Sunday, June 15, 2008

13. Demokrasia, polisi na raia

AFRIKA wakati mwingine inachekesha. Pakiwa sio wakati wa uchaguzi askari wetu wanashindwa kulinda usalama wa raia na mali zao. Lakini, ghafla bin vuu, uchaguzi au ugomvi wa kisiasa ukizuka askari polisi lukuki wanatoka hukowanakotokana na kuifanya kazi ya kuwalinda walio madarakani kwa namna ambayo wanawashinda hata polisi wa nchi za Magharibi.


Swali hapa ni, je, polisi kazi yao ni kuwalinda wale walioko madarakani au raia wote bila kubagua.



Ni nini kitakachotokea kama anayelindwa ni mwizi wa kura au kitu kingine?



Je, haitachekesha na pengine kuhuzunisha sana kuona mtu kaibiwa kisha mwizi ndiye anayemsakizia mbwa amuume au amuue eti?



Je, kuna nafasi katika mfumo wetu kuwa na jeshi la polisi ambalo haliwajibiki kwa aliyeko madarakani bali kwa raia. Ni nani achague Mkuu wa Polisi-Bunge au Rais?



Jibu moja kwa moja ni kuwa ili kuwe na haki ni lazima Mkuu wa Polisi achaguliwe na bunge kwa niaba ya wale wanaowawakiisha.



Kwa namna hii kiongozi huyo hatamuogopa mtu au chama tawala katika kufanya maamuzi yake. Na hii ndio demokrasia katika medani ya usalama wa nchi na watu wake.

***

No comments: