Ni lazima mahesabu ya serikali, wizara zote, miji yote, Benki kuu na taasisi nyingine muhimu yawe wazi na yanayoweza kufikiwa na yeyote anayetaka kuyachambua na kuyafanyia upembuzi wa kina.
Katika hili haki na uhuru wa mwananchi kufikia nyaraka za serikali lazima iwepo na itumike kwa jinsi mtu anavyotaka ili mradi ndani ya wigo wa kisheria na kikatiba.
Pengine wakati wa kuwa na SERIKALI YA VITABU WAZI [OPEN BOOK GOVERNMENT] kwa maana ya kwamba tutakuwa na nafasi ya kuona kila baada ya muda fulani serikali imepata nini na imetumia nini na sisi kuweza kuipongeza au kuikosea umefika?
Hapa Tanzania toka zoezi la ubianfsishaji [mali ambazo kinadharia zilikuwa zetu wote] hatujui ni fedha kiasi gani ilipatikana, imekwenda wapi na sisi tuliokuwa na HISA KATIKA TAIFA LA KIJAMAA tunaambulia nini?
Ni muhimu kukumbuka kuwa Karl Marx alikwishatutahadharisha juu ya kutumia mfumo wa demokrasia kama mfumo wa kujenga jamii ya kistaarabu. Yeye alisema kwamba: 'Mfumo huu ni mzuri tu mpaka pale watu wanapogundua kwamba wanaweza kuifilisi benki kuu na mtu asiwafanye lolote!'
Demokrasia ndio. Lakini lazima ifungamane na mifumo ya kulinda watu na nchi dhidi ya uovu na hasara zinazoweza kusababishwa na wajanja wachache katika jamii wakishirikiana na mabwana zao wa nje.
***
Sunday, June 15, 2008
Subscribe to:
Post Comments (Atom)

No comments:
Post a Comment