Sunday, June 15, 2008

16. Demokrasia na matumizi ya mikopo katika maendeleo.

NI DHAHIRI kuwa mara kadhaa nchi za Kiafrika zinakopa na kisha fedha hizo hazitumiki katika miradi husika.

Fedha inaweza kuhamishwa wakati wowote kwa amri ya mtu mmoja na ikatumika vibaya au vizuri bila watu kujua kinachoendelea.

Demokrasia mikoani itahakikisha kuwa kila mkopo unaohusu mkoa unatumika kweli kuleta maendeleo ya wakazi wa mkoa husika na sio vinginevyo.

Pengine utafika wakati pia ambapo serikali za nje, benki za ndani na nje na wafadhili wengine wanaweza kuingia mkataba moja kwa moja na waziri mkuu wa mkoa husika na hivyo kuhakikisha fedha yote inafika pale inapohitajika kufika.

Mazungumzo na wageni kadhaa imeonesha kuna 'walakini' mkubwa katika mfumo wa kidemokrasia kuikabidhi serikali ya nchi fedha zote za msaada na mkopo. Kutokana na 'lakini' hii sasa hivi wageni wengi wanaangalia jinsi wanavyoweza kufadhili mikoa, miradi na watu binafsi ili kuharakisha kasi ya kuondokana na umasikini Afrika. Tukiwa na serikali za mikoa zenye madaraka ya kujiamulia masuala yao ya kiuchumi na kijamii kazi hii itakuwa rahisi mno.
***

No comments: