Sunday, June 15, 2008

10. Demokrasia na uwekezaji kaika sekta za uchumi na jamii

LENGO mojawapo muhimu la Demokrasia ni kuhakikisha kuwa watu wanakuwa na uhuru na haki ya kufanya maamuzi yote katika masuala mbalimbali yanayogusa maisha yao.

Jambo moja muhimu ni hali yao ya maisha. Na hali ya maisha ya mtu wa Arumeru hadi Zanzibar au Amboni mpaka Zambia haiwezi kuamuliwa na mtu aliyeko Dar es salaam au Lusaka.

Maamuzi lazima yafanyike pale pale watu walipona makazi yao maana wao ndio wako katika fursa nzuri ya kuamua ni lipi muhimu kulifanya au kulipata katika wakati uliopo.

Na demokrasia ya kweli haitegemei fedha za msaada. Demokrasia ya kweli inategemea zaidi kutumia akili za watu kupata ufumbuzi wa matatizo na matarajio yao ya kila wakati.
Kwa miaka kadhaa sasa, mathalani, nchi nyingi zimeshindwa angalau kukarabati na kutengeneza barabara na reli tulizoachiwa na wakoloni au viongozi wetu wa mwanzo tulizopata kwa njia ya mikopo au msaada. Achilia mbali kujenga miundonmbinu mipya.

Ili kuwa na demokrasia ya kweli ni muhimu Afrika iweze angalau kuwa na akili ya kuhakikisha hatupotezi hata hiki tulicho nacho kwa sera zinazolenga kuwa na uwezo wa watu na rasilimali kwa ajili ya ukarabati na uboreshaji kile kilichopo.

Pengine, hata ufanyaji kazi wetu unapaswa ubadilike.

Hiki katika miaka hii ya sayansi na teknolojia Waziri wa Miundombinu anastahili kuwa kwenye ofisi iliyoko kwenye jengo fulani au kwenye hema kando ya barabara au reli au bwawa linalojengwa? Au basi maalum lenye uwezo wa kuwa na ofisi na sehemu ya kuishi waziri huyo na wasaidizi wake kadhaa?

Bila shaka Waziri akiendelea kukaa ofisini kila mwaka kama sio kila mwezi tutaendelea kupata taarifa mbovu kuhusu

Ujenzi wa barabara, reli, daraja, bwawa, kiwanja cha ndege, bandari na kadhalika. Watakaofanya kazi kwa kutania wataendela kufanya hivyo na watakaokwiba wataendelea kufanya hivyo.i

Ni lazima tuwe na utaratibu fulani wa kuhakikisha kuwa asilimia fulani ya kipato cha taifa inatumika katika ukarabati na kuhifadhi kile kilichopo wakati huo na hasa katika miundombinu na huduma za jamii.
***

No comments: