Sunday, June 15, 2008

18. Demokrasia na Matumizi mabaya ya fedha na kusahaulika serikali za mitaa

TATIZO la serikali kuu kuwa katika mji mmoja ni kwamba fedha nyingi za matumizi ya serikali huwa zinawanufaisha wakazi wa jiji husika na sio wakazi wa miji mingine.

Aidha, serikali katika mji mkuu hujiona ina majukumu makubwa ya siasa za nje na kwa kiasi kikubwa fedha nyingi hutumika katika masuala ya nje ukilinganisha na kile kinachotumika katika serikali za miji na mikoa nje ya makao makuu.

Demokrasia ya kweli haiwezekani kama serikali kuu nzima itaendelea kuwa katika mji na mkoa mmoja.

Kwa kufuata nadharia ya siasa na uchumi wa kisekta wakati umefika sasa wa wizara kugawanya kulingana na shughuli wanazofanya katika kanda mbalimbali.

Hii ina maana Dar es salaam inaweza ikawa na Makao Makuu ya Wizara nne au tano; Mwanza wizara nne au tano; Arusha Wizara nne au tano; Mbeya Wizara nne au tano; Dodoma Wizara nne au tano na hivyo kuifaidisha miji hiyo na kanda nzima hususan katika fedha za matumizi ya serikali na masurufu ya watumishi wake.

Mifano ipo ya kuwa na jengo moja linaloweza kuweka Makao Makuu ya Wizara tano,kumi au serikali nzima. Tuige lile linalofaa.

Mabadiliko haya yatawezesha pia serikali kuwa inaangalia kwa karibu zaidi maendeleo ya ndani ya nje badala ya kujishughulisha na mambo mengi madogo madogo ya nje lakini yenye gharama nyingi na kubwa lakini hakuna manufaa yanayolingana na matumizi yanayofanyika mwaka hadi mwaka.
***

No comments: