wa vyama walipo ni bomu na hawawezi kufikisha jimbo au mkoa au nchi pale sehemu husika inapostahili. Wakati mwingine hukataa kuwa mwanachama wa chama fulani kwa sababu ya kiwango cha wizi na ufisadi anauona ndani ya chama husika. Aidha, huweza kukataa pia kuwa mgombea wa chama fulani kwa sababu anaamini kwamba vyama vilivyopo havitetei maslahi ya mwananchi bali maslahi binafsi ya viongozi wa vyama hivyo.
Vilevile, huweza kuamua hivyo kutokana na kutambua fika viongozi waliopo wamebeba na hawana uwezo wa kiakili, kifikira na kivitendo wa kuongoza watu na nchi.
Dhuluma kubwa inayofanywa na katiba iliyopo ni ile ya kumpa mtu haki ya kupiga kura [bila kujali ni mwanachama au sio mwanachama wa chama fulani] lakini wakati huo ikamnyima haki ya kupigiwa ila tu mtu anapokuwa ni mwanachama wa chama cha kisiasa kilichosajiliwa.
Ni dhambi isiyo na msamaha kwa mwananchi yoyote kushiriki katika vitendo vya uhuni, ubabe, unyang'anyi wa haki na uhuru wa mtu kupitia katika kuichezea na kuivuruga katiba kwa maslahi ya wachache au chama fulani cha kisiasa. Ndivyo ilivyo pia katika kupora haki ya mgombea huru.
Hadi wa leo hapajaruhusiwa kuwa na mgombea huru, mathalani, nchini Tanzania. Hata hivyo, mtu akiangalia kwa makini atagundua kuwa amri ya kukataa wagombea huru haiungwi mkono na vifungu mbalimbali vya katiba.
Katika sura hii tutajaribu kulionesha hilo huku tukitaraji kuwa wanasheria na wapigania haki na uhuru wa binadamu kwa kushirikiana na Tume ya Uchaguzi wataliangalia jambo hili kwa macho mapya na kuondoa dhuluma wanayofanyiwa wale wanaotaka kufikia hatua ya juu katika msonge wa mahitaji ya binadamu kama ilivyoainishwa na Abraham Maslow.
Mitihani kwa wasiokubali vyama vilivyopo
Hali ilivyo hivi sasa ni kwamba mwananchi au mwanasiasa anayetaka kuwa mgombea huru anaiweka nchi au yeye mwenyewe anajikuta katika mitihani ifuatayo:
a) Kama ni mwanachama wa chama fulani anajikuta kifungoni pale anapokuwa kakiona chama ni kichafu na kibovu kiasi cha kutisha;
b) Anajikuta ni mnafiki kwa nafsi yake na anaowawakilisha;
c) Analazimishwa kutekeleza sera na mambo asiyokubaliana nao;
d) Ananyimwa nafasi ya kuchangia ubunifu, mawazo mapya na kutumika kwa fursa za maendeleo au kutatua matatizo ya wananchi kwa njia bora na yenye manufaa kwa wananchi zaidi kuliko inavyofanywa na chama au vyama;
e) Anajikuta hawezi kutumia haki zake nyingi alizopewa kikatiba kama raia;
f) Anajikuta kwamba ingawa yeye ni bora kuliko wengi wengine ananyimwa nafasi ya kuongoza nchi;
g) Inafikia hatua nchi inaongozwa na viongozi dhaifu, wezi na wabovu kutokana na vyama kuwazuia au kuwapiga vita watu walio bora kuliko wao;
h) Kwa kuwa viongozi hao (wanaowazuia wagombea huru) wanajua hakuna wanachokifanya na hawajiamini wanaanza kujiingiza kwenye vitendo vya kuimaliza nchi kiuchumi na kijamii kama bima yao ya baadaye endapo wataondolewa madarakani kwa njia yoyote ile. Njia hizo za kuifukarisha zaidi nchi ni pamoja na kushirikiana na watu wengine kuibia benki kuu na serikali au kuingia mikataba ya kiwizi wizi au kutumia fedha zilizopangwa kwa maendeleo ya wengi kwa maslahi binafsi kwa wachache au ya chama chao.
Kulazimisha uanachama ni kuvunja katiba
Kuwalazimisha watu kuwa wanachama wa chama cha kisiasa ni kosa. Kumnyima mtu haki ya kupigiwa kura eti kwa sababu sio mwanachama wa chama cha kisiasa nalo ni kosa. Na haya yote yanaweza kushuhudiwa na vifungu mbalimbali vya Katiba ya Jamhuri ya Muungano [1998] hususan Sura ya Kwanza, Sehemu ya Kwanza hadi ya tatu, kama tutakavyoonesha hapa chini.
Kifungu namba 5.-(1) cha katiba ya JMT kiasema "Kila raia wa Tanzania aliyetimiza umri wa miaka
kumi na minane anayo haki ya kupiga kura katika uchaguzi
unaofaywa Tanzania na wananchi. Na haki hii itatumiwa kwa
kufuata masharti ya ibara ndogo ya (2) pamoja na masharti
mengineyo ya Katiba hii na ya Sheria inayotumika nchini
Tanzania kuhusu mambo ya uchaguzi."
Masharti yaliyomo katika ibara hiyo ya pili hayazungumzii kabisa kwamba raia huyo lazima awe mwanachama wa chama cha kisiasa. Kutaka mgombea kuwa mwanachama wa chama cha kisiasa lakini sio akiwa mpiga kura ni hitilafu ya kisheria yenye kuonesha uonevu na dhuluma dhidi ya haki ya kikatiba ya raia.
Ingawa kifungu namba 8.-(1) katika katiba hiyo hiyo Sehemu ya pIli kinabainisha kwamba " Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayofuata
misingi ya demokrasia na haki ya kijamii, na kwa hiyo -
(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali
itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa
wananchi kwa mujibu wa Katiba hii;
(b) lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi;
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi;
(d) wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao
kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii " msimamo wa sasa wa serikali kutokubali mgombea huru unaonesha sio wananchi walio na haki na uhuru wa kuamua bali ni serikali. Ari iliyoko kwenye kifungu hicho haionekani katika maamuzi na vitendo vya serikali inayotakiwa kuisimamia katiba hiyo. Ari hiyo ingelikuwepo kutokana na kifungu hiki tu, serikali isingethubutu kupinga kuwepo kwa mgombea huru.
Watanzania kunyimwa haki ya kugombea uchaguzi kama wagombea huru hakuungwi mkono hata kidogo na kifungu Namba
12.-(1) ambacho kinabainisha wazi kwamba: " Binadamu wote huzaliwa huru, na wote ni sawa."
Na sehemu yake ya
(2) inaendelea: " Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na
kuthaminiwa utu wake."
Hali ilivyo sasa ni kuwa anayetaka kuwa mgombea huru hana haki wala usawa. Na ni pale tu serikali itakapopenda ndio atapata heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake.
Pamoja na kuwanyima watu uhuru wa kuwa wagombea huru bado serikali imeendelea kukubali kifungu Namba
15.-(1) kinachotangaza kuwa: " Kila mtu anayo haki ya kuwa huru na kuishi kama mtu huru.
Ambacho kinashadidiwa na kifungu kidogo cha
(2) kinachosema: " Kwa madhumuni ya kuhifadhi haki ya mtu kuwa huru na
kuishi kwa uhuru, itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote
kukamatwa, kufungwa, kufungiwa, kuwekwa kizuizini,
kuhamishwa kwa nguvu au kunyang'anywa uhuru wake ......."
Licha ya kauli hii serikali imeendelea kuwafungia watu kuwa wagombea huru na kuwahamisha kwa nguvu [kutoka kwenye kundi la wanaotaka kuwa wagombea na kuwaweka kwenye kundi la wapiga kura tu] watu na kuwanyang'anya uhuru wao wa kuwa wagombea huru katika chaguzi mbalimbali.
Vifungu vingine kama vile kile cha 16, 17, 18, 19, 20, 21, 22 na 31 vingelikuwa vinaeleweka vizuri na wanasheria na wabunge waliopo wangeligundua kosa linalofanyika kwa kuwanyima watu kuwa wagombea huru katika uchaguzi.
Mathalani katika kifungu Namba 16 kinazungumza haki ya faragha ambayo inaweza pia kutafsiriwa kama haki ya mtu kuwa peke yake kwa kuwa hataki au hapendi kushirikiana na watu wa aina fulani waliomo katika chama fulani.
Haki ya Uhuru wa mtu kwenda atokako, Uhuru wa Maoni na uhuru wa mawazo kama ilivyo katika kifungu Namba 17 na 18 havionekani kuzingatiwa pia katika msimamo wa serikali wa kuwazuria wagombea huru katika chaguzi mbalimbali.
Kifungu Namba
20.-(1) kinathibitisha kwamba: " Kila mtu anastahili kuwa huru, bila ya kuathiri sheria
za nchi, kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani,
kuchanganyika na kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo
hadharani, na hasa zaidi kuanzisha au kujiunga na vyama au
mashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi au
kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi mengineyo."
Kutokana na hayo hapo juu ni dhahiri kuwa serikali inakiuka kifungu hiki kwa sababu haiyumkiniki kwa mtaka kuwa mgombea huru kuwa anaathiri visivyo sheria za nchi. Ila kama kuna amri ya uonevu, kumnyima mtu haki yake na ukandamizaji.
Aidha kifungu kinachozungumzia Uhuru wa kushiriki shughuli za umma
na hususan Haki ya Kufanya Kazi ni kifungu kilicho bayana kikibainisha kwamba kwa muktadha wa kile tunachokizungumza kuwa uamuzi wa kuzuia wagombea huru ni uamuzi wa kumnyima mtu haki ya kushiriki shughuli za umma na kufanya kazi hasa kwa wale ambao wamekwishapita ngazi nne za mwanzo za msonge wa Maslow.
Hofu juu ya wagombea huru
Kufikia hapa tumegundua kuwa kuzuia kwa wagombea huru kikatiba ni kosa.
Swali la kujiuliza ni je, ni kwanini serikali za awamu mbalimbali za CCM zimegwaya kuruhusu wagombea huru.
Ninadiriki kusema kuwa udhaifu na ubovu wa chama hicho na serikali yake ndio sababu kubwa ya kukataliwa kwa wagombea huru.
Vile vile wakati wowote ule ambao chama kinafanya maamuzi ya kiajabu ajabu na yasiyo na maslahi kwa wananchi itakuwa ni rahisi kukiacha chama na mtu kuendelea na ubunge kama mbunge asiye na chama.
Kwa chama hili ni hatari, kwa nchi hili lina faida kubwa kwa kuwa linasafisha vyama na kuwaruhusu wenye uchungu na kiu ya maendeleo ya watu wao kufanya mambo yao bila kukwaza na upofu au uziwi au au umdwebedo au ulegelege au udhaifu wa chama husika.
Wagombea huru wana hatari kubwa ya kuwa kina Slaa au Mwakyembe mara mbili ya hawa waliopo.
Isitoshe kwa wale wenye uwezo wataweza kuleta maendeleo ya haraka zaidi katika majimbo yao kiasi cha vyama vingine kutokuwa na nafasi tena ya kushinda sehemu hizo mpaka mgombea huyo aache au afe.
Wagombea huru wanaweza kuwa chachu kuu ya kufanikisha kuzima kiu ya wakazi wa mikoa mbalimbali nchini kuwa na haki na uhuru wa kusimamia na kuendesha masuala yao ya kiuchumi na kijamii katika ngazi ya mkoa jambo litakaloondosha kumaktaimu kwa mikoa kadhaa inayokwaza na urasimu na umangimeza toka makao makuu ya mptio nchini.
Wagombea huru katika kipindi hiki cha vyama vingi wataweza kutoa changamoto mbalimbali kwa vyama vya kisiasa na serikali kiasi cha kurahisisha mno watu kutofautisha kati ya chuya na mchele safi.
Nimalizie sehemu hii kwa kurudia kusema kwamba katiba kimsingi inaruhusu kuwepo kwa mgombea huru. Lakini kutokana na maslahi ya kichama, kwa bahati mbaya wabunge wa huko siku za nyuma na mahakama wameshawishiwa visivyo kuwakataa bila sababu yoyote ya msingi. Msimamo huu ni mmoja kati ya ile inayochangia kudumaza demokrasia badala ya kukuza na kuimarisha demokrasia hapa Afrika.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
© 2009 Sammy W.I.Makilla
Mgombea huru ni raia yeyote katika nchi fulani anayegombea nafasi yoyote ile ya uongozi bila kuwa mwanachama wa chama fulani.
Katiba kwa kawaida huainisha wajibu na haki za watu kwa misingi ya matamko mbalimbali ya Haki za binadamu na nyinginezo na kisha hutoa haki kwa kila mtu katika misingi ya usawa, ikiwemo ile haki ya kupigiwa na kupiga kura. Baadhi ya nchi hapa Afrika , hata hivyo, zimeamua kuwadhulumu wananchi wao kwa kuwanyima watu wao haki ya kupigiwa kura kwa visingizio vya aina mbalimbali . Ni haki ya wananchi kudai na kuona kwamba wanakuwa na uhuru wa kupigiwa na kupiga kura. Na sio waruhusiwe tu na pengine kulazimishwa kupiga kura lakini wasiwe na haki ya kugombea nafasi mbalimbali za uongozi toka chin hadi juu katika nchi yao.
Uamuzi wa mtu kuwa mgombea huru husababishwa na mambo mbalimbali. Hufanya hivyo, aghalabu, kwa sababu anaamini kwamba viongozi wa vyama walipo ni bomu na hawawezi kufikisha jimbo au mkoa au nchi pale sehemu husika inapostahili. Wakati mwingine hukataa kuwa mwanachama wa chama fulani kwa sababu ya kiwango cha wizi na ufisadi anauona ndani ya chama husika. Aidha, huweza kukataa pia kuwa mgombea wa chama fulani kwa sababu anaamini kwamba vyama vilivyopo havitetei maslahi ya mwananchi bali maslahi binafsi ya viongozi wa vyama hivyo.
Vilevile, huweza kuamua hivyo kutokana na kutambua fika viongozi waliopo wamebeba na hawana uwezo wa kiakili, kifikira na kivitendo wa kuongoza watu na nchi.
Dhuluma kubwa inayofanywa na katiba iliyopo ni ile ya kumpa mtu haki ya kupiga kura [bila kujali ni mwanachama au sio mwanachama wa chama fulani] lakini wakati huo ikamnyima haki ya kupigiwa ila tu mtu anapokuwa ni mwanachama wa chama cha kisiasa kilichosajiliwa.
Ni dhambi isiyo na msamaha kwa mwananchi yoyote kushiriki katika vitendo vya uhuni, ubabe, unyang'anyi wa haki na uhuru wa mtu kupitia katika kuichezea na kuivuruga katiba kwa maslahi ya wachache au chama fulani cha kisiasa. Ndivyo ilivyo pia katika kupora haki ya mgombea huru.
Hadi wa leo hapajaruhusiwa kuwa na mgombea huru, mathalani, nchini Tanzania. Hata hivyo, mtu akiangalia kwa makini atagundua kuwa amri ya kukataa wagombea huru haiungwi mkono na vifungu mbalimbali vya katiba.
Katika sura hii tutajaribu kulionesha hilo huku tukitaraji kuwa wanasheria na wapigania haki na uhuru wa binadamu kwa kushirikiana na Tume ya Uchaguzi wataliangalia jambo hili kwa macho mapya na kuondoa dhuluma wanayofanyiwa wale wanaotaka kufikia hatua ya juu katika msonge wa mahitaji ya binadamu kama ilivyoainishwa na Abraham Maslow.
Mitihani kwa wasiokubali vyama vilivyopo
Hali ilivyo hivi sasa ni kwamba mwananchi au mwanasiasa anayetaka kuwa mgombea huru anaiweka nchi au yeye mwenyewe anajikuta katika mitihani ifuatayo:
a) Kama ni mwanachama wa chama fulani anajikuta kifungoni pale anapokuwa kakiona chama ni kichafu na kibovu kiasi cha kutisha;
b) Anajikuta ni mnafiki kwa nafsi yake na anaowawakilisha;
c) Analazimishwa kutekeleza sera na mambo asiyokubaliana nao;
d) Ananyimwa nafasi ya kuchangia ubunifu, mawazo mapya na kutumika kwa fursa za maendeleo au kutatua matatizo ya wananchi kwa njia bora na yenye manufaa kwa wananchi zaidi kuliko inavyofanywa na chama au vyama;
e) Anajikuta hawezi kutumia haki zake nyingi alizopewa kikatiba kama raia;
f) Anajikuta kwamba ingawa yeye ni bora kuliko wengi wengine ananyimwa nafasi ya kuongoza nchi;
g) Inafikia hatua nchi inaongozwa na viongozi dhaifu, wezi na wabovu kutokana na vyama kuwazuia au kuwapiga vita watu walio bora kuliko wao;
h) Kwa kuwa viongozi hao (wanaowazuia wagombea huru) wanajua hakuna wanachokifanya na hawajiamini wanaanza kujiingiza kwenye vitendo vya kuimaliza nchi kiuchumi na kijamii kama bima yao ya baadaye endapo wataondolewa madarakani kwa njia yoyote ile. Njia hizo za kuifukarisha zaidi nchi ni pamoja na kushirikiana na watu wengine kuibia benki kuu na serikali au kuingia mikataba ya kiwizi wizi au kutumia fedha zilizopangwa kwa maendeleo ya wengi kwa maslahi binafsi kwa wachache au ya chama chao.
Kulazimisha uanachama ni kuvunja katiba
Kuwalazimisha watu kuwa wanachama wa chama cha kisiasa ni kosa. Kumnyima mtu haki ya kupigiwa kura eti kwa sababu sio mwanachama wa chama cha kisiasa nalo ni kosa. Na haya yote yanaweza kushuhudiwa na vifungu mbalimbali vya Katiba ya Jamhuri ya Muungano [1998] hususan Sura ya Kwanza, Sehemu ya Kwanza hadi ya tatu, kama tutakavyoonesha hapa chini.
Kifungu namba 5.-(1) cha katiba ya JMT kiasema "Kila raia wa Tanzania aliyetimiza umri wa miaka
kumi na minane anayo haki ya kupiga kura katika uchaguzi
unaofaywa Tanzania na wananchi. Na haki hii itatumiwa kwa
kufuata masharti ya ibara ndogo ya (2) pamoja na masharti
mengineyo ya Katiba hii na ya Sheria inayotumika nchini
Tanzania kuhusu mambo ya uchaguzi."
Masharti yaliyomo katika ibara hiyo ya pili hayazungumzii kabisa kwamba raia huyo lazima awe mwanachama wa chama cha kisiasa. Kutaka mgombea kuwa mwanachama wa chama cha kisiasa lakini sio akiwa mpiga kura ni hitilafu ya kisheria yenye kuonesha uonevu na dhuluma dhidi ya haki ya kikatiba ya raia.
Ingawa kifungu namba 8.-(1) katika katiba hiyo hiyo Sehemu ya pIli kinabainisha kwamba " Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni Nchi inayofuata
misingi ya demokrasia na haki ya kijamii, na kwa hiyo -
(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka yote, na Serikali
itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa
wananchi kwa mujibu wa Katiba hii;
(b) lengo kuu la serikali litakuwa ni ustawi wa wananchi;
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi;
(d) wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali yao
kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii " msimamo wa sasa wa serikali kutokubali mgombea huru unaonesha sio wananchi walio na haki na uhuru wa kuamua bali ni serikali. Ari iliyoko kwenye kifungu hicho haionekani katika maamuzi na vitendo vya serikali inayotakiwa kuisimamia katiba hiyo. Ari hiyo ingelikuwepo kutokana na kifungu hiki tu, serikali isingethubutu kupinga kuwepo kwa mgombea huru.
Watanzania kunyimwa haki ya kugombea uchaguzi kama wagombea huru hakuungwi mkono hata kidogo na kifungu Namba
12.-(1) ambacho kinabainisha wazi kwamba: " Binadamu wote huzaliwa huru, na wote ni sawa."
Na sehemu yake ya
(2) inaendelea: " Kila mtu anastahili heshima ya kutambuliwa na
kuthaminiwa utu wake."
Hali ilivyo sasa ni kuwa anayetaka kuwa mgombea huru hana haki wala usawa. Na ni pale tu serikali itakapopenda ndio atapata heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake.
Pamoja na kuwanyima watu uhuru wa kuwa wagombea huru bado serikali imeendelea kukubali kifungu Namba
15.-(1) kinachotangaza kuwa: " Kila mtu anayo haki ya kuwa huru na kuishi kama mtu huru.
Ambacho kinashadidiwa na kifungu kidogo cha
(2) kinachosema: " Kwa madhumuni ya kuhifadhi haki ya mtu kuwa huru na
kuishi kwa uhuru, itakuwa ni marufuku kwa mtu yeyote
kukamatwa, kufungwa, kufungiwa, kuwekwa kizuizini,
kuhamishwa kwa nguvu au kunyang'anywa uhuru wake ......."
Licha ya kauli hii serikali imeendelea kuwafungia watu kuwa wagombea huru na kuwahamisha kwa nguvu [kutoka kwenye kundi la wanaotaka kuwa wagombea na kuwaweka kwenye kundi la wapiga kura tu] watu na kuwanyang'anya uhuru wao wa kuwa wagombea huru katika chaguzi mbalimbali.
Vifungu vingine kama vile kile cha 16, 17, 18, 19, 20, 21, 22 na 31 vingelikuwa vinaeleweka vizuri na wanasheria na wabunge waliopo wangeligundua kosa linalofanyika kwa kuwanyima watu kuwa wagombea huru katika uchaguzi.
Mathalani katika kifungu Namba 16 kinazungumza haki ya faragha ambayo inaweza pia kutafsiriwa kama haki ya mtu kuwa peke yake kwa kuwa hataki au hapendi kushirikiana na watu wa aina fulani waliomo katika chama fulani.
Haki ya Uhuru wa mtu kwenda atokako, Uhuru wa Maoni na uhuru wa mawazo kama ilivyo katika kifungu Namba 17 na 18 havionekani kuzingatiwa pia katika msimamo wa serikali wa kuwazuria wagombea huru katika chaguzi mbalimbali.
Kifungu Namba
20.-(1) kinathibitisha kwamba: " Kila mtu anastahili kuwa huru, bila ya kuathiri sheria
za nchi, kukutana na watu wengine kwa hiari yake na kwa amani,
kuchanganyika na kushirikiana na watu wengine, kutoa mawazo
hadharani, na hasa zaidi kuanzisha au kujiunga na vyama au
mashirika yaliyoanzishwa kwa madhumuni ya kuhifadhi au
kuendeleza imani au maslahi yake au maslahi mengineyo."
Kutokana na hayo hapo juu ni dhahiri kuwa serikali inakiuka kifungu hiki kwa sababu haiyumkiniki kwa mtaka kuwa mgombea huru kuwa anaathiri visivyo sheria za nchi. Ila kama kuna amri ya uonevu, kumnyima mtu haki yake na ukandamizaji.
Aidha kifungu kinachozungumzia Uhuru wa kushiriki shughuli za umma
na hususan Haki ya Kufanya Kazi ni kifungu kilicho bayana kikibainisha kwamba kwa muktadha wa kile tunachokizungumza kuwa uamuzi wa kuzuia wagombea huru ni uamuzi wa kumnyima mtu haki ya kushiriki shughuli za umma na kufanya kazi hasa kwa wale ambao wamekwishapita ngazi nne za mwanzo za msonge wa Maslow.
Hofu juu ya wagombea huru
Kufikia hapa tumegundua kuwa kuzuia kwa wagombea huru kikatiba ni kosa.
Swali la kujiuliza ni je, ni kwanini serikali za awamu mbalimbali za CCM zimegwaya kuruhusu wagombea huru.
Ninadiriki kusema kuwa udhaifu na ubovu wa chama hicho na serikali yake ndio sababu kubwa ya kukataliwa kwa wagombea huru.
Vile vile wakati wowote ule ambao chama kinafanya maamuzi ya kiajabu ajabu na yasiyo na maslahi kwa wananchi itakuwa ni rahisi kukiacha chama na mtu kuendelea na ubunge kama mbunge asiye na chama.
Kwa chama hili ni hatari, kwa nchi hili lina faida kubwa kwa kuwa linasafisha vyama na kuwaruhusu wenye uchungu na kiu ya maendeleo ya watu wao kufanya mambo yao bila kukwaza na upofu au uziwi au au umdwebedo au ulegelege au udhaifu wa chama husika.
Wagombea huru wana hatari kubwa ya kuwa kina Slaa au Mwakyembe mara mbili ya hawa waliopo.
Isitoshe kwa wale wenye uwezo wataweza kuleta maendeleo ya haraka zaidi katika majimbo yao kiasi cha vyama vingine kutokuwa na nafasi tena ya kushinda sehemu hizo mpaka mgombea huyo aache au afe.
Wagombea huru wanaweza kuwa chachu kuu ya kufanikisha kuzima kiu ya wakazi wa mikoa mbalimbali nchini kuwa na haki na uhuru wa kusimamia na kuendesha masuala yao ya kiuchumi na kijamii katika ngazi ya mkoa jambo litakaloondosha kumaktaimu kwa mikoa kadhaa inayokwaza na urasimu na umangimeza toka makao makuu ya mptio nchini.
Wagombea huru katika kipindi hiki cha vyama vingi wataweza kutoa changamoto mbalimbali kwa vyama vya kisiasa na serikali kiasi cha kurahisisha mno watu kutofautisha kati ya chuya na mchele safi.
Nimalizie sehemu hii kwa kurudia kusema kwamba katiba kimsingi inaruhusu kuwepo kwa mgombea huru. Lakini kutokana na maslahi ya kichama, kwa bahati mbaya wabunge wa huko siku za nyuma na mahakama wameshawishiwa visivyo kuwakataa bila sababu yoyote ya msingi. Msimamo huu ni mmoja kati ya ile inayochangia kudumaza demokrasia badala ya kukuza na kuimarisha demokrasia hapa Afrika.
© 2009 Sammy W.I.Makilla
© 2009 Sammy W.I.Makilla
Subscribe to:
Posts (Atom)
