Sunday, June 15, 2008

8. Demokrasia, utendaji na tathmini ya kazi

KUNA maswali kadhaa kuhusiana na Rasilimali Watu [Human Resource] yanayopaswa kujibiwa ili tuwe na uwezo wa kujenga demokrasia na taifa imara kiuchumi.

Je, elimu na ujuzi watu wetu walio nao sasa vinawatosha kusimamia ujenzi wa demokrasia nchini?

Kama panahitajika elimu na ujuzi zaidi au tofauti ni ujuzi na elimu gani hizo? Ni nani anayeweza kutupatia ujuzi na elimu hizo? Je, gharama ya kukosa elimu na ujuzi huo itakuwa ni ndogo ukifananisha na kuwa na elimu na ujuzi huo?

Hivi sasa tunajua ni mambo gani ambayo kila waziri, naibu waziri, katibu mkuu, mkuu wa idara, mkuu wa mkoa, mkuu wa wilaya na watumishi wengine wa serikali wanayotakiwa kufanya. Tunayachagua vipi? Ni kigezo tosha cha utendaji kazi? Kuna utafiti wowote uliofanyika na pengine kulinganisha viongozi wetu na watu wa taifa lingine ambalo labda lina utendaji bora zaidi kiutumishi?

Ni kwa namna na njia gani tunazoweza kuzitumia kuwatathmini viongozi waliopo? Tunatumia vipindi gani? Na kama mtu akionekana anapwaya afanywe nini?

Palikuwa na hatua za kuanzisha kutumika kwa mfumo wa tathmini wazi [OPRAS]-lakini inaelekea umekwama mahala fulani. Lakini penda tusipende hatuwezi kuendelea na hatuwezi kujenga demokrasia bila ya kuwa na menejimenti ya utendaji na uwajibikaji [Perfomance Management] -chombo pekee kinachoweza kutenganisha kati ya takataka na nafaka halisi..

Demokrasia sio mfumo unaoweza kujengwa na wababishaji, waigizaji na watu wanaofanya utani na ujinga, umasikini na maradhi kwa hasara ya watu wetu.
***

No comments: